'Tuzo' au 'tunzo', wataalam wa lugha tafadhali

'Tuzo' au 'tunzo', wataalam wa lugha tafadhali

Makini

Senior Member
Joined
Dec 23, 2014
Posts
154
Reaction score
59
Kwa muda sasa nimekua nikisikia watu mbali mbali wakisema 'mtu anapewa au anatunikiwa tunzo fulani'. Mimi kwa uzoefu wangu najua kwamba hilo neno ni Tuzo, lakini sasa kutokana na watu wengi sana kuongeza hiyo herufi n hapo katikati, naanza kupata mashaka kwamba huenda neno sahihi ni tunzo.

Wataalamu wa lugha, uhakika uko wapi? Tuzo au tunzo.

Natanguliza shukrani.

 
Neno sahihi ni TUZO na si TUNZO,juzi kwenye KTMA Zembwela alikuwa ananichefua alipokuwa akitamka Tunzo,mara ni mmoja kati ya kijana badala ya vijana
 
Mimi bado napata gagaziko kama sio uvulivuli ktk hayo maneno. Tuangalie mfano wa sentensi hiz halafu tuseme ipi sahihi
1; Sasa ni zamu ya kumtunza mama wa bi harusi.
2;Sasa n zamu ya kumtuza mama wa bi harusi.
Sasa tuone hapo ipi sahihi ndipo tuseme ipi sahihi
 
Tusitumie uzoefu kudadavua maana hizo. TUNZO na TUZO ni kitu kilekile ikiwa na maana maana mbili. maana ya kwanza ni KITU KINACHOTOLEWA KUWA NI ZAWADI ANAYOPEWA MTU BAADA YA KUFANYA JAMBO ZURI. Pili, FICHUO au UVUMBUZI.
[Rejelea kamusi ya Kiswahili Sanifu ukurasa wa 415]
 
Back
Top Bottom