Uboreshwaji wa data za wanandoa hasa kwa dini ya Kikristo

Uboreshwaji wa data za wanandoa hasa kwa dini ya Kikristo

Msingi wa ndoa ni uaminifu, database ni wewe na mkeo, acheni janja janja.
 
Habari..

Kumekuwa na udanganyifu kwenye baadhi ya ndoa za kikristo. Kwa sheria na taratibu zao imeruhusiwa ndoa moja tu. (Nyingine zitafungwa ikiwa mwanandoa mmoja amefariki au ndoa kubatilishwa na kanisa)

Nimeshahudia kesi za watu watatu wakristo, mmoja alifunga ndoa na mwanamke ambaye alishafunga ndoa mkoani Kilimanjaro na baadae kuamia Dar Es Salaam. Mwanamke alidanganya kuwa hakuwahi kuolewa. Baada ya kesi kuunguruma- ndoa ilibatilishwa.

Pia kuna ndoa mbili wanaume wamefunga ndoa mikoani (nje ya dar), baadae wakagundulika kuwa walishafunga ndoa.

Ushauri: ingekuwa vyema swala La ndoa lingewekwa kwenye mtandao. Taarifa za ndoa zingekuwa kama kwenye google sheet ili taarifa ziweze kuonekana katika makanisa. Wachungaji na mapadri wapewe access ya hiyo program ili kuondoa duplicate.
RITA inatakiwa aidha iunder upya, imegwe ili issue za vizazi na vifo zijitegemee kwa taasisi yake na issue za ndoa na talaka, kivyake, na issue za mirathi na udhamini kivyake. leo hii wakristo wengi tu wana ndoa na mke yupo hai ila wanaenda bomani na kufunga ndoa na mwingine na wanaishi na mitala, wengi sana tunawajua. ilitegemewa, kama mtu ameshafunga ndoa, database ionyeshe, asipate cheti kingine, database ionyeshe huyu alishafunga ndoa na hajaivunja ile ya awali.

kwenye vyeti vya kuzaliwa nako, unaweza kupata hata kumi ukiamua, kila mkoa ukienda unapata na msajili mkuu hajui kama vimejirudia. kwenye vifo kuna watu wanauawa wakati wapo hai, wengi sana.
 
Hilo swala linaisha karibuni maana lazima mtu awe na NIDA ndo unaandikishwa
 
Amri ya kuvunja ndoa zote inatolewa na Mahakama tu, hakuna kanisa, sinagogi, hema wala msikiti unaoweza kutoa hiyo amri na ndoa zote zinavunjwa na msajili wa ndoa ambaye ndie mtekelezaji wa hiyo amri ya Mahakama.

Tatizo watu wengi wanafikiri ndoa za kikristu hasa katoliki eti hazina talaka/hazivunjwi.

Mwisho kabisa chini ya sheria ya ndoa, ni kosa la jinai mtu kudanganya taarifa zake kuhusu hali ya ndoa na lina adhabu imechangamka kidogo.
 
Ndugu, mimi pia mkatoliki. Na hizo ndoa nilizozishuhudia ni za kikatoliki. Sisi wakatoliki hatuna database zaidi ya matangazo ya kanisani, mtu anadanganya sehemu alizoishi.

Kama upo karibu na padri yeyote, jaribu kuuliza hili. Jimboni kuna mahakama ya kanisa. Kesi za namna hii, ni nyingi. Na kila siku ndoa zinabatilishwa. Fanya utafiti.
Lakini,wewe mwenyewe umeshuhudia/kueleza waligundulika na ndoa zikabatilishwa.Unafikiri iliwezekanaje?
 
Ndiyo. Ukienda na cheti cha ndoa kwenye ofisi za RITA wanakufanyia huo uhakiki na mzigo utakua unatambulika. Kwa sasa nasikia hata baadhi ya huduma, kama bima ya afya wanapomsajili mwanachama mpya hawakubali cheti cha ndoa ambacho hakijahakikiwa.
Aisee ngoja tulifanyie kazi
 
Lakini,wewe mwenyewe umeshuhudia/kueleza waligundulika na ndoa zikabatilishwa.Unafikiri iliwezekanaje?
Ndoa nyingi zinajulikana kwenye mitandao kupitia accounts za MCs au wapiga picha. Inawezekana zinazotambulika na kubatilishwa ni chache sana kuliko wanaoendelea kuishi katika vifungo
 
Ndoa nyingi zinajulikana kwenye mitandao kupitia accounts za MCs au wapiga picha. Inawezekana zinazotambulika na kubatilishwa ni chache sana kuliko wanaoendelea kuishi katika vifungo
Tukijikita kwenye neno "inawezekana" tunakuwa hatuna jibu lenye uhakika.
 
Amri ya kuvunja ndoa zote inatolewa na Mahakama tu, hakuna kanisa, sinagogi, hema wala msikiti unaoweza kutoa hiyo amri na ndoa zote zinavunjwa na msajili wa ndoa ambaye ndie mtekelezaji wa hiyo amri ya Mahakama.

Tatizo watu wengi wanafikiri ndoa za kikristu hasa katoliki eti hazina talaka/hazivunjwi.

Mwisho kabisa chini ya sheria ya ndoa, ni kosa la jinai mtu kudanganya taarifa zake kuhusu hali ya ndoa na lina adhabu imechangamka kidogo.
Ni kweli upo sahihi mkuu. Wanachofanya mahakama ya kanisa (ntazungumzia katoliki, maana nimeshafanya utafiti). Wao wataiandikia mahakama kubatilisha ndoa mpya(ya pili) kwasabb ndoa mpya imefungwa kwasabb za udanganyifu.
 
Ni kweli upo sahihi mkuu. Wanachofanya mahakama ya kanisa (ntazungumzia katoliki, maana nimeshafanya utafiti). Wao wataiandikia mahakama kubatilisha ndoa mpya(ya pili) kwasabb ndoa mpya imefungwa kwasabb za udanganyifu.
Sijakuelewa Mkuu.
Mahakama ya kanisa au unazungumzia Bodi ya Usuluhishi wa Migogoro ya Ndoa?.

Umeniacha nje hapo. Sababu iwe itakavyokuwa ni Mahakama tu yenye mamlaka ya kutoa uamuzi juu ya gali ya ndoa na amri juu ya ndoa hiyo.

Hakuna chombo chochote kingine kinachoipangia Mahakama au kuiongoza Mahakama kwenye hayo mamlaka yake.

Hata Fomu Na. 3 ya Bodi ya Usuluhishi Migogoro ya Ndoa, bado haiipangii Mahakama nini chakufanya.

Hii ni area yangu ya practice naielewa vyema.
 
Sijakuelewa Mkuu.
Mahakama ya kanisa au unazungumzia Bodi ya Usuluhishi wa Migogoro ya Ndoa?.

Umeniacha nje hapo. Sababu iwe itakavyokuwa ni Mahakama tu yenye mamlaka ya kutoa uamuzi juu ya gali ya ndoa na amri juu ya ndoa hiyo.

Hakuna chombo chochote kingine kinachoipangia Mahakama au kuiongoza Mahakama kwenye hayo mamlaka yake.

Hata Fomu Na. 3 ya Bodi ya Usuluhishi Migogoro ya Ndoa, bado haiipangii Mahakama nini chakufanya.

Hii ni area yangu ya practice naielewa vyema.
Kwenye kanisa katoliki kuna chombo huru kinachoshughulika na kesi zinazohusu kanisa. Wanaitwa mahakama. Kuna watawa ambao ni wataalam wa sheria za kanisa na hizi zisizo za kanisa, wanafanyakaz humu. (Kanisa katoliki lina mifumo ya kiutawala kama serikali).

Kanisa katoliki linasheria zake. Wao wanauwezo wa kubatilisha ndoa kutokana na sheria zao. Kisha watatoa taarifa ya ubatilishwaji wa ndoa hiyo kwa mamlaka ya kiserikali. Ubatilishwaji wa ndoa kikatoliki kunamuondolea bi harusi/ bwana harusi kifungo cha kutofunga ndoa nyingine. (Ataruhusiwa kuoa/kuolewa tena ndani ya kanisa katoliki).
 
Hilo swala linaisha karibuni maana lazima mtu awe na NIDA ndo unaandikishwa
Ndugu, naweza kupata ufafanuzi litaishaje? Kama mtu ataandika namba ya NIDA labda kanisa A, je kanisa B lililo nje ya mkoa wa kanisa A litapataje taarifa??
 
RITA inatakiwa aidha iunder upya, imegwe ili issue za vizazi na vifo zijitegemee kwa taasisi yake na issue za ndoa na talaka, kivyake, na issue za mirathi na udhamini kivyake. leo hii wakristo wengi tu wana ndoa na mke yupo hai ila wanaenda bomani na kufunga ndoa na mwingine na wanaishi na mitala, wengi sana tunawajua. ilitegemewa, kama mtu ameshafunga ndoa, database ionyeshe, asipate cheti kingine, database ionyeshe huyu alishafunga ndoa na hajaivunja ile ya awali.

kwenye vyeti vya kuzaliwa nako, unaweza kupata hata kumi ukiamua, kila mkoa ukienda unapata na msajili mkuu hajui kama vimejirudia. kwenye vifo kuna watu wanauawa wakati wapo hai, wengi sana.
Naungana na wewe mkuu. Kuhusu cheti cha kuzaliwa:- kuna jamaa yangu alihitaji kujiunga na moja ya vyombo vya ulinzi hapa nchini Ila umri ulishampita. Akaenda wilayani, akapata cheti kipya ambacho amepeleka miaka 10 mbele. Kwasasa kupitia cheti chake, bado hajafika miaka 25
 
Kwenye kanisa katoliki kuna chombo huru kinachoshughulika na kesi zinazohusu kanisa. Wanaitwa mahakama. Kuna watawa ambao ni wataalam wa sheria za kanisa na hizi zisizo za kanisa, wanafanyakaz humu. (Kanisa katoliki lina mifumo ya kiutawala kama serikali).

Kanisa katoliki linasheria zake. Wao wanauwezo wa kubatilisha ndoa kutokana na sheria zao. Kisha watatoa taarifa ya ubatilishwaji wa ndoa hiyo kwa mamlaka ya kiserikali. Ubatilishwaji wa ndoa kikatoliki kunamuondolea bi harusi/ bwana harusi kifungo cha kutofunga ndoa nyingine. (Ataruhusiwa kuoa/kuolewa tena ndani ya kanisa katoliki).
Sahivi ndio nimekuelewa ulichokizungumzia Mkuu, ila ni kwamba Canon haiwezi kuvunja ndoa.

Ni kweli kuwa zinahayo mazingira lakini kwa Tanzania hili haliwezekani hata kidogo.

Sababu ni kuwa sheria ya ndoa.haijatambua chombo kingine chochote tofauti na Bodi ya Usuluhishi na Mahakama.

Hata kanisa litamke kutoitambua ndoa ya waumini wake kamwe haliwezi kuivunja. Ni sawa na BAKWATA nao waliwahi kuvunja.ndoa mfano ile ya Dr. Mwaka lakini baadae Mahakama ikasema hawana huo uwezo same kwa kanisa.

Maombi ya kuvunjwa kwa ndoa ni maombi ya wanandoa wenyewe na wala sio mtu au taasisi nyingine yoyote, sababu ndoa ni mkataba baina ya watu wawili (mume na mke) hivyo mtu wa tatu hayupo kwenye terms zake.

Swali ni je Mkristu mwenye ndoa akiamua kuhama dini je ndoa yake inabatilika?, jibu ni hapana ndoa inabaki kuwepo na hii ni kwasababu hakuna ndoa ya kikristu wala kiislamu hiyo ni mifumo zilivyofungwa. Ndoa ni aina mbili tu, Mke Mmoja na Wake Wengi.

Hizo zingine ni mifumo na mifumo haiwezi kubatilisha ndoa.
 
Habari..

Kumekuwa na udanganyifu kwenye baadhi ya ndoa za kikristo. Kwa sheria na taratibu zao imeruhusiwa ndoa moja tu. (Nyingine zitafungwa ikiwa mwanandoa mmoja amefariki au ndoa kubatilishwa na kanisa)

Nimeshahudia kesi za watu watatu wakristo, mmoja alifunga ndoa na mwanamke ambaye alishafunga ndoa mkoani Kilimanjaro na baadae kuamia Dar Es Salaam. Mwanamke alidanganya kuwa hakuwahi kuolewa. Baada ya kesi kuunguruma- ndoa ilibatilishwa.

Pia kuna ndoa mbili wanaume wamefunga ndoa mikoani (nje ya dar), baadae wakagundulika kuwa walishafunga ndoa.

Ushauri: ingekuwa vyema swala La ndoa lingewekwa kwenye mtandao. Taarifa za ndoa zingekuwa kama kwenye google sheet ili taarifa ziweze kuonekana katika makanisa. Wachungaji na mapadri wapewe access ya hiyo program ili kuondoa duplicate.
Hata ungemuwekea mwanadamu alama 😂 atachiti tu

Hata ukimfungua kengele wewe chezana wanyama wengine siyo bin adam
 
Back
Top Bottom