LESIRIAMU
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 8,721
- 13,959
Majimbo mengi yana wabunge ambao wapo kwa miaka mingi na wengine hata 10. Lakini hakuna alama yeyote ya kazi zao zaidi ya zile zilizofanywa na serikali pamoja na kuwa na nafasi kubwa ya kufanya shughuli za maendeleo jimboni wao binafsi.
Pesa wanazodanganya watu kuwapa zawadi zingeweza kufanya kazi za kusaidia jamiii katika sekta za afya, elimu, kilimo, miundombinu nk
Kwa mfano Jimbo la Iramba Magharibi, kuna mtu makini sana katika kuleta maendeleo anaitwa Eng. Jumbe Katala. Ni msomi mzuri sana na alipogombea mwaka 2010 kura hazikutosha lakini akaendelea kufanya kazi za maendeleo jimboni na sasa amekamilisha kujenga shule ya kidato cha tano ja sita inayoitwa Katala High School na itasaidia sana kuelimisha vijana wamaomaliza kidato cha nne bila kujua wataendeleaje na masomo kwa kwa nafasi ni chache.
Eng. Katala kawa mkombozi kielimu na anasema atajenga shule za high school katika kila tarafa na mengine mengi amechangia hata katika Chama cha Mapinduzi.
Ana upeo mkubwa sana wa kutuvusha wana Iramba kimaendeleo. Amesoma uhandisi shahada ya kwanza chuo kikuu maarufu cha Cantebury kule Christchurch New Zealand na ya pili kule chuo kikuu cha Delft nchini Uholanzi. Ni shujaa wa miundo mbinu na kafanya kazi Wizara ya Ujenzi, Tanroads na Dart Agency akiwa meneja wa mradi wa mwendokasi ambao kwa sasa jiji la Dar linanufaika. Akaenda kufanya kazi Bank ya Maendeleo Africa (African Development Bank) na kufanikisha nchi kupata fedha za kujenga mwendokasi awamu ya pili kutoka katikati ya jiji hadi Mbagala, mradi ambao unaendelea kujengwa. Pia amefanikisha nchi kupewa fedha katika miradi mingine mingi hapa Nchini.
Sasa Jumbe Katal huyu ndiye anatufaa ubunge Iramba Magharibi na sio wabunge wa mbwembwe nyingi. Sasa ni wakati muafaka wa kuwauliza wanaowania ubunge Iramba kuwa wameifanyia nini Iramba mbali na miradi iliyofadhiliwa na Serikali? Wana Iramba tumtafute Mhandisi Katala aje kuchukua jimbo hili ambalo tunaona watu wanafanya mbwembwe tu. Ana maono sana na Iramba na meaka 2010 alisema atahakikisha Iramba inakuwa na Benki yake ili kuinua uchumi wa Iramba kwa kukopesha wana Iramba kwa riba nafuu ili kufanikisja sghuli za kimaendeleo katika fani zote.
Waliopo wameshindwa hata kutumia maono haya na kazi yao ni kucheza cheza dansi majukwaani tu na kugawa vizawadi vya hapa na pale visivyokuwa na tija kimaendeleo.
Ni zamu ya Eng. Jumbe Katala atuvushe wana Iramba Magharibi.
Pesa wanazodanganya watu kuwapa zawadi zingeweza kufanya kazi za kusaidia jamiii katika sekta za afya, elimu, kilimo, miundombinu nk
Kwa mfano Jimbo la Iramba Magharibi, kuna mtu makini sana katika kuleta maendeleo anaitwa Eng. Jumbe Katala. Ni msomi mzuri sana na alipogombea mwaka 2010 kura hazikutosha lakini akaendelea kufanya kazi za maendeleo jimboni na sasa amekamilisha kujenga shule ya kidato cha tano ja sita inayoitwa Katala High School na itasaidia sana kuelimisha vijana wamaomaliza kidato cha nne bila kujua wataendeleaje na masomo kwa kwa nafasi ni chache.
Eng. Katala kawa mkombozi kielimu na anasema atajenga shule za high school katika kila tarafa na mengine mengi amechangia hata katika Chama cha Mapinduzi.
Ana upeo mkubwa sana wa kutuvusha wana Iramba kimaendeleo. Amesoma uhandisi shahada ya kwanza chuo kikuu maarufu cha Cantebury kule Christchurch New Zealand na ya pili kule chuo kikuu cha Delft nchini Uholanzi. Ni shujaa wa miundo mbinu na kafanya kazi Wizara ya Ujenzi, Tanroads na Dart Agency akiwa meneja wa mradi wa mwendokasi ambao kwa sasa jiji la Dar linanufaika. Akaenda kufanya kazi Bank ya Maendeleo Africa (African Development Bank) na kufanikisha nchi kupata fedha za kujenga mwendokasi awamu ya pili kutoka katikati ya jiji hadi Mbagala, mradi ambao unaendelea kujengwa. Pia amefanikisha nchi kupewa fedha katika miradi mingine mingi hapa Nchini.
Sasa Jumbe Katal huyu ndiye anatufaa ubunge Iramba Magharibi na sio wabunge wa mbwembwe nyingi. Sasa ni wakati muafaka wa kuwauliza wanaowania ubunge Iramba kuwa wameifanyia nini Iramba mbali na miradi iliyofadhiliwa na Serikali? Wana Iramba tumtafute Mhandisi Katala aje kuchukua jimbo hili ambalo tunaona watu wanafanya mbwembwe tu. Ana maono sana na Iramba na meaka 2010 alisema atahakikisha Iramba inakuwa na Benki yake ili kuinua uchumi wa Iramba kwa kukopesha wana Iramba kwa riba nafuu ili kufanikisja sghuli za kimaendeleo katika fani zote.
Waliopo wameshindwa hata kutumia maono haya na kazi yao ni kucheza cheza dansi majukwaani tu na kugawa vizawadi vya hapa na pale visivyokuwa na tija kimaendeleo.
Ni zamu ya Eng. Jumbe Katala atuvushe wana Iramba Magharibi.