Ubinafsi ndio unaowafanya watu wanaoana

Ubinafsi ndio unaowafanya watu wanaoana

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Kila mmoja wetu ameshawahi kusiki kuwa mtu fulani anamuoa/olea na mwingine kwa madai kuwa wanapendana au anampenda huyo anaeingia nae kwenye ndoa,madai haya yapo na huenda hata wewe unafikiri hivyo hivyo.

Leo nataka nikupe ushahidi kuwa sio kweli kuwa watu wanaoana kwasababu ya kupendana au kupenda bali ni kwasababu ya ubinafsi tu ni vigumu sana kusema kuna watu ambao wanaoana kwasababu wanapendana au mmoja kumpenda mwenzake,hili linatokana na mfumo wa kimaisha tulio nao leo pamoja na wengi kutokujua hata upendo ni kitu gani.

Kupenda kuna maana ya kumkubali mwenzako bila masharti ikiwa ni pamoja na kujitoa kwaajili ya furaha yake na sio furaha yako, sasa tukija kwenye suala la ndoa na mahusiano kwa ujumla wake mara nyingi watu wanaingia kwenye uhusiano na wale ambao wanajisikia raha kuwa nao karibu au kwa kifupi wanahisia chanya nao.

Watu hawa wamejikuta wakisema kwamba wanawapenda wahusika hivyo kufanya jitihada za kuingia ndoani na wahusika na wamekuwa wakitamani hata kufa pale ambapo wanashindwa kuingia kwenye ndoa na wahusika,lakini je kwa tafsiri hiyo hapo juu ni kweli kwamba watu hawa wanaongozwa na upendo kutamani kuingia kwenye ndoa au kuna kitu kingine?

Ukweli mchungu ni kwamba hawaongozwi na upendo bali ubinafsi,nasema hivi kwasababu kinachomuongoza mtu kuingia ndoani ni zile hisia zake yeye kwa mhusika na sio hisia za mhusika kwake yeye, yaani iko hivi, wewe unapokutana na mtu halafu ukajisikia amani na furaha kuwa karibu yake utasema unampenda na utataka uendelee kuwa nae.

Karibu maisha yako yote ili uendelee kujisikia vizuri na sio mwenzako kujisikia vizuri, hapoa wala hutajali mwenzako anajisikiaje kwasababu tu wewe unajisikia vizuri unapokuwa nae utataka akuoe au umuoe,huu ni ubinafsi,yaani unajifikiria wewe tu na unaingia humo kwenye ndoa kwasababu wewe unajisikia vizuri na sio mwenzako

Hata wale ambao wanasema wanapendana,yaani wanakutana watu wawili ambao wote wanajisikia vizuri pale ambapo wanakuwa pamoja,hawa nao wanapoingia kwenye ndoa sio kwasababu wanapendana bali ni kwasababu kila mmoja anajisikia vizuri anapokuwa na mwenzake,hii ina maana kwamba kila mmoja anaongozwa na yeye kujisikia vizuri kwa mwenzake na sio kuongozwa na hisia za mwenzake kwake

Kama kweli tungekuwa tunaomngozwa na upendo basi tungeolewa au kuoa wale ambao wao tu wanajisikia vizuri kuwa na sisi,hii inamaana kwamba tunajitoa kwaajili ya furaha za wengine kama maana ya kupenda ilivyo,yaani uende kuoa au kumuoa yule ambae wewe huna hisia chanya nae lakini yeye anazo hisia chanya kwako hapo utakuwa umempenda na kuongozwa na upendo kuingia kwenye ndoa.

Ukweli huu mchungu ni mgumu kukubaliwa na wengi, kwasababu tumeaminishwa kuwa upendo ni wa aina fulani wakati sio kweli. Je wewe ni mmoja wa wale wanaoongozwa na ubinafsi au hapana?
 
real
basi sioi/siolewi mpaka nipate anaejisikia furaha zaidi yangu mimi kua karibu naye

is that so?
 
Kama nikienda kuoa mtu ambaye sina hisia chanya naye ila yeye ana hisia chanya namie kwa mjibu wa maelezo yako kwamba ndo ntakuwa nmempenda, basi yeye atakuwa mbinafsi coz kaamua kuolewa na mtu ambae hana hisia chanya nae. UNAFIKIRI KUTAKUWA NA MAPENZI YA KWELI TENA HAPO?
 
mkuu ulichosema ni sahii, hasa wanawake maraningi upendo wao usukumwa na mfumo wa maisha.angalia hao dada walio kwenda shule na kupata kazi nzuri kama kwao ni rahisi kupata mchumba.
 
hii kitu sikubaliani nayo kabisa. Kuna watu hasa wanaume ambao anaweza akamuoa msichana fulani kwa ajili yakumfanya huyo girl awe happy and peaceful, kuna mwingine anakuwa na hamu tu kumsaidia fulani katika hali aliyonayo labda ya msongo then katika harakati hizo na mapenzi yanajichanganya mwisho wanaoana.
 
hii kitu sikubaliani nayo kabisa. Kuna watu hasa wanaume ambao anaweza akamuoa msichana fulani kwa ajili yakumfanya huyo girl awe happy and peaceful, kuna mwingine anakuwa na hamu tu kumsaidia fulani katika hali aliyonayo labda ya msongo then katika harakati hizo na mapenzi yanajichanganya mwisho wanaoana.

Umesema kitu aisee.
 
Kama nikienda kuoa mtu ambaye sina hisia chanya naye ila yeye ana hisia chanya namie kwa mjibu wa maelezo yako kwamba ndo ntakuwa nmempenda, basi yeye atakuwa mbinafsi coz kaamua kuolewa na mtu ambae hana hisia chanya nae. UNAFIKIRI KUTAKUWA NA MAPENZI YA KWELI TENA HAPO?

Upo sahihi mkuu,
 
real
basi sioi/siolewi mpaka nipate anaejisikia furaha zaidi yangu mimi kua karibu naye

is that so?
Ukiweka sharti bado utakuwa umefanya hivyo kwasababu yako binafsi which means unakuwa mbinafsi ...!!
 
hii kitu sikubaliani nayo kabisa. Kuna watu hasa wanaume ambao anaweza akamuoa msichana fulani kwa ajili yakumfanya huyo girl awe happy and peaceful, kuna mwingine anakuwa na hamu tu kumsaidia fulani katika hali aliyonayo labda ya msongo then katika harakati hizo na mapenzi yanajichanganya mwisho wanaoana.
Sasa ambacho hukubaliani nacho ni kipi?
 
Kama nikienda kuoa mtu ambaye sina hisia chanya naye ila yeye ana hisia chanya namie kwa mjibu wa maelezo yako kwamba ndo ntakuwa nmempenda, basi yeye atakuwa mbinafsi coz kaamua kuolewa na mtu ambae hana hisia chanya nae. UNAFIKIRI KUTAKUWA NA MAPENZI YA KWELI TENA HAPO?
Hapa naongea na wewe .....

Kama utafanya hivyo utakuwa umeongozwa na upendo .....

Yaani umejitoa kwaajili ya furaha ya mwingine,huo ndio upendo!
 
watu hawaingii kwenye ndoa kwa sababu ya kipendana, bali ni tamaa za ngono, maumbile na mali.

kama ni upendo, huja badae sana ambapo bila hata kuwa na hivyo mlivyovutiwa navyo , mtu huendelea kumthamin mwenzi wake kama ikivyojuwa mwanzo
 
Ndoa ni muunganiko wenye kuleta furaha katika kipindi cha maisha yao yote kwa wale ambao wameunganishwa na upendo wa dhati kutoka ndani ya nyoyo zao...upendo ambao unawafanya watu wawe mwili mmoja katika kila hali..hapa namaanisha kwenye shida na raha....siku zote ni raha kuwa na umpendae na ni jambo lenye kuzijaza nyoyo zetu furaha na raha wakati wote...machungu ya ndoa yanaanzia pale unafiki unaoingia ndani yake...ninasema unafiki kwa kuwa si kila mwanandoa huwa anaingia ndoani kwa sababu ya upendo bali wengine hufuata mali na vitu vingine vya kupendeza machoni lakini sio rohoni.....matokeo yake ndio huzaa majuto ndani ya ndoa na kuzaa falsafa kuwa ndoa ni gereza la mateso ilihali maana halisi ya ndoa haiko hivyo.....tunapochagua wenzi wa maisha tujitahidi kuzipa nafasi nyoyo zetu ziamue...kwani upendo wa kweli hutoka mioyoni mwetu na sio mifukoni mwa mwetu au mwa mtu....na kipimo cha upendo usiwe mali bali matendo ya yule anayedai anakupenda kwani MUNGU hajawahi kumficha mnafiki....
 
Back
Top Bottom