wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 24,709
- 26,829
Ukitokea Kimara kama unapita juu kwenda mjini pale mwisho flyover inakoishia mbele kidogo kuna mtaa (traffic light). Hii taa kuna muda zinafanya kunakuwa na foleni hadi juu kule kwenye flyover kabisa. Leo asubuhi kulikuwa na foleni hadi mwanzo wa daraja lenyewe (Tanesco) hii ni kwa yanayoenda tu mjini.
Mamlaka husika tunomba kama mfanye mpango wa kutatua hili au kama kuna uwezekano magari yanayopita juu kufika pale stendi ya mkoa yanyooshe au kama kuna magari yanayotoka Kimara kama yanaenda kuingia Ubungo stendi yawe yanapita chini tu; haina haja yapite juu alafu yakifika mbele yanaenda kusimama kusubiri taa ziruhusu alafu huku nyuma yanasababiha foleni.
Ni hayo tu, asanteni.
Maendeleo hayana chama.
Mamlaka husika tunomba kama mfanye mpango wa kutatua hili au kama kuna uwezekano magari yanayopita juu kufika pale stendi ya mkoa yanyooshe au kama kuna magari yanayotoka Kimara kama yanaenda kuingia Ubungo stendi yawe yanapita chini tu; haina haja yapite juu alafu yakifika mbele yanaenda kusimama kusubiri taa ziruhusu alafu huku nyuma yanasababiha foleni.
Ni hayo tu, asanteni.
Maendeleo hayana chama.