Ubora wa tv za Star-X

Mkuu naomba experience yako Kama unazielewa vizuri tv aina ya boss, kuna ambayo nimeiona nchi 42" ya mwaka 2017 ina resolution yake ni 2160 yaani mara mbili ya 1080.Picha yake ilinivutia sana inatumia android.
Mkuu mi sijawahi zitumia tv za boss labda nipitie specification zake kwanza.
Natumia TCL sahivi baada ya kutoka samsung.
 
TCL ni wa tatu Duniani miaka mingi sasa, sema wanacompete na samsung na LG kwenye TV zetu hizi za kibongo za bei rahisi ila kwenye TV high end kama za OLED bado hajafika level hizo.

os yao hio Roku, pia unaweza ukaieka tv yoyote unanunua tu stick ya roku na kupachika kwenye tv yako.



mimi napenda kampuni ambazo ni wa wazi, kila kitu wanachotumia wanasema na specs zipo wazi unanunua unachokijua. sio kampuni nyengine za mfukoni tu hakuna maelezo duniani kuhusu hio kampuni.
 
100%!
 
Decoder yao nilinunua MPEG4 kilichotokea siku moja meamka nawasha tv naambulia nembo ya star x tu kwny screen.... Hakuna kinachoendelea mpaka leo.....
 
Mkuu kwa ushauri wako hivi Ipi ni nzuri hapa japo brand zote zinafanya poa incase of quality ya picha na durability japo chochote kinaweza dumu matunzo yakianza kwa mtumiaji.Ahsanteh
1.lG LED Tv 32 inch
2.SAMSUNG LED Tv 32 inch

Na hii ROKU inaweza fanya kazi kwenye LG au SAMSUNG ili kuifanya iwe smart(Android Box) au hii sio kazi yake na vipi ubora wake
 

inategemea na hio tv mkuu. hizo hizo za inch 32 zipo za 720p na za 1080p, zipo ambazo ni smart na zisizo smart, zinatofautiana ports na vyenginevyo.

roku ndio os sio android. imetengenezwa maalum kwa kwa ajili ya tv, haina apps kama android ila vitu basic vya tv inafanya.

kwa mazingira ya ki Africa Android ni nzuri kuliko Roku sababu sisi tunataka bure hatulipii kustream.
 
Mkuu, nakushukuru kwa maelezo yako hapo juu. Natumia star x ya nchi 43, hii niliinunua kama dharula baada ya sumsung LED nchi 48 yangu kuanguka na kupasuka kioo.

Nikaipeleka pale niliponunua Freedom communication wakaniambia repair ni kama 1.5M, nikaamua kununua star x kama dharula kwa 700,000.

Toka nimeinunua kama miaka 3 hvi ila juzi hapa ndio nikaona kama hizi tv sio quality kabisa, hua sina mwenendo wa kuangalia tv hata nikiwa nyumbani, sasa juzi hyo niliishika kuna kitu nilikua narekebisha, ndio nikaona inaweka rangi mara mistari nikajua hakuna kitu kabisa ingawa haijawahi kusumbua, sijawahi kupata malalamiko hapa hom kama inasumbua.

Ngoja nirudi sumsung au lg. Kweli cheap is expensive. Inaweza kuja kuzimika ghafla au ikaungua.
 
Ahsanteh mkuu ila nipe option kulingana na ulichoongea hapo juu kupitia brand hizo mbili bado nahitaji msaada wa hilo na iwe tu ambayo sio smart.
 
so mzee unataka kusema now brand matata ambayo mtu wala unaweza ukajivutavuta nayo kimaisha ni hiyo TLC?
 
Ahsanteh mkuu ila nipe option kulingana na ulichoongea hapo juu kupitia brand hizo mbili bado nahitaji msaada wa hilo na iwe tu ambayo sio smart.
ngumu kupata tv mpya ambayo sio smart, sababu mpaka low end tv zina hizo features.
angalia hizi models.

-LG 32LH550b
-Samsung UN32J6300 1080p
-Samsung UN32J4000 720p

hio samsung yenye 1080p kwa mbele kama utaipata ni nzuri zaidi,
 
so mzee unataka kusema now brand matata ambayo mtu wala unaweza ukajivutavuta nayo kimaisha ni hiyo TLC?
Yeah hio hapo ni unakuwa una utulivu wa nafsi ukiinunua. Tofauti na brand nyingine ambazo sio kongwe sokoni kama mr.uk, boss, star-x n.k!
 
Kuna tatizo moja kubwa sana Tanzania. Kununua kwa Kigezo kimoja tu ambacho umekariri

Unasikia mtu anakwambia star X mimi nnayo miaka 3 haisumbui, tecno yangu tangu ninunue sijaona tatizo

Kwakweli kununua vitu vya electronics hasa TV au Simu haiishii tu kusema kimekaa miaka mingapi.

TV kwa mfano zina mambo mengi ya kuangalia. Ikiwepo Ubora wa picha, Rangi, Kioo, speaker ukiachilia mbali tecnolojia za ziada, kama HDR, Mirroring nk nk

Sasa unakuta mtu anakwambia nna Mr Uk mwaka wa saba, kaangalie Iyo TV picha na Rangi duh unaweza kimbia. TV ukienda pembeni tu 45° unaona usiku

Kwahiyo kununua hv vitu yahtaji ki Review mambo mengi. Binafsi hata mitandaoni nakutaga Samsung inch 55 labda inauzwa mil 1, unavutiwa labda bei cheap. Lakini cha kwanza nitamuomba muuzaji Model ya TV husika. Hapo naweza kukaa sasa google hata masaa 2 nai Review taratibu.

Kuanzia Display, Colour, Finishing materials, Innovation inazokuja nazo Nk nk
 
Kwenye vitu vya eletronics ukifanya kosa kidogo tu litagharimu mda mrefu
 
mkuu vip phillips uimara wake?
Mkuu hiyo Philips ni jina tu,ndani siyo ile Philips ya kutoka Uholanzi ya miaka iliyopita. Jina lilikuwa licenced kwa TPV ya china tangu 2005 for entry level TV sets na kuanzia 2011 wachukua TV sets zote za Philips. Kwa hiyo hizo Philips TV humo ndani siyo Philips. Kama vile TCL wanavyopewa mkataba na Samsung kutengeneza mainly entry level TV sets
Na kuna kampuni nyingi sana ambazo zinafanya outsourcing hasa kwa entry level products kupunguza gharama.
Ukiangalia kwa undani au ukiwa ni mtu kufanya research haswa wakati huu wa utandawazi utagundua vitu vingi sana vinatengenezwa sehemu moja ila vinavikwa nguo tofauti na jina tofauti.Na kwa walio huko home wapambane na fake products kwa wakati huo huo. Nafikiri nimejibu swali,kuna wakuu wengine wanaweza kuongezea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…