Ubaguzi unaendelea kuitafuna CHADEMA

Ubaguzi unaendelea kuitafuna CHADEMA

Kati ya vitu ambavyo sitakaa nimridhishe au kumsimulia mtu, na hasa mtoto wangu ni kuhusu CCM.

Sina ushabiki wa vyama, ila kwa hiki chama sipendi hata kusikia. Kama ni kichaka, ni kile kisicho pitika hata na sisimizi.
Ndugu.
Hoja yako inaonyesha kama hujitambui au hutambui kile unachokisema.

Ulichofanya hapa katika andiko lako kinaonyesha siyo kupenda tu kuisikia CCM bali pia kutaka wanaJF wachangie mada zinazohusu CCM.

Mleta mada hajataja CCM katika mada yake lakini wewe unaanza kuongelea masuala ya CCM kuonyesha ni jinsi unavyofatilia masuala ya CCM.
 
Ndugu.
Hoja yako inaonyesha kama hujitambui au hutambui kile unachokisema.

Ulichofanya hapa katika andiko lako kinaonyesha siyo kupenda tu kuisikia CCM bali pia kutaka wanaJF wachangie mada zinazohusu CCM.

Mleta mada hajataja CCM katika mada yake lakini wewe unaanza kuongelea masuala ya CCM kuonyesha ni jinsi unavyofatilia masuala ya CCM.
Kwakifupi nikwamba watanzania wamechoka ccm wanataka chama mbadala nawameshakipata chama chao Mungu alichowaletea Chadema

Mwanahabari Huru
 
Tatizo la kuruhusu watu wengine wafikirie kwa niaba yako.

Siitaji mtu kufikiri kwa niaba yangu kwa ufahamu nilikuwa nao. Huitaji elimu ya pekee kujua mfumo unaoelekea kufa wa ccm.

Hatuwezi kuishi katika ndoto kwa miaka 50 ya uhuru bila kuwa na malengo na mwelekeo chanya. Walio kwenye mfumo huu bado wanaishi katika maoni na wapo kwenye bango la fikra kimaoni.

Mwana falsafa Plato anasema aliye kwenye ulimwengu wa kimaoni bado haufahamu uhalisia wa vitu. Hapa ndipo tunapopata maana ya ujinga, yaani asiyefahamu jambo.

Mtaji mkubwa wa ccm ni wingi wa wajinga. Tunashukuru kwamba kila kukicha idadi ya wajinga inapungua. Hiki ndicho kiyama cha ccm.

Kutoka kwenye mkwamo huu wa fikra tunaitaji "a philosopher king," anayefahamu uhalisia wa vitu. Hili nalo kwa sasa lipo njiani.

Kamwe utawala dhalimu haudumu. Huu ni wakati wa kusoma alama za nyakati. Ni sawa na kifo cha nyani kwamba miti yote huteleza.
 
MwanaDiwani labda huo ubaguzi umesaidia mno kwa CHADEMA kuwapiga CCM easily leo uchaguzi wa marudio Mbezi au?
 
Last edited by a moderator:
Chadema tafuteni mchagga akamrithi ubunge Zitto kigoma

Hawa jamaa hilo wanaliweza pia...hawatabiriki kabisa. Waliwahi kumsimamisha MMASAI agombee Ubunge CHALINZE kwa wakwere na wazaramo, ni kama vile wamechanganyika lakini ndivyo wanavyoendesha chama chao.

Wao kwao sifa ya kuwa kiongozi ni kutoka kasikazini na kuwa mkristo...mimi sio mtu wa kaskazini labda nipitie kwenye ukristo nitapata Kick.
 
Mwl. Nyerere alishawahi kusema, "dhambi ya ubaguzi haifi, inaendelea. Dhambi ya ubaguzi ukishakuitenda inaendelea, ni sawa na kula nyama ya mtu, ukila nyama ya mtu utaendelea tu.".

Kila siku dhambi ya ubaguzi inazidi kumea na kuimarika ndani ya CHADEMA kiasi kwamba kwa sasa wamefikia hata kuanza kutesa baadhi ya watu ili kuendeleza dhambi ya ubaguzi.

Viongozi wa CHADEMA kila siku wanapanda kwenye majukwaa na kujigamba wakisema baadhi ya waajiriwa wa Usalama wa Taifa wanawapa siri za serikali na CCM lakini wanasahau kuwa, maneno yao yanachagiza Karma Law inayosema, What goes around comes around or as you sow, so shall you reap.

Viongozi wa CHADEMA walishawahi kunukuliwa kwenye mikutano katika thread hii;


CHADEMA wanafurahi sana kudai wanapewa siri za Serikali au CCM na baadhi ya waajiriwa wa Usalama wa Taifa lakini wanakuwa wa kwanza kutoa malalamiko na kudai wanahujumiwa pale siri zao zinapochukuliwa na watu hao hao wanaodai wanawapa siri za serikali au CCM. Waingereza wanasema, Don't hate the player, hate the game!

Unapopewa lazima pia ufahamu kuwa utatoa kwa njia hiyo hiyo iliyotumika katika kupewa. This is natural justice!

Baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA ni ruksa kuwasiliana na baadhi ya wana usalama wa taifa (TISS) lakini mwanaCHADEMA mwingine akifanya hivyo hukumu yake ni kuteswa ndani ya ofisi za Red Brigade.

Baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA ni ruksa kuwa na rafiki au ndugu ambaye anafanya kazi katika idara ya Usalama wa taifa, lakini mwanachama mwingine akionekana hata anapanda gari ya mfanyakazi wa usalama wa Taifa adhabu yake ni kuteswa na kufukuzwa uanachama.

Baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA ni ruksa kuwa na namba za simu za viongozi wa CCM au serikali lakini mwanachama mwingine akiwa pia na namba hizo hizo anaitwa msaliti.

Baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA huwa wanafanya mawasiliano na Mwenyekiti wa CCM Taifa, lakini hao hao viongozi wakigundua mwanachama mwingine anafanya pia mawasiliano kama hayo, watamuita msaliti ambaye adhabu yake ni kufukuzwa ndani ya chama.

Hii haitokei kwa bahati mbaya bali kinachofanyika ni
endelezo la dhambi ya ubaguzi ambayo inaendelea kuitafuna CHADEMA.

Chacha Wangwe aliishabikia hali hii lakini mwisho wake ilimtafuna.

Zitto Kabwe, Prof. Kitila na Mwigamba waliishabikia hali hii mwisho wake imewatafuna.

Khalid Kagenzi pia aliishabikia kwa kuanzisha Red Brigade, mwisho wake imemtafuna karibia apoteze maisha yake wakati anateswa ndani ya ofisi za Red Brigade kama siyo wasamalia wema kupiga kelele kuomba msaada.

CUF na NCCR-Mageuzi walishabikia ubaguzi wa CHADEMA kwa mwamvuli wa UKAWA, kwa sasa umeanza kuwatafuna kwa kuanza kubaguliwa!. Neno UKAWA kwa sasa ni bidhaa isiyouzwa au kuuzika ndani ya midomo ya wanaCHADEMA baada ya kupata kile walichokuwa wanakitaka kwenye chaguzi za serikali za mitaa.


Ifahamike tu, leo ni kwa mwingine ndani ya CHADEMA lakini kesho ni kwako unayeendeleza ubaguzi huo ndani ya CHADEMA.

Ni kweli angalia matokeo ya marudio uchaguzi wa aerikali za mitaa ya pale mbezi yanonyesha ni jinsi gani ubaguzi unavyo itesa cdm.pooole sana mkuu
 
WAKATI MNAINANGA CHADEMA. SOMA HII..............M
CHADEMA SASA HII NI KUTAFUTA SIFA BHANA. LZM IONYESHE UTU KWA CCM JAPO KIDOGO......

Chama cha Drmokrasia na Maendeleo- CHADEMA kimeisambaratisha vibaya Chama cha Mapinduzi -CCM katika uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa uliofanyika leo katika mtaa wa Kingazi Kwembe Mbezi DSM

Katika matokeo yaliyotangazwa muda huu hapa kituoni Chadema kimepata ushindi wa kimbunga wa kura 500 huku CCM wakiambulia kura 180

Ushindi huu ni aibu kubwa kwa CCM iliyopiga kampeni kufa na kupona kwa kutumia wabunge na baadhi ya mawaziri.

Ni shangwe kuu zimetanda kila mahali huku mamia ya wananchi wakipeperusha bendera za Chadema.
 
Ni kweli angalia matokeo ya marudio uchaguzi wa aerikali za mitaa ya pale mbezi yanonyesha ni jinsi gani ubaguzi unavyo itesa cdm.pooole sana mkuu

we waache wabwabwaje sisi tunazidisha imani kwa chadema.
 
MwanaDiwani labda huo ubaguzi umesaidia mno kwa CHADEMA kuwapiga CCM easily leo uchaguzi wa marudio Mbezi au?
Ndugu,
Hata shetani mpaka sasa yupo hapa duniani na anaendelea kugeuza binadamu pamoja na kwamba Mungu ana uwezo wa kumuondoa katika harakati zake.

Think deeply!
 
MwanaDiwani labda huo ubaguzi umesaidia mno kwa CHADEMA kuwapiga CCM easily leo uchaguzi wa marudio Mbezi au?

Ukizungumzia Mbezi unazungumzia wachaga na vigango vyao.Ndio sawa leo uzungumzie CUF ishinde Kibosho
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli angalia matokeo ya marudio uchaguzi wa aerikali za mitaa ya pale mbezi yanonyesha ni jinsi gani ubaguzi unavyo itesa cdm.pooole sana mkuu
Hata shetani anawatesa sana kila siku wana wa Mungu lakini hii haina maana kuwa Mungu hayupo.

Tafakari!
 
Ukizungumzia Mbezi unazungumzia wachaga na vigango vyao.Ndio sawa leo uzungumzie CUF ishinde Kibosho

Vipi kule sumbawanga nakwenyewe kuna wachaga wengi kama mbezi?vipi liwale nakwenyewe kuna wachaga wengi?vipi mtwara kuna wachaga wengi?vipi tandahimba kuna wachaga wengi?vipi nachingwea kuna wachaga wengi?punguza ndoto zako hizo na ukubali dawa ikuingie vema
 
We mjinga kwani watu wa sumbawaga na mbezi ni wachaga,hizo propaganda za ccm tumeshazizooeaa,walizusha adi udini ,
 
Huu unafiki wa CHEDEMA wakusema eti wanafanya maamuzi magumu wakuwatimua wanachama wenye msimamo kinzani ni woga tu...kumbe wanajificha kwenye kivuli cha woga, woga wa kunyang'anywa madaraka, woga wa viongozi wa kupingwa ama kushindwa kwa hoja
 
Ukizungumzia Mbezi unazungumzia wachaga na vigango vyao.Ndio sawa leo uzungumzie CUF ishinde Kibosho

With due respect
Kyela hamna wachaga na CHADEMA ikashinda kuongoza mamlaka ya mji mdogo kutoka vitongoji 2 mwaka 2009 hadi 28 mwaka huu

Nadhani kuna mwamko fulani umewaingia watz au una wazo gani?
 
Back
Top Bottom