Uamuzi wa kujengwa ukuta kuzunguka Mererani kulinda madini ya Tanzanite ulifikiwa mwaka 2002, lakini ukawekwa kapuni

Ukuta sawa lakini unajengwa juu ya ardhi haujengwi nchini ya ardhi.Huko ardhini inaweza kujengwa tunnel ya kutokea nje ya ukuta huo na madini kutoroshwa.Natoa angalizo kwa serikali kama mtaalam wa Sekta ya madini.Hapo Mererani huko chini migodi inaingiliana wanaita "mitobozano",huo ukuta wa juu unaweza usisaidie sana madini yanaweza kupita chini kwa chini na kuvuka huo ukuta kwenda vitalu vingine ambavyo siyo A,B,C wala D.Kwangu mm ningekuwa Serikali ningejenga ukuta eneo lote la Mererani na kufanya patrol mita 100-200 kuzunguka huo ukuta kuhakikisha kwamba hakuna shimo lolote linatokeza nje ya Ukuta huo.Aidha,madini ya Tanzanite ningeyafanya nyara ya Serikali.Ukikutwa nayo isivyo halali,wafa.
 
Haya ni mawazo mazuri sana ya kuimalisha usalama wa ndani. Mimi layman ningependa tu kujua HUU WIZI ULIOKUWA UNAENDELEA ULIKUWA UNAFANYIKAJE? Kwani kwa kufahamu vyema mbinu zinazotumika ndivyo unavyoweza kuwa na mbinu bora za kuzuia.

Kwani bado mzigo unaweza kupita getini kwa declaration tofauti, ukapita kama kitu kingine au ukapita mzigo mkubwa kana kwamba ni mzigo wenye thamani ndogo.

Kwanza kabisa ngoja nieleze kidogo utamaduni wa uchimbaji madini kwa mtu mmoja mmoja unavyofanyika Tanzania, wachimbaji wengi wanakuwa wamedhaminiwa, tajiri anaweza kuwa yuko Arusha,mzawa au mgeni ( foreigner), akishamzamini mchimbaji pesa ya kununua vifaa vya uchimbaji na chakula kwa makubaliano ya ukipata mali lazima uniuzie mimi, mchimbaji akienda kuchimba na akapata kiasi lets say gram 1,wataangalia leo bei inasemaje, pengine ni 50 usd, tajiri atatoa pesa yake kwanza aliyomdhamini mchimbaji kama ni usd 20, then kinachobaki 30 anampatia mchimbaji na yeye anachukua mali. Lakini mchimbaji huyu akipata mali hupeleka mzigo kwa tajiri aliyemdhamini, wewe hata ukiwa na kampuni yako ya ununuzi uko eneo la tukio mchimbaji hawezi kukuuzia, kama yuko hotelini huyo tajiri mali itamkuta huko, hivyo tajiri anaweza asiwe hata ni vibali vya ununuzi au license yeyote kutoka serikalini na akaweza kupata mali kila siku kutoka kwa wachimbaji, baada ya miezi kadhaa tajiri mzigo wake umekuwa mwingi huyo anasafirisha, hivyo serikali inakosa mapato . Lakini kwa njia hii ya uzio na biashara ifanyike ndani ya eneo hilo, maana itawalazimu wafanyabiashara wote wawe na vibali husika kutoka serikali kuwa mule ndani, wachimbaji wawe mule ndani, mchimbaji akipata mali hata kama amedhaminiwa atamuuzia tajiri wake na tajiri wake atalipa ushuru maana watu wa TRA watakuwa ndani pia. Hivyo mchimbaji hataweza kutoka na mali nje, na wanunuzi watatoka na mali yao ambayo wamenunua na wameshalipia ushuru.
 
Vp awa jamaa zetu masai na wajaluo wanaouza madini madogomadogo wataendelea kuwepo mjini au ndo safari ya kurudi kijijini itaanza
 
Kwanza kabisa ngoja nieleze kidogo utamaduni wa uchimbaji madini kwa mtu mmoja mmoja unavyofanyika Tanzania, wachimbaji wengi wanakuwa wamedhaminiwa, tajiri anaweza kuwa yuko Arusha,mzawa au mgeni ( foreigner), akishamzamini mchimbaji pesa ya kununua vifaa vya uchimbaji na chakula kwa makubaliano ya ukipata mali lazima uniuzie mimi, mchimbaji akienda kuchimba na akapata kiasi lets say gram 1,wataangalia leo bei inasemaje, pengine ni 50 usd, tajiri atatoa pesa yake kwanza aliyomdhamini mchimbaji kama ni usd 20, then kinachobaki 30 anampatia mchimbaji na yeye anachukua mali. Lakini mchimbaji huyu akipata mali hupeleka mzigo kwa tajiri aliyemdhamini, wewe hata ukiwa na kampuni yako ya ununuzi uko eneo la tukio mchimbaji hawezi kukuuzia, kama yuko hotelini huyo tajiri mali itamkuta huko, hivyo tajiri anaweza asiwe hata ni vibali vya ununuzi au license yeyote kutoka serikalini na akaweza kupata mali kila siku kutoka kwa wachimbaji, baada ya miezi kadhaa tajiri mzigo wake umekuwa mwingi huyo anasafirisha, hivyo serikali inakosa mapato . Lakini kwa njia hii ya uzio na biashara ifanyike ndani ya eneo hilo, maana itawalazimu wafanyabiashara wote wawe na vibali husika kutoka serikali kuwa mule ndani, wachimbaji wawe mule ndani, mchimbaji akipata mali hata kama amedhaminiwa atamuuzia tajiri wake na tajiri wake atalipa ushuru maana watu wa TRA watakuwa ndani pia. Hivyo mchimbaji hataweza kutoka na mali nje, na wanunuzi watatoka na mali yao ambayo wamenunua na wameshalipia ushuru.
Hii itakuwa kwa tanzanite tu au migodi yote?
 
Jana Rais John Magufuli aliamuru kujengwa ukuta kuzunguka eneo la Mererani na kulinda madini ya adimu duniani ya Tanzanite ili kuwezesha upatikanaji wa kodi itokanayo na mauzo ya madini hayo kwa urahisi.

Ukuta huo utakaokuwa na urefu wa kilomita za mraba 15, utazuia eneo la kilomota za mraba 81.99 na litazuia maeneo yote ya uchimbaji ya A, B, C, na eneo D.

Sambamba na ukuta huo pia kutajengwa barabara nzuri ya lami ambayo itatokea kwenye machimbo hayo hadi uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro yaani KIA.

Uamuzi wa kujengwa kwa ukuta huo inasemwa kwamba umechelewa yaani kwamba ukuta huo ulipaswa kujengwa mwaka 2002 baada ya timu ya washauri wa kitanzania na wawakilishi wa wanunuzi wakubwa wa madini hayo kuafiki kwamba kulikuwa na haja ya kujengwa kwa ukuta huo kwa wakti ule.

Timu hiyo iloitwa Tanzanite Tueson Protocol ilishauri kujengwa ukuta huo kudhibiti biashara haramu ya madini hayo na mitandao yake yote.

Hiyo ilitokana na mabadiliko mbalimbali ya sheria za kuhusiana na ugaidi katika nchi mbalimbali baada ya ripoti mbalimbali kuhusisha biashara ya hiyo ya madini na masuala ya ugaidi ambapo kiongozi wa magaidi duniani kwa wakati huo Osama Bin Laden alikuwa akihisiwa kujishirikisha na biashara hiyo.

Kujengwa kwa ukuta huu kutadhibiti si tu wafanya biashara halali bali pia wafanyabiashara wenye leseni na kuondoa biashara haramu ya magendo ya madini hayo.

Tanzanite ni madini ambayo yanapatikana nchini Tanzania pekee na yana soko kubwa nchini Marekani kiasi cha asilimia 99.

Lakini madini hayo yanasafirishwa moja kwa moja kwenda nchini Marekani kupitia katika nchi za Thailand, Kenya na India huku serikali ya Tanzania kwa miaka Zaidi ya 15 ikiwa inakosa mapato yake halali kutokana na upotevu huo.

Kujengwa kwa ukuta huo pia kutasaidia shughuli hizo za uchimbaji kudhibitiwa kirahisi, kupatikana fursa nzuri za wafanyabiashara wa katika maeneo hayo kama mama ntile na migahawa mingine, mahoteli, klabu za usiku na hata biashara za magari!

Biashara zote hizi zinawezesha kupatikana kwa kodi za mapato kwa kuwa wafanyabiashara hawa wote watakuwa wamesajiliwa rasmi katika mfumo wa TRA kwa wote kuwa na namba maalum za TIN.

Pia mgodi huo wa Marerani utawezesha wafanyabiashara waingizaji wa vifaa mbalimbali vya uchimbaji wa madini hayo kutoka nje ya nchi kuweza kufanya hivyo kuwa kutumia mfumo mmoja wa anuani ya eneo hilo hivyo hata kama mtu anaagiza mzigo kutoka marekani, au Uchina basi uaandikwa anuani ya Mererani.

Je, mwana JF unachukuliaje uamuzi huu wa kujengwa kwa ututa kudhibiti eneo lote za Mererani?

Je, faida zake zingine kubwa ni zipi?

Je , kuna hasara yoyote ile?

Tafadhali toa maoni yako bila kuingiza siasa.

Kama kawaida yangu napenda majadiliano yenye tija.

Karibu.


WanaJF nisaidieni kuelewa .
Urefu wa ukuta
" 15 kilomita za mraba " kweli nimelewa
 
WanaJF nisaidieni kuelewa .
Urefu wa ukuta
" 15 kilomita za mraba " kweli nimelewa

Ni eneo la kilomita za mraba 15 na siyo urefu.

Ahsante kwa kuiona hiyo hiyo kasoro na nimerekebisha .
 
Vp awa jamaa zetu masai na wajaluo wanaouza madini madogomadogo wataendelea kuwepo mjini au ndo safari ya kurudi kijijini itaanza

Nadhani wakiwa wako sawa wataendelea na biashara kwa uwazi kabisa.
 
Kwanza kabisa ngoja nieleze kidogo utamaduni wa uchimbaji madini kwa mtu mmoja mmoja unavyofanyika Tanzania, wachimbaji wengi wanakuwa wamedhaminiwa, tajiri anaweza kuwa yuko Arusha,mzawa au mgeni ( foreigner), akishamzamini mchimbaji pesa ya kununua vifaa vya uchimbaji na chakula kwa makubaliano ya ukipata mali lazima uniuzie mimi, mchimbaji akienda kuchimba na akapata kiasi lets say gram 1,wataangalia leo bei inasemaje, pengine ni 50 usd, tajiri atatoa pesa yake kwanza aliyomdhamini mchimbaji kama ni usd 20, then kinachobaki 30 anampatia mchimbaji na yeye anachukua mali. Lakini mchimbaji huyu akipata mali hupeleka mzigo kwa tajiri aliyemdhamini, wewe hata ukiwa na kampuni yako ya ununuzi uko eneo la tukio mchimbaji hawezi kukuuzia, kama yuko hotelini huyo tajiri mali itamkuta huko, hivyo tajiri anaweza asiwe hata ni vibali vya ununuzi au license yeyote kutoka serikalini na akaweza kupata mali kila siku kutoka kwa wachimbaji, baada ya miezi kadhaa tajiri mzigo wake umekuwa mwingi huyo anasafirisha, hivyo serikali inakosa mapato . Lakini kwa njia hii ya uzio na biashara ifanyike ndani ya eneo hilo, maana itawalazimu wafanyabiashara wote wawe na vibali husika kutoka serikali kuwa mule ndani, wachimbaji wawe mule ndani, mchimbaji akipata mali hata kama amedhaminiwa atamuuzia tajiri wake na tajiri wake atalipa ushuru maana watu wa TRA watakuwa ndani pia. Hivyo mchimbaji hataweza kutoka na mali nje, na wanunuzi watatoka na mali yao ambayo wamenunua na wameshalipia ushuru.

Mkuu, ahsante sana kwa maelezo mafupi na mazuri yalojitosheleza.

Hii ndiyo JF tunayoitaka.

Dhima kuu ni kusanyaji wa mapato kupitia wachimbaji, wauzaji na wanunuzi yaani madalali wa ndai na nje ya nchi,

Safi kabisa.
 
Ukuta sawa lakini unajengwa juu ya ardhi haujengwi nchini ya ardhi.Huko ardhini inaweza kujengwa tunnel ya kutokea nje ya ukuta huo na madini kutoroshwa.Natoa angalizo kwa serikali kama mtaalam wa Sekta ya madini.Hapo Mererani huko chini migodi inaingiliana wanaita "mitobozano",huo ukuta wa juu unaweza usisaidie sana madini yanaweza kupita chini kwa chini na kuvuka huo ukuta kwenda vitalu vingine ambavyo siyo A,B,C wala D.Kwangu mm ningekuwa Serikali ningejenga ukuta eneo lote la Mererani na kufanya patrol mita 100-200 kuzunguka huo ukuta kuhakikisha kwamba hakuna shimo lolote linatokeza nje ya Ukuta huo.Aidha,madini ya Tanzanite ningeyafanya nyara ya Serikali.Ukikutwa nayo isivyo halali,wafa.

Na hilo ndilo lengo kuu ya serikali hii ya awamu ya tano kuzuia njia za panya.

Kinachofanyika twaweza kukiita kwa kiingereza "Transformation in mining sector" yaani mabadiliko katika udhibiti katika sekta ya madini.

Yaani ni poa sana.
 
Mi huwa nachoka kusapoti chochote kile maana hamna accountability. Yaani zitakusanywa za kukusanywa na hutosikia matumizi.

Ila miaka hii tutajenga hadi tukome.

Twajenga kaw ajili ya vizazi vijavyo au siyo?
 
Je, CCM inaweza kuondokana kabisa na ufisadi?

je uongozi wake sasa hivi upo vipi?

Je, vipi kuhusu uwezo wao CCM ya sasa kiutendaji?
Kwa Tanzania yetu: ufisadi ni CCM, na CCM ni ufisadi. Hivyo kujibu maswali yako: a) CCM haiwezi kuondoka na ufisadi kwani ufisadi ndiyo CCM; b) uongozi wa sasa zaidi ya kupiga kelele na kutumia bunduki kuua nzi, ufisadi bado unaendelea. Magufuli ku-personalise taratibu za manunuzi ya umma bila kufuata sheria: Bunge kuidhinisha bajeti, na government tendering kufuata; na c) uwezo wa kiutendaji wa CCM actually ni mbovu ever, kwani hali ya umaskini imekuwa mbaya, huku walio kwenye network ya Magufuli wakila kuku kwa mlija pamoja naye.
 
Huwezi kuzuia kwa asilimia 100 kila ujanja wa wananchi lakini ukuta utasaidia kwa kiasi kikubwa.
Nimesema humu, Magufuli is too mechanical! Kinguge alikuwa sawa kumwita nyapala! Sasa nyapala akipata managerial position, matokeo yake ndiyo hayo.

Seriously, chifu unaamini ukuta ndiyo suluhisho la wizi na ukwepaji kodi? Mbona bandarani kuna ukuta, lakini mpaka kesho wizi unaendelea? Mbona kwenye migodi ya Acacia kuna kuta za kufa mtu, lakini 'wizi' bado unaendelea? Magufuli analindwa masaa 24, lakini bado anaweza kufanya ufisadi kwa ku-personalise manunuzi ya serikali!!
 
Kule ndan

Nikuondoe hofu, hilo wazo lako pia ni gumu sana kwa utekelezaji wake, kumbuka kuwa baada ya serikali kugundua hila kadha wa kadha ninaamini watapenyeza ma shushushu lukuki watakaoajiriwa pale kama wafanyakazi ambao hawatakua wakijuana, hii imetumika sana kwenye makampuni ya ujenzi wa barabara hapa nchini
Mashushushu hawa TISS ama? Mbona wapo hadi Ikulu lakini ufisadi ulikuwepo na unaendelea kuwepo?
 
Jana Rais John Magufuli aliamuru kujengwa ukuta kuzunguka eneo la Mererani na kulinda madini ya adimu duniani ya Tanzanite ili kuwezesha upatikanaji wa kodi itokanayo na mauzo ya madini hayo kwa urahisi.

Ukuta huo utakaokuwa na urefu wa kilomita za mraba 15, utazuia eneo la kilomota za mraba 81.99 na litazuia maeneo yote ya uchimbaji ya A, B, C, na eneo D.

Sambamba na ukuta huo pia kutajengwa barabara nzuri ya lami ambayo itatokea kwenye machimbo hayo hadi uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro yaani KIA.

Uamuzi wa kujengwa kwa ukuta huo inasemwa kwamba umechelewa yaani kwamba ukuta huo ulipaswa kujengwa mwaka 2002 baada ya timu ya washauri wa kitanzania na wawakilishi wa wanunuzi wakubwa wa madini hayo kuafiki kwamba kulikuwa na haja ya kujengwa kwa ukuta huo kwa wakti ule.

Timu hiyo iloitwa Tanzanite Tueson Protocol ilishauri kujengwa ukuta huo kudhibiti biashara haramu ya madini hayo na mitandao yake yote.

Hiyo ilitokana na mabadiliko mbalimbali ya sheria za kuhusiana na ugaidi katika nchi mbalimbali baada ya ripoti mbalimbali kuhusisha biashara ya hiyo ya madini na masuala ya ugaidi ambapo kiongozi wa magaidi duniani kwa wakati huo Osama Bin Laden alikuwa akihisiwa kujishirikisha na biashara hiyo.

Kujengwa kwa ukuta huu kutadhibiti si tu wafanya biashara halali bali pia wafanyabiashara wenye leseni na kuondoa biashara haramu ya magendo ya madini hayo.

Tanzanite ni madini ambayo yanapatikana nchini Tanzania pekee na yana soko kubwa nchini Marekani kiasi cha asilimia 99.

Lakini madini hayo yanasafirishwa moja kwa moja kwenda nchini Marekani kupitia katika nchi za Thailand, Kenya na India huku serikali ya Tanzania kwa miaka Zaidi ya 15 ikiwa inakosa mapato yake halali kutokana na upotevu huo.

Kujengwa kwa ukuta huo pia kutasaidia shughuli hizo za uchimbaji kudhibitiwa kirahisi, kupatikana fursa nzuri za wafanyabiashara wa katika maeneo hayo kama mama ntile na migahawa mingine, mahoteli, klabu za usiku na hata biashara za magari!

Biashara zote hizi zinawezesha kupatikana kwa kodi za mapato kwa kuwa wafanyabiashara hawa wote watakuwa wamesajiliwa rasmi katika mfumo wa TRA kwa wote kuwa na namba maalum za TIN.

Pia mgodi huo wa Marerani utawezesha wafanyabiashara waingizaji wa vifaa mbalimbali vya uchimbaji wa madini hayo kutoka nje ya nchi kuweza kufanya hivyo kuwa kutumia mfumo mmoja wa anuani ya eneo hilo hivyo hata kama mtu anaagiza mzigo kutoka marekani, au Uchina basi uaandikwa anuani ya Mererani.

Je, mwana JF unachukuliaje uamuzi huu wa kujengwa kwa ututa kudhibiti eneo lote za Mererani?

Je, faida zake zingine kubwa ni zipi?

Je , kuna hasara yoyote ile?

Tafadhali toa maoni yako bila kuingiza siasa.

Kama kawaida yangu napenda majadiliano yenye tija.

Karibu.
So far so good,ni hatua nzuri sana! Ila ili tufaidi zaidi madini yetu ya Tanzanite,nashauri mambo yafuatayo.
1.Tanzanite One isiruhusiwe kusafirisha nje unpolished Tanzanite.Hii inatutia hasara sana.Inasemekana soko la Marekani peke yake linatengeneza faida ya zaidi ya dola za kimarekani million 500 kwa mwaka,bila kujali masoko mengine ya Ulaya,Asia na Australia! Pesa yote hii ingebaki hapa nchini kama tungeuza processed Tanzanite.Not forgetting of course the employment opportunities which would be created by the processing industry.
2.Kwa sasa Tanzanite One ndiyo inayo-certify minerals kutoka kwa wachimbaji.This is wrong.Hatujui kama Tanzanite One wana weledi unaotakiwa na pia kama wanafanya kazi hiyo kwa uaminifu.
Nashauri kiundwe kitengo maalum cha certification Wizara ya Nishati na Madini.Kitengo hiki kiwe na wataam wenye weledi na uaminifu wa hali ya juu.

3.Tuanze Training Programme ya wataalam kwa ajili ya processing & certification of Tanzanite kama hatujaanza.

We simply cannot sit by and look while our mineral resources are being stolen by the unscrupulous so called wawekezaji, kumbe ni vibaka tu.

Hongera sana Rais Magufuli kwa kuthubutu.
 
Nani kakudanganya? Tanzanite imepotea kwa sasa mpaka Tanzanite one wameamua kuuza mgodi.
Nani kakuambia inapimwa kwa maneno? Vipimo vimefanyika na Stamico, tanzanite ipo ya kutosha kwenye kitalu a mpaka d ambapo ndipo patawekewa ukuta, gharama za ujenzi wa hii miundombinu ni ghali sana usifikiri inafanyika kienyejienyeji.
 
Back
Top Bottom