Two years in a row, J. Kikwete hatokuwepo Davos

Kweli kabisa, maana huyo aliyekuwa anatumbua lakini wafanyakazi alikuwa akiwalipa, wa vyeti feki wote walikuwa wanalipwa, nyongeza za mishahara zilikuwepo, ajira kibao, mikopo ya wanavyuo kama kawa. Sasa huyu mbona yanamshinda pamoja na kubana matumizi???
Suala la ajira na mishahara wakati wa JK mimi naweza kuwa shahidi mzuri manake niliona haya mambo kwa macho yangu baada ya kuwa nimeajiriwa na NMB 2 years earlier.

Enzi za Mkapa unaweza kupita hata mwaka bila kufungua akaunti yoyote ya mfanyakazi. Mkwere alipoingia madarakani ikawa kufungua akaunti za wafanyakazi wa serikali ni shughuli za kila wakati na mara kwa mara mnafungua kwa makundi manake unakuta manispaa imepokea wafanyakazi angalau 50 kwa mkupuo!

Kwenye mishahara sasa! Nakumbuka siku ya kwanza tunaingiza mishahara ya wafanyakazi kwenye akaunti zao (officially), walimu wa certificate wanaonza kazi walikuwa wanalipwa Sh. 60,100 na hiyo ilikuwa 2006.

Yaani hapo hata ukizingatia suala la inflation, bado utakuta hivi kawaacha wakiwa wanalipwa zaidi ya mara 3 ya alivyowakuta!

Yote 9, kumi studying opportunities! Kama kuna mtumishi wa umma hakuchukua digrii wakati wa JK then I doubt kama atachukua tena digrii maishani mwenzake!!
 
Bora yule mswahili anajua jinsi ya kufanya watu wake waishi huyu alieishi kwenye shida ana Roho mbaya sana hata kula Milo ya kawaida tuu hataki wale Nchi yenye rutuba kila sehemu...
 
Katika karne ya 21 ni muhimu kuhudhuria WEF Davos meetings. Akishindwa kwenda Rais basi washauri wakuu wa sera na mipango wanapaswa kwenda.

Wakati tunajifungia kwenye kiboksi chenye giza na ndoto ya "Tanzania ya viwanda" wenzetu wanazungumza 4th Industrial Revolution.
 
Muache JK apumzike bwana, JK aliyafanya yake zama zake za miaka 10 zimeisha sasa ni zamu ya JPM..

Jk alipanda ndege kwenda Davos na huko kwingine na sisi tulipanda sana ndege kwenda hong-kong,dubai,thailand,Guanzhou nk kariakoo ikawa mwayamwaya, wazambia, wacongo, wacomoro, waburundi, warwanda wakajazana kuja kununua na hoteli zote mjini Dar es salaama zikawa bize..

Bank watu wakakopa na kukopesheka wakazungusha hela na kulipa bank nazo zikawa bize, watu wakajenga majumba ya kifahari mafundi ujenzi wakawa bize mzunguko ukawafikia mpaka wa mikoani vijijini huko bibi na babu zetu tukawalea vizuri, viwanda wa cement na maduka ya vifaa vya ujenzi yakaota kama uyoga, watanzania wakawa sio waoga tena kwenda ughaibuni mpaka leo hii vijana wa uswahilini wengine wanaishi China, SouthAfrica, Dubai nk, muache JK apumzike bwana...

Au huoni magari yalivyopungua barabarani hapo Dar es salaama na jiji liko kimya kama limepigwa short ya umeme, wewe unafikiri ni hali ya kawaida..
Mkuu nauliza namba za magari inayoanza herufi "E" huko Dar yako? sasa tunaenda mwaka wa tatu huu herufi D bado ipo huku kwetu
 
DUSfOgfXkAE3sj5.jpg
 
Back
Top Bottom