Tuwekane sawa kuhusu oral interviews hapa.

Tuwekane sawa kuhusu oral interviews hapa.

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
31,206
Reaction score
88,986
Habari wakuu.
Najua wapo wengi kama mimi hatujawahi udhuria ata oral interview moja, maana ndio tume graduate sio muda. Lakini kwakua humu ndani kuna watu washawahi udhuria nyingi tu (serikalini na private sectors), na ata wengine ni mameneja au ma-hr wanaohusika na haya mambo, tunaombeni msaada wenu hapa.

Tutaenda kwa maswali, kama utaliweza tunaomba ulijibu moja au ata mengi kati ya haya na watakao ongeza wadau hapa chini:

1. Tufanye ndio nimeitwa interview. Ni vitu gani siku ile inabidi niende navyo? Kuna baadhi ya job vacancy zikitangazwa wanasema kabisa siku ya usaili njoo na vyeti. Je, kuna aja ya kwenda na CV na cover ltter tena? Je, naweza kwenda na plain paper, mfano wakiniuliza swali naanza kujibu kwa kuwachorea ili waelewe vema??

2. Average kunakua na interviewers wangapi? Najua namba sio constant, ila wanaweza kuzidi wa5? Maana wakiwa wengi unakua unashambuliwa sasa. Dah.

3. Ukiingia chumba cha interview, vipi kuwasalimia kuna haja ya kuwapa mkono? Au salam moja tu kwa wote mfano good morning, inatosha? Na nikikaa kwenye kiti, naanza kujieleza au nisubiri wanichokoze? vipi wakikaa kimya wananiangalia tu. Naweza kimbia mm.

4. Vipi kuhusu utani. Katikati ya interview unaweza ingizia utani?

5. Na je, mara nyingi wale interviewers wanakua wataalamu wa nilichosomea mm au wanaweza kua sio? Mfano, nimeitwa intetview ya civil engineer, je wao wanakua ma civil eng au wanaweza kua wengine tu?
Na maswali yao vipi? Yanakua ya darasani sanasana au?

Wadau nitapenda mkiongeza maswali na wataalamu tutapenda mtujibu.

Shukrani.
 
Kila interview ina mahitaji yake. Barua ya mwaliko wa interview itakyambia na wakinyamaza waulize. Dont asume. Idadi ya interviewer inategemea ba muundo na nafasi inayoombwa.
Public sector ina watu wengi ukilinganisha na private sector. Nimewahi kuwa interviewed na watu 8 (public) na pia na mtu 1(private).
Kuna mitandao mingi ya maswala ya interview. Browse the net.
 
1. Elimu uliyo ipata haijakusaidia kwani imekunyima ujasiri na kujiamini kwa kile ulicho somea!
2. Kwenye panel si zaidi ya 5 mara nyingi .
3.Na vilevile kwenye panel kunaweza kuwa na mtaalam wa fani hyo 1 au 2 na wengine na wengine wakakuhoji mambo ya kijamii, kiutawala na mengineyo kukupima uelewa wako wa kutatua maswali.
4. barua ambatanishi si muhimu sana ila vyeti na Cv vyaweza tumiwa.
5. Vile hakuna mtilikio wa maswali ya ufanane kwa fani mbalmbal swali ambalo ni very common ni ( explain your self,let us know you.........)
6. overconfidence haitakiwi wala belowconfidence haitakiwa be constant kama pai.
7 polite language iz very ......
8.wasipo kwambia karb kit waweza uliza tafadhali naweza kaaaaa.
kwa leo inatosha kwa mawasilano tumia 0765
 
Maintain eye to eye contact,balance your confidence not over or under confidence,professional handshaking is highly advised,itafute google in resources nyingi na video clip za kukusaidia.
 
Kila interview ina mahitaji yake. Barua ya mwaliko wa interview itakyambia na wakinyamaza waulize. Dont asume. Idadi ya interviewer inategemea ba muundo na nafasi inayoombwa.
Public sector ina watu wengi ukilinganisha na private sector. Nimewahi kuwa interviewed na watu 8 (public) na pia na mtu 1(private).
Kuna mitandao mingi ya maswala ya interview. Browse the net.

Watu 8 dah si kama ugomvi sasa.
Ok. Nadhani maswali watakua wanauliza kwa mpangilio na si kama kirabuni.

Je, swali moja inabidi nijibu kwa zaidi ya dakika 3 kweli? ie. Majibu ni short na maelezo kidogo au ndio full explanations tu.

Nilishawahi sikia kuna badhi hawapendi wewe uwe muongeaji sana. Wana penda mtu una hit point na nyama kidogo.
 
Thanks wakuu. Mmeshauri niingine net, nimecheki kidogo.
Kuna hii issue ya mavazi.
Wana shauri mavazi kuvaa inategemeana na nafasi yako unayoipigania. Mtu wa mambo ya mining, technician, eng mavazi yake ni tofauti na wa Human Resoc, Acc etc.

Pia katika mavazi wameshauri usiongezee vitu visivo vya ziada kama Kofia, cheni, "kacha za kimasai zile", miwani ya jua, au usijipulizie marashi yale yenye harufu kali.

Pia usiende na vitu visivo vya lazima kama maji, au kinywaji chochote, gazeti, ikiwezekana ata simu weka silent ata kama mpo chumba cha kusubiri,

Na ukifika eneo la tukio, kwanza wanasema usiwahi sana, mfano interview inaanza saa 10am sio poa eti ww unafika saa 8am na kuanza kuzagaa zagaa bila mpangilio, angalau saa 9:40am hivi fresh na pia usichelewe sana. Eti wengine wmeshaanza kuingia ww ndio unafika. Hii tabia sana wanawake ndio wanayo.

Mwenye ya ziada please..
 
Nlienda interview moja juzi kati ya shirika la umma walikua kama mia mule ndani na kila mtu alikua na swali anauliza,then mmoja anaandika marks kwny karatasi yake kila ukijibu.

Kitendo cha kuingia tu hadi kukaa tayari wakaniwekea marks.

Kuna wale wa karibu nlikua nikitupia jicho naona marks wanazonipa..2 ya kumi,maswal mengne 5,mengne 8.

Waliniuliza kila kitu.
-everythng kuhusu my undergraduate dissertation
-who am i?
-what do i expect frm them if i get employed?
-Their organisation structure
-Their mission and vision
- what was my greatest failure?
-whether i am married/unmarried/dating and why?
Mengine mpaka nkikumbuka. Ila nlitoka nimelowa jasho. I made it tho.
 
Interview za wabongo wanakompliketi sana na kufuata sheria nyiingi ili wakukwamishe.
Za wenzetu yani ni simple tu na za kishkaji.
 
Nlienda interview moja juzi kati ya shirika la umma walikua kama mia mule ndani na kila mtu alikua na swali anauliza,then mmoja anaandika marks kwny karatasi yake kila ukijibu.

Kitendo cha kuingia tu hadi kukaa tayari wakaniwekea marks.

Kuna wale wa karibu nlikua nikitupia jicho naona marks wanazonipa..2 ya kumi,maswal mengne 5,mengne 8.

Waliniuliza kila kitu.
-everythng kuhusu my undergraduate dissertation
-who am i?
-what do i expect frm them if i get employed?
-Their organisation structure
-Their mission and vision
- what was my greatest failure?
-whether i am married/unmarried/dating and why?
Mengine mpaka nkikumbuka. Ila nlitoka nimelowa jasho. I made it tho.

Eeehhhhh... Hapo hapo... Kwa idadi hiyo ulivoingia uliwasalimiaje? hand'shaking or jus good mornng? Kuna anybody alikuinvite ukae kwenye kiti au ulijirushoa tu.

Umesema marks tokea unavoingia zikatolewa. Did you mean style ya kubisha hodi, muonekano na mavazi, mwendo na salam au? kidogo tupe mwanga mzee, maana umetuambia tu yaliokukuta na sio ulichofanya..
 
Kuna mshkaji aliniambia alienda interview. Ikafika zamu yake akaitwa kwenye chumba. Kubisha hodi akaambiwa karibu. Anafungua mlango ndani giza tororo. Haoni kitu. Akajiuliza apapase pembeni ya mlango kama kuna switch au? Akili ikakmtuma achukue Nokia tochi yake akawasha. Kumulika mbele mijitu kibao. Akawasalimia hafu akawaambia poleni na giza. Walibaki wanacheka sana. Wakamsifu kwa kua na Plan B. Kumbe switch walikua nayo karibu, wakawasa mambo yakaendelea.
Sijui alikua ananitania au yuko serious.
 
Secret Service It's funny nkikumbuka nacheka. Hayo ya uingieje au ufanyaje tunaita ettiquete katika fani yetu sie. Inajumuisha vitu vingi hadi mavazi,mwonekano etc jaribu kugoogle.

Mie nlifatwa nje na admin officer. Tukaingia wote ndani. So sikunock mlango. Nlivoingia Nkazubaa kdogo nt knowing what to do or where to sit mpaka panel chair akanambia welcome. Nkawambia Goodmorning. Wakaitikia. Then huyo chairlady akanambia,"please,have a seat," huku akinionesha vacant seat,nkakaa.

Hapo nkachungulia panelist wa karibu wamenipa 4/10 na mwingne 5/10. I was shocked. They couldn't have been that unfair,not after every attempt I made wth ettiquete. I was tense.

Before I calmed,chairlady akaanza kutambulisha kila panelist. It was so boring and tedious maana walikua kama mia like I said.

Before I realised it was over, nkaskia naulizwa,"Briefly,tell us who you are".
Uzuri nlifanya utafiti jana yake hw to answer that qn. So nkajibu fresh. Nkachungulia the guy who gave me 5/10 for ettiquete earlier akanipa 8/10 this time. I chuckled. It sort of boosted my confidence and i rose up to the threshold.

Ndo maswali yakaendelea one after the other.
 
Last edited by a moderator:
Kuna swali moja nilikuwa najiuliza kila siku how best to answer. Nimegundua hivi karibuni.

Ukiulizwa if your boss cant see your solution from the angle that you do, and you believe that you are correct. What will you do?

Nadhani best way to approach it ni kusema i will insist with evidence and best practices where it worked. But in the end of the day we succed or fail as a team. I will be watchfull throughout and try to see if there is anywhere i can rescue the situation before worse comes to the worst.
 
Kuna mshkaji aliniambia alienda interview. Ikafika zamu yake akaitwa kwenye chumba. Kubisha hodi akaambiwa karibu. Anafungua mlango ndani giza tororo. Haoni kitu. Akajiuliza apapase pembeni ya mlango kama kuna switch au? Akili ikakmtuma achukue Nokia tochi yake akawasha. Kumulika mbele mijitu kibao. Akawasalimia hafu akawaambia poleni na giza. Walibaki wanacheka sana. Wakamsifu kwa kua na Plan B. Kumbe switch walikua nayo karibu, wakawasa mambo yakaendelea.
Sijui alikua ananitania au yuko serious.

hii mpya katika experience yangu ya utafutaji wa ajira,hii sijaisikia aisee.
 
Hizi interview watu wanapenda kuchezea watu akili,nilishawahi kuenda interview hapo maktaba kuu nikaulizwa maswali yangu vema,mwisho wakaniambia imba wimbo wa taifa nikaumba vizuri,nilipotoka njee katika kuhojiana na wenzangu wakaniambia uliimba nkasema ndio Je,ulikaa ama ulisimama??duh duh jasho wimbo niliimba nikiwa nimekaa,leo nafanya kazi benk ckuwahi itwa tena na TAESO.
 
nilienda interview moja swali la kwanza wakaniambia...why ur dreadlocks?nikasema nina zao wamejileta nilimwaga lecture mpaka wakaanza kutingisha vichwa,wakaniuliza je tukikupa kazi utanyoa raster zako...nikawapa jibu NO!mmoja akawa kama mkatis vile why hutaki ajira wewe?nika mjibu ajira nataka sana tu na ndo maana niko hapa ila ndugu waheshimiwa hizi raster ni imani yangu kama mlivyo na dini zenu na imani zenu,sithani kama kazi yangu inafanywa kwa imani yangu,pia na vigezo vyote muhimu mlivyo kuwa mnaitaji raster isiwe sababu kwani raster sio zinazo fanya kazi ni brain na skills nilizo nazo.wote wakapiga makofi.mmoja akaniambia u got gut..emeajiriwa.hahahhaa
 
Habari wakuu.
Najua wapo wengi kama mimi hatujawahi udhuria ata oral interview moja, maana ndio tume graduate sio muda. Lakini kwakua humu ndani kuna watu washawahi udhuria nyingi tu (serikalini na private sectors), na ata wengine ni mameneja au ma-hr wanaohusika na haya mambo, tunaombeni msaada wenu hapa.

Tutaenda kwa maswali, kama utaliweza tunaomba ulijibu moja au ata mengi kati ya haya na watakao ongeza wadau hapa chini:

1. Tufanye ndio nimeitwa interview. Ni vitu gani siku ile inabidi niende navyo? Kuna baadhi ya job vacancy zikitangazwa wanasema kabisa siku ya usaili njoo na vyeti. Je, kuna aja ya kwenda na CV na cover ltter tena? Je, naweza kwenda na plain paper, mfano wakiniuliza swali naanza kujibu kwa kuwachorea ili waelewe vema??

2. Average kunakua na interviewers wangapi? Najua namba sio constant, ila wanaweza kuzidi wa5? Maana wakiwa wengi unakua unashambuliwa sasa. Dah.

3. Ukiingia chumba cha interview, vipi kuwasalimia kuna haja ya kuwapa mkono? Au salam moja tu kwa wote mfano good morning, inatosha? Na nikikaa kwenye kiti, naanza kujieleza au nisubiri wanichokoze? vipi wakikaa kimya wananiangalia tu. Naweza kimbia mm.

4. Vipi kuhusu utani. Katikati ya interview unaweza ingizia utani?

5. Na je, mara nyingi wale interviewers wanakua wataalamu wa nilichosomea mm au wanaweza kua sio? Mfano, nimeitwa intetview ya civil engineer, je wao wanakua ma civil eng au wanaweza kua wengine tu?
Na maswali yao vipi? Yanakua ya darasani sanasana au?

Wadau nitapenda mkiongeza maswali na wataalamu tutapenda mtujibu.

Shukrani.


Dear Secret Service, there is nothing like "Oral Interview". Interview is always oral, so you cannot say oral interiview. Is the same as saying "repeate again". That is written test or screening test, sawa!!

Rudi darasani.
 
Dear Secret Service, there is nothing like "Oral Interview". Interview is always oral, so you cannot say oral interiview. Is the same as saying "repeate again". That is written test or screening test, sawa!!

Rudi darasani.

Shukrani mkuu Kiriba aisee. Ili ndio darasa huru bila fees. Thanks mzee.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom