Mkwaruzo
JF-Expert Member
- Feb 21, 2011
- 563
- 98
Mvua ndiyo hizi. Ni mategemeo yangu kuwa wakulima tumeipokea kwa mikono miwili na kuifurahia sana. Kwani ni matarajio yetu kuwa baada ya miezi kadhaa tutavuna mazao kedekede kutokana na mbegu tutazopandikiza ktk mashamba yetu. Lakini kwaku kuasana siyo vibaya, napenda kuitumia fursa hii kwa wakulima wenzangu. Haitopendeza kama mbegu zako utazipanda katika shamba ambalo siyo la kwako, kufanya hivyo ni kumdhulumu mwenye shamba kwani na yeye anafurahia apande akipendacho. Pia kuna mashamba ambayo siyo rasmi kupandwa mazao yeyote, hivyo tahadharini na kufanya uvamizi katika mashamba hayo, sheria kali zitachukuliwa kwa watakaokiuka agizo hili. Pia umakini uwepo ktk upandaji wa mbegu hizo, kwani haifurahishi kuona zinapandwa kinyume na inavyotakiwa. Pia natoa nasaha zangu kwa wale ambao hawana mashamba, wafanye haraka kwenda kuyanunua na kwa wauzaji wapunguze gharama za uuzaji. Mwisho kwa yale mashamba ambayo yapo tayari, basi inabidi yatendewe haki pia yatunzwe ili yasije kuvamiwa na magugu yakaja kugeukwa msitu. Jamani ni wajibu wetu kuitendea haki kauli mbiu ya Tz ya KILIMO KWANZA.
Ni hayo tu.
Ni hayo tu.