Ubora wa mawasiliano nchini umeshuka sana, TCRA fanyeni kazi yenu

Ubora wa mawasiliano nchini umeshuka sana, TCRA fanyeni kazi yenu

olimpio

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2023
Posts
419
Reaction score
867
Nimepitia ripoti ya robo ya pili ya mwaka ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania nimeona TCRA wametujulisha kuhusu kushuka kwa ubora wa mawasiliano ya simu nchini lakini hawajasema wanafanya nini baada ya mawasiliano hayo ubora wake kushuka.

Ripoti imekaa vizuri sana na hawajataka kuficha kitu chochote ,sasa swali linakuja makampuni ya simu kwa nini yanaendelea kunyamazia ubora wa mawasiliano yao kushuka? sio Vodacom , Tigo sijui YAS,Airtel na TTCL.

Ninawashauri TCRA wawapige faini kali mitandao ya simu ili ubora wa mawasiliano urejee kuwa sawa, siku hizi ukipiga simu ukiongea kwa dakika sita ,lazima ukate upige tena kwa nini?
Hii mitandao ya simu isichekewe ,haiwezekani niongee kwa dakika sita then dakika moja simsikii ninayeongea naye ,kuna silent calls nyingi sana.

Ukiangalia Ripoti ya TCRA inaonyesha kila mtoa huduma amepata asilimia zaidi ya 95% ya ubora, kuna haja ya kutofautisha ubora wa kila category ,hapa imejumuishwa sana ,watu wanalalamikia simu za kupiga hazina ubora ,lakini hapa imechanganywa simu na intaneti, nashauri wabadirishe wakitenganisha intanet na simu za kupiga wataona maajabu.

1770535430327.png
 
Hivi TTCL bado wapo?
Nauliza tu kwa kuwa mkongo wa TAIFA kuwafikishia watu majumbani hata sijui uliishia wapi?
Nafikiri wangechukua mkopo hata wa Bilioni 500 wasambazie watu iNTERNET majumbani hiyo hela ingeweza kurudi ndani ya mwaka mmoja.
Ni kama wana colateral ila hawaichukulii mkopo; hata sielewi kwa kweli...
 
Hivi TTCL bado wapo?
Nauliza tu kwa kuwa mkongo wa TAIFA kuwafikishia watu majumbani hata sijui uliishia wapi?
Nafikiri wangechukua mkopo hata wa Bilioni 500 wasambazie watu iNTERNET majumbani hiyo hela ingeweza kurudi ndani ya mwaka mmoja.
Ni kama wana colateral ila hawaichukulii mkopo; hata sielewi kwa kweli...
Fiber
Na simu pia wapo na inatumika km kawaida ila watu sio wengi
Hio ni km TBC na TRC ila kuna muda inakufa kuna muda inafufuka inategemea ni kipaumbele cha nani
 
Back
Top Bottom