VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Nimefarijika kuona rafiki yangu na Wakili Msomi mwenzangu Nyaronyo Mwita Kicheere akinisihi kupitia makala yake ya ----- kwenda Chalinze. Nimejiuliza vya kutosha juu ya kwanini hasa niende Chalinze na nilikache Bunge la Katiba hapa Dodoma. Nyaronyo amefanikiwa kunishawishi kwenda Chalinze. Naahidi ya kuwa kesho nitasafiri toka hapa Dodoma kwenda Chalinze,mkoani Pwani. Na matokeo ya Kalenga yatanikuta huko huko.
Chalinze patakuwa hapatoshi. Watu wa Pwani ambao wanaonekana kama wakumbatiaji wasiobadilika wa CCM watakuwa na nafasi adimu ya kuuonesha umma wa nchi hii rangi yao sahihi. Watashangilia na kuzomea bila woga kipindi chote cha kampeni. Wako tayari.Tayari kisiasa. Tayari kufa,tayari kupona
Wanawasubiri wanasiasa na sisi wafuatiliaji wa siasa wa nchi hii wafurike Chalinze. Waende kujieleza kwanini wawachague wao na wala si wengine.Waende na sera na si hela. Chalinze ya sasa si ile ya zamani. Chalinze kutakuwa na hoja za haja na vihoja vya kutongoja. Wagombea wote wa vyama vyote vya Chalinze wako tayari na imara. Wameshahika ajenda zao na kuandaa sauti zao kwenda kusikika.
Kwa Chalinze ya sasa niijuayo, ngumu kubashiri. Mchanganyiko wa makabila na kipato cha waishio pale ndivyo vinitishavyo katika utabiri wangu. Siwezi na sitaki kutabiri. Shime twendeni Chalinze.Taarifa tutakazozitoa mitandaoni zikosolewe kwa ushahidi na si vinginevyo.
Torongey namjua.Ridhiwani namjua. Wa CUF namsikia tu. Nani atasema na kuvuna nini Chalinze? Twendeni tukashuhudie. Si uchaguzi wa kubeza pale ambapo mtoto wa Rais anagombea Ubunge. Kukosolewa kwa Mgombea wa aina hiyo ni kukosolewa kwa chama chake na hata familia yake. Nyaronyo amesema:hapatatosha. Hata mimi naamini.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma na kuanzia kesho Chalinze)
Chalinze patakuwa hapatoshi. Watu wa Pwani ambao wanaonekana kama wakumbatiaji wasiobadilika wa CCM watakuwa na nafasi adimu ya kuuonesha umma wa nchi hii rangi yao sahihi. Watashangilia na kuzomea bila woga kipindi chote cha kampeni. Wako tayari.Tayari kisiasa. Tayari kufa,tayari kupona
Wanawasubiri wanasiasa na sisi wafuatiliaji wa siasa wa nchi hii wafurike Chalinze. Waende kujieleza kwanini wawachague wao na wala si wengine.Waende na sera na si hela. Chalinze ya sasa si ile ya zamani. Chalinze kutakuwa na hoja za haja na vihoja vya kutongoja. Wagombea wote wa vyama vyote vya Chalinze wako tayari na imara. Wameshahika ajenda zao na kuandaa sauti zao kwenda kusikika.
Kwa Chalinze ya sasa niijuayo, ngumu kubashiri. Mchanganyiko wa makabila na kipato cha waishio pale ndivyo vinitishavyo katika utabiri wangu. Siwezi na sitaki kutabiri. Shime twendeni Chalinze.Taarifa tutakazozitoa mitandaoni zikosolewe kwa ushahidi na si vinginevyo.
Torongey namjua.Ridhiwani namjua. Wa CUF namsikia tu. Nani atasema na kuvuna nini Chalinze? Twendeni tukashuhudie. Si uchaguzi wa kubeza pale ambapo mtoto wa Rais anagombea Ubunge. Kukosolewa kwa Mgombea wa aina hiyo ni kukosolewa kwa chama chake na hata familia yake. Nyaronyo amesema:hapatatosha. Hata mimi naamini.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma na kuanzia kesho Chalinze)