Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,326
- 859,863
Jamaa mmoja alichomwa mshale na mtu aliyefanikiwa kukimbia bila kuonekana, akiwa kwenye maumivu makali akabahatika kupata msaada na kupelekwa hospitali
Cha kushangaza sana akakataa matibabu yoyote mpaka
-Aliyemchoma ajitokeze
-Kisha aeleze sababu za kumchoma
-hilo tukio alilipanga lini
-akiwa na nani
-alimchoma akiwa umbali gani
-huo mshale aliupata wapi nknk
Huo haukuwa muda sahihi wa kuhoji hayo yote kipaumbele kilikuwa ni kupata matibabu ili kuokoa maisha na hasa ikizingatiwa anatoka damu nyingi na huyo aliyemchoma wala hajapatikana. Alikufa bila kupata majibu ya maswali yake
Vipaumbele ni jambo moja la muhimu sana katika maisha.. ni lazima katika maisha ujue ni kipi cha lazima na ni kipi cha muhimu! Na je ufanye ya lazima kwanza au ya muhimu?
Huyo ndugu aliyechomwa mshale ilikuwa ni muhimu kumfahamu aliyemchoma huo mshale na kwanini alimchoma nk lakini lakini haikuwa lazima kwa wakati ule. Ni matokeo yake haya alipoteza maisha
Tumefeli mengi tu katika maisha yetu kama mtu mmoja mmoja vikundi na hata kama taifa kwa ujumla wake. Tumeshindwa kufanya mengi, Tumeshindwa kabisa kufanikisha mengi kwakuwa tumeshindwa kujua sisi ni nani na tumetoka wapi na tuna vipaumbele gani na je ni vya muhimu au ni vya lazima?
Hata ndani ya JamiiForums mijadala mingi sana yenye tija kwa taifa na hata kwa mtu mmoja mmoja imeshindwa kukamilika au kupoteza maana yake kwa ubishi tu wa kipuuzi kabisa
Mijadala mingi imeondoshwa kwenye mstari na kuanza kujadili mtu na hulka zake binafsi! Kujadili na kubishana kosa dogo tu la kiuandishi ambapo vyote hivi vinakuwa haviko kwenye msingi wa mada
Unapoingia kwenye mjadala fulani usikubali kamwe kuburuzwa na kutolewa nje ya mada! Baki kwenye msingi wa mada huku ukibishana kwa hoja..wapo wengi ambao wana tabia za bondia Tyson akishindwa anang'ata masikio...! Mijadala hupanua ufahamu na kushughulisha akili
Jua kipaumbele chako ninini kwenye chochote katika maisha yako fanya yake ya lazima kwanza kisha yafuate ya muhimu utaona matunda yake
Barikiwa sana......!!!!
Cha kushangaza sana akakataa matibabu yoyote mpaka
-Aliyemchoma ajitokeze
-Kisha aeleze sababu za kumchoma
-hilo tukio alilipanga lini
-akiwa na nani
-alimchoma akiwa umbali gani
-huo mshale aliupata wapi nknk
Huo haukuwa muda sahihi wa kuhoji hayo yote kipaumbele kilikuwa ni kupata matibabu ili kuokoa maisha na hasa ikizingatiwa anatoka damu nyingi na huyo aliyemchoma wala hajapatikana. Alikufa bila kupata majibu ya maswali yake
Vipaumbele ni jambo moja la muhimu sana katika maisha.. ni lazima katika maisha ujue ni kipi cha lazima na ni kipi cha muhimu! Na je ufanye ya lazima kwanza au ya muhimu?
Huyo ndugu aliyechomwa mshale ilikuwa ni muhimu kumfahamu aliyemchoma huo mshale na kwanini alimchoma nk lakini lakini haikuwa lazima kwa wakati ule. Ni matokeo yake haya alipoteza maisha
Tumefeli mengi tu katika maisha yetu kama mtu mmoja mmoja vikundi na hata kama taifa kwa ujumla wake. Tumeshindwa kufanya mengi, Tumeshindwa kabisa kufanikisha mengi kwakuwa tumeshindwa kujua sisi ni nani na tumetoka wapi na tuna vipaumbele gani na je ni vya muhimu au ni vya lazima?
Hata ndani ya JamiiForums mijadala mingi sana yenye tija kwa taifa na hata kwa mtu mmoja mmoja imeshindwa kukamilika au kupoteza maana yake kwa ubishi tu wa kipuuzi kabisa
Mijadala mingi imeondoshwa kwenye mstari na kuanza kujadili mtu na hulka zake binafsi! Kujadili na kubishana kosa dogo tu la kiuandishi ambapo vyote hivi vinakuwa haviko kwenye msingi wa mada
Unapoingia kwenye mjadala fulani usikubali kamwe kuburuzwa na kutolewa nje ya mada! Baki kwenye msingi wa mada huku ukibishana kwa hoja..wapo wengi ambao wana tabia za bondia Tyson akishindwa anang'ata masikio...! Mijadala hupanua ufahamu na kushughulisha akili
Jua kipaumbele chako ninini kwenye chochote katika maisha yako fanya yake ya lazima kwanza kisha yafuate ya muhimu utaona matunda yake
Barikiwa sana......!!!!