U hali gani Rafiki

Buswelu

JF-Expert Member
Aug 16, 2007
1,998
352

Mambo ni aje?

Nimekukumbuka ewe rafiki mwema mweledi. Mvumilivu asiyeua inzi kwa rungu. Anayejua kuwa leo ni kesho ya jana. Asiyeamini katika hali ya kumgoja chini aliyeko juu. Wewe unayejua kuwa kasi ya baiskeli inatokana na nguvu yako ya kunyonga pedeli.
Nakusalimia sana wewe ambaye ni mgumu kuingia ama kutoka mahali popote kama kotapini. Wewe ambaye unajua kuwa si kila mwenye pua kubwa anazo kamasi nyingi. Na unajua kabisa kuwa mwenye shavu kubwa kama .............. siye alikuibia bisi zako..
Nakusalimia sana...

Wasalaam,

Buswelu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom