UBUNGO, DAR: Machinga wapewa siku 3 waondoke

UBUNGO, DAR: Machinga wapewa siku 3 waondoke

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,091
DAR: Serikali yatoa siku 3 kwa wafanyabiashara ndogondogo wa eneo la Ubungo wawe wameondoka eneo hilo ili kupisha ujenzi wa barabara za juu.

Mradi huo wa barabara za juu(flyover) unatarajiwa kuanza hivi karibuni baada ya serikali kukamilisha taratibu za utoaji tenda kwa kandarasi ya Ujenzi.

c648c3ea918c605ad8abeee2a8b66617.jpg


UBUNGO.jpg



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa najaribu sana kuwaza......
Kwa jinsi serikali inavyo wa disturb wakazi wa Daslam......
What if wakiamua kuhama jiji na kuelekea kwenye mikoa mingine isiyo na bugudha.....
Hapa nawaza tu
 
DAR: Serikali yatoa siku 3 kwa wafanyabiashara ndogondogo wa eneo la Ubungo wawe wameondoka eneo hilo ili kupisha ujenzi wa barabara za juu.

Mradi huo wa barabara za juu(flyover) unatarajiwa kuanza hivi karibuni baada ya serikali kukamilisha taratibu za utoaji tenda kwa kandarasi ya Ujenzi.

c648c3ea918c605ad8abeee2a8b66617.jpg
http://
www.jamiiforums.com/mobile-gallery/9256c56d5fe5d8c19dc19725397ba67a.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
Vijana nchi hii sijui wamekosea nini, wanachukuliwa kama MAJAMBAZI ?

- Waliosoma hawapewi ajira ?
- Wakiwa machinga wanafukuzwa kila leo na polisi ?
- Wakifanya biashara zao ziwe rasmi hawapewi TAX HOLIDAY wala GRACE PERIOD. Hata kabla ya faida wanakabwa na TRA, TFDA, NEMC, OSHA, FIRE, BRELA, COSOTA etc

- Hivi vijana wa nchi hii WAISHI Vipi ?
 
Walishapewa taarifa mapema kuhama sehemu hiyo kilichofanyika Leo ni Meya kwenda kufanya ustaarabu kuwakumbusha jukumu lao la kuhama kabla ya kuondolewa kwa nguvu.....

Hakuna mtu anayeonewa kwenye sakata la hapo ubungo maana toka mwaka Jana taarifa za ujenzi huo walikua nayo...
 
Tatizo ni kwanini serikali hahikutenga sehemu ya wamachinga.
Mradi wa flyover ndio unawakumbusha mwazo walifanya makosa
Vibanda vyao vinahamishika ingekuwa walijenga ni sawa....halafu wakiandaliwaga sehemu huwa hawaendi.
 
Huwa najaribu sana kuwaza......
Kwa jinsi serikali inavyo wa disturb wakazi wa Daslam......
What if wakiamua kuhama jiji na kuelekea kwenye mikoa mingine isiyo na bugudha.....
Hapa nawaza tu
Sasa wewe mkuu hutaki hizo flyover sijengwe hapo? Au unajua kupinga tu kila kitu?
 
Back
Top Bottom