mAgaziJuTO.
Senior Member
- Feb 22, 2014
- 119
- 37
Mimi ni mwalimu wa kawaida(msingi)Mshahara(soma posho) wangu kutokana na kufuta ujinga watoto wa kinyamwanga ni Tgts C1 ukitoa makato yote+deni la faidika ninabaki na 163,250 mkononi.Nina mke na watoto wawili+mama mzazi.Nimepanga uswahilini ambapo ninalipia 30,000 kwa mwezi(ukitoa kwenye 163,250 kinachobaki ndicho changu).mwezi uliopita nilipokea mshahara(soma posho)tarehe 26,hadi kufikia tar.10 april sikuwa na kitu,hivyo kutoka hapo hadi leo tar 20 naishi kwa mikopo na mizinga.Hadi leo nina deni lisilopungua 70,000 hivyo hadi kufikia mshahara(soma posho)sijui nitakuwa nimebaki na kiasi gani!hivyo nataka kujua,ualimu ni KAZI au SHUGHULI?