Maisha ni mechi/na muda ndio refaree
Utasotea benchi/kazana ongeza bidii
Pia maisha ka kitasa/na elimu ndio ufunguo
Usi force kuishi kisasa/ujana utakuvua nguo
Baro achana na usharo/ujana usikutie kiburi
Jobless chimba hata mtaro/kama umekosa shughuli
Ukubwa si kutoka jando/na kujua kutongoza
Ubishoo uweke kando/ukizubaa utakuponza
Ladha ya chai sukari/majani yanaweka rangi
Ukipenda vitu vizuri/ubakhili mwachie mangi.
Utozi si supra na gucci/kwanza tafuta chapaa
Bidada hukuficha uchi/Iweje ukatae kuzaa
Ya plus maisha/bila kuingizwa kambini
Majembe utawalimisha/pasi waingiza mipini
Tambua, harusi yamalaya/ni msiba kwa alo walaghai
Acha kuishi kiyahaya/jiji litakutoa nishai
Kumbuka,maisha ni msamiati/na elimu ndio kamusi
Soma panga mikakati/ujinga zigo la nuksi
Umasikini chuo cha msoto/walohitimu wamejifunza
Mkubwa wa jiko ni moto/chunvi madini ya uvinza.....,..,,..