Ubinafsi tunaofanya kwa watoto wetu unasikitisha

ANKO JEI

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,278
2,364
Kwa jinsi nilivyo na haraka nikusalimu kifupi tu, Uhali gani?

Baada ya kukaa kuwaza nimekuja kujua wengi wetu ni wabinafsi sana, na wengine hata hatujui kuwa tunachofanya ni ubinafsi wa kutisha.

Wewe unajiona kabisa una familia au niseme mtoto ili uelewe vizuri, ila still una mawazo mgando ya kushikilia hako kaajira kako, miaka inaenda huwazii hawa watoto wako itakuaje, na unajua kuwa wewe mwenyewe ulipata hiyo kazi kwa bahati nasibu tu kama sio kuhonga na kuna asilimia kubwa ni kazi ambayo huwezi kumrithisha mwanao.

Badala uwaze kufanya jambo ambalo litawaandalia watoto wako future nzuri, we umetulia tu unawaza kutembea na wake za watu hapo ofisini. Tengeneza connection ambazo watoto wako hawatakuja pata tabu bro! asikudanganye mtu connection zitakuja isha, yani kwajinsi dunia ilivyochafuka nadhani hapo baadae bila connection huwezi pata kazi.

Usikute una mtoto wakike lakini hata huwazi kuanza kumuandalia mazingira yake akisoma asije pata tabu kupata kazi au kujiajiri, we kazi yako kumpeleka mlimani city akachorwe kama spiderman na kula ice cream, sisemi ni vibaya lakini usijipige kifua kuona ndo umemaliza jukumu lako, huyo mtoto atakua mkubwa atakua na chura atavutia wanaume humo maofisini, bro atatafunwa sana ili kupata kazi.

Ishi na watu vizuri kununua gari haimaanishi majirani zako hawana juhudi za maisha, ukiishi nawatu vizuri hao watoto wako au familia yako itafurahi baadae,watasaidiwa na watu wasio wajua kwasababu uliishi nao vizuri.Kuna watu leo wanaogopa hata kutumia bini zao kutokana na upuuzi wa wazazi wao miaka ya nyuma, na kuna watu akitaja ubini tu ataulizwa baba ako ni yupi.

Usijiwazie wewe tu ndugu yangu, kuna kizazi kinasubiri kuja kufurahia maajabu uliyofanya ukiwa hai.

Ni hayo tu.

Anko Jei
 
Kwa jinsi nilivyo na haraka nikusalimu kifupi tu, Uhali gani?

Baada ya kukaa kuwaza nimekuja kujua wengi wetu ni wabinafsi sana, na wengine hata hatujui kuwa tunachofanya ni ubinafsi wa kutisha.
Bro hebu tuanze na wanao, umewafanyia hivi ulivyoshauri?
 
Kwa jinsi nilivyo na haraka nikusalimu kifupi tu, Uhali gani?

Baada ya kukaa kuwaza nimekuja kujua wengi wetu ni wabinafsi sana, na wengine hata hatujui kuwa tunachofanya ni ubinafsi wa kutisha.
Ukute hapo una kabiadhara ka 10M unatukana watu, biadhara ni kipaji sio kila mtu anaweza hata awe na mtaji. Hizo connections unazozisema unazifanya wakati umri wa watoto wako ni miaka mingapi? Hao unaoconekti nao wakipoteza hicho unachokiwinda? Ajira, biashara, nafasi nk.

Chamsingi somesha watoto shule nzuri na uwape maarifa mengine ya kujiajiri ikitokea hawakuajiriwa.
 
Maisha hayana kanuni mie ninafanya biashara kubwa tu ila ajira siiachi. Mshahara mkubwa mtamu ndugu yangu.

Ndio maana watu wanaenda kwa waganga wasitoke kwenye ajira
 
Maisha hayana kanuni mie ninafanya biashara kubwa tu ila ajira siiachi. Mshahara mkubwa mtamu ndugu yangu.

Ndio maana watu wanaenda kwa waganga wasitoke kwenye ajira
Kuna wenzio amekaa na ajira tu hana ishu nyingine.

Hiyo biashara yako ni unaweza kuwafundisha watoto na wakaja kufurahia maisha vema tu mkuu.
 
Sina mtoto bado, but nishaanza kuandaa mazingira, mishe zangu nyingi hata nikifa watakuja kufaidi vizuri sana.
ingekuwa poa kama ungekuwa na mtoto tuone mfano halisia..maana siku zote matarajio na uhalisia ni vitu viwili tofauti
 
ingekuwa poa kama ungekuwa na mtoto tuone mfano halisia..maana siku zote matarajio na uhalisia ni vitu viwili tofauti
Uhalisia ni kwamba nimeshaanza kuandaa vitu kwaajili yao..mtoto ni majaliwa ila akija atakuta mazingira fulani.
 
Unakuta jitu tajiri alafu lina mental health- ugonjwa wa akili ( chizi )
 
Back
Top Bottom