Ubunifu unaiua Sahara Media Group

De Opera

JF-Expert Member
May 23, 2013
480
927
Wapwa, kuna taarifa inasambaa kuhusu mgomo wa wafanyakazi Sahara Media Group, kwamba hawajalipwa mishahara miezi mitatu sasa sababu kampuni haina hela.

Mi huwa nawaza Sahara ni media kubwa na ni kongwe sana ila program zake ni local, kitu ambacho hakiwavutii wanamatangazo. Quality ya vipindi iko chini. Program manager hana budi kuamka, media itakufa.
 
Hivi ni kweli huo mgomo upo? Mbona leo nimesikiliza kipindi cha michezo saa mbili asubuhi?

Kuna kadada kanaitwa Mwanaunique kana sauti nzuri sana, dah! sijui itakuwaje!!
Kale kadada kapo vizuri ila kamekutana na media haijachangamka.

Kwanza hapa mwanza Sahara media ingekuwa ni ya kukutana nayo kila kona ya mtaa. Sema ndio hivo imelala.
 
Katika zama hizi za MEDIA CONVERGENCE mainstream media aka VYOMBO VYA HABARI VYA UTANGAZAJI PENDWA yaani Redio na Television vikishindwa kuendana na haya mabadiliko upo uwezekano wa kupotea na kushindwa kujiendesha kabisa.

Ni muhimu media owners wafahamu kwamba kuna change ya paradigms za namna hadhira inavyokula maudhui.

Mtindo wa sasa ni wa ushindani na uuzaji wa maudhui yenye ubora wa hali ya juu mfano wa NETFLIX, BOOMPLAY, SPOTIFY, MILLARD AYO nk

Pia new media inaenda na mtindo wa kileo wa kuwafuata audience waliko.

Pia wanahitaji content ya maana mfano football, na other premiere shows.

Shangaa kwamba redio za FM kubwa Bongo kwenye radio garden tu humo, hawamo!!

Kingine ni UBORA UBORA UBORA, Kukosa ubora ni tatizo kubwa kwa majority ya broadcast media za Tanzania both radio na TV.

AZAM MEDIA imekuja kuonyesha tofauti ya namna UBORA unavyohitajiwa sokoni; pia, MULTICHOICE pamoja na gharama zao kuwa kubwa bado wanaandamiwa. ZAMA za kutazama Picha zilizofubaa zilishapitwa.

MEDIA OWNERS Wabadilike; wakubaliane na nini soko la sasa linataka.

BROADCAST CONTENT kibongobongo HAINOGI sababu kubwa ni UBORA na kushindwa kuwafikia Hadhira waliko yaani kwenye mtandao wa intaneti.

UBORA na KWENDA NA MABADILIKO yaliyopo sokoni.
 
Katika zama hizi za MEDIA CONVERGENCE mainstream media aka VYOMBO VYA HABARI VYA UTANGAZAJI PENDWA yani Redio na Television vikishindwa kuendana na haya mabadiliko upo uwezekano wa kupotea na kushindwa kujiendesha kabisa.

Ni muhimu media owners wafahamu kwamba kuna change ya paradigms za namna hadhira inavyokula maudhui.

Mtindo wa sasa ni wa ushindani na uuzaji wa maudhui mfano wa NETFLIX, BOOMPLAY, SPOTIFY nk pia online media inadoenda na kuwafuata audience walk.

UBORA UBORA UBORA pia ni tatizo kubwa kwa majority ya broadcast media Tanzania.

AZAM MEDIA imekuja kuonyesha tofauti ya namna UBORA unavyohitajiwa sokoni; pia, MULTICHOICE pamoja na gharama zao kuwa kubwa bado wanaandamiwa. ZAMA za kutazama Picha zilizofubaa zilishapitwa.

MEDIA OWNERS Wabadilike; wakubaliane na mini soko la sasa linataka.

BROADCAST CONTENT kibongobongo HAINOGI sababu kubwa ni UBORA na kushindwa kuwafikia Hadhira waliko yaani kwenye mtandao wa intaneti.

UBORA na KWENDA NA MABADILIKO yaliyopo sokoni.
Postive point kaka. Kuna redio moja iko kule ngara, siku moja nilikuwa nasikiliza nikaamua tu kuzima redio. 😂 yaani mtangazaji ana bonge la vocal jalala likasome! Nikajisemea 'Huyu mtangazaji aliamua kabisa kuwa mtangazaji, na shuleni wakakubali kabisa wakamtunuku cheti'!?
 
unaitamani kivp mkuu
Huwa natamani kuwa mmoja wa mwendesha vipindi pale kama Radio Free, au Star Tv. Maana Startv huwa naona quality ya content zao yaani kwa sisi maengineer wa maudhui/Content creators tunapata presha ya moyo kuona quality kama ile inaenda kwa watazamaji.
 
Huwa natamani kuwa mmoja wa mwendesha vipindi pale kama Radio Free, au Star Tv. Maana Startv huwa naona quality ya content zao yaani kwa sisi maengineer wa maudhui/Content creators tunapata presha ya moyo kuona quality kama ile inaenda kwa watazamaji.
Kama expert pia inabidi uangalie na soko linataka nini.
Wewe unaweza kuangalia quality ya picha, colour grading, quality ya sauti, graphics na issue zingine technical, ukainvest huko kwa nguvu zote kumbe watazamaji wako wanahitaji setting na quality ya mkojani.

Kuwa too professional kwenye soko la bongo ni risk pia. Kama wewe ni content creator, hili nalo ukalitizame
 
Wapwa, kuna taarifa inasambaa kuhusu mgomo wa wafanyakazi Sahara Media Group, kwamba hawajalipwa mishahara miezi mitatu sasa sababu kampuni haina hela.

Mi huwa nawaza Sahara ni media kubwa na ni kongwe sana ila program zake ni local, kitu ambacho hakiwavutii wanamatangazo. Quality ya vipindi iko chini. Program manager hana budi kuamka, media itakufa.
mimi nakupinga,mimi binafsi naisikiliza zaidi RFA...na ninaiona ni bora kuliko radio yoyote hata TZ!!
 
mimi nakupinga,mimi binafsi naisikiliza zaidi RFA...na ninaiona ni bora kuliko radio yoyote hata TZ!!
kaka, radio free ya kina Kidbwoy kuja mpaka kwa wale mabinti wenye sauti taamu kina Rahabu Fred, Elika Elias, Glory Robinson, Froza Muhando, ndio ilikuwa moto!

Kaka unaumri gani umeanza kusikiliza radio free?, maana mimi nimesikiliza hii redio toka zamani kipindi hiko hizi FM redio hazikuwa kiviile, ukifungua FM Band unakutana na chwaaaaaah😁. Tulikuwa tunatumia masafa ya kati (AM Band), na penyewe kushika hadi eneo liwe zuri. Ilikuwa mpaka usubiri jioni ndio inaanza kushika kwa mbali then unasikiliza hadi asubuhi kuanzia saa nne nne hivi inapotea tena.
 
Kama expert pia inabidi uangalie na soko linataka nini.
Wewe unaweza kuangalia quality ya picha, colour grading, quality ya sauti, graphics na issue zingine technical, ukainvest huko kwa nguvu zote kumbe watazamaji wako wanahitaji setting na quality ya mkojani.

Kuwa too professional kwenye soko la bongo ni risk pia. Kama wewe ni content creator, hili nalo ukalitizame
Hapo umenena kaka! 😂
Watu wanatembea na upepo! 😆
 
Back
Top Bottom