Tuwe wakweli, tatizo la nchi hii ni Mawaziri au Rais wa nchi?

JK ni zaidi ya mzigo, maana mzigo unaweza kuutua hata kwa hasara.

JK ni janga.

Mara zote nikisikia "Rais ni mchapakazi, anaangushwa na washauri/ watendaji wake tu" nataka kutapika. Kama angekuwa mchapakazi asingeweza kuchagua washauri/ watendaji ovyo, na ingetokea hivyo kwa bahati mbaya -inatokea mara moja moja- angekuwa na mechanism ya kuwajua wazembe ni nani na kuwatoa mara moja. Mbona huyu kila mara tunasikia apologists wanamtetea kwa kuwatoa "bangusilo" washauri/ watendaji wake tu?

Halafu tusimuangalie sana JK na kumtupia lawama yeye kama vile yeye kajifikisha hapo mwenyewe.

JK ni kielelezo tu cha jamii nzima, kwamba mtu anaweza kuwa bw.ege mtozeni kama JK na bado akawa rais wa Tanzania.

Sasa hapo tatizo ni kubwa kuliko JK, ni kwa wote waliomchagua, ni katika mifumo yote aliyopitia mpaka kufika alipo, kuanzia shule alizosoma -mpaka UDSM- kwenda jeshini, kwenda bungeni, kwenye wizara nyeti alizoshika, mpaka Mkapa kumuweka Mambo ya Nje miaka 10 akimtayarisha kwamba siku moja akishika nchi asiwe zezeta.

Inaonekana kote kume fail.

Hata watu wa upinzani nao wana sehemu yao ya lawama kwa kutokuwa na upinzani tahbiti ambao ungewapa Watanzani chaguo la mbadala lenye matumaini. Maana sasa hivi kuna Watanzania wanaipigia kura CCM si kwa sababu wanaipenda sana, ila wakiangalia upinzani wanaona kila siku migogoro, not ready for the prime time - not that CCM is overly ready itself.

Kwa hiyo jamii nzima collectively ime fail, si suala la rais tu.

Rais anachukua lawama kubwa kwa sababu ana wajibu mkubwa na haki / ushawishi kufanya mengi.


Tatizo ni ninyi wanafiki wakubwa mlitarajia rais afanye nini akafanye na kazi za uwaziri hamna haya nyie ni mangapi JK ameifanyia hii kweli fadhila ya Punda mateke.

Mambo aliyofanya JK hayajapata kufanywa na Rais yeyote tangu tupate uhuru kama kuna mtu anapinga basi atakuwa anasumbuliwa na mambo mawili udini au ukabila.
 
Tatizo ni ninyi wanafiki wakubwa mlitarajia rais afanye nini akafanye na kazi za uwaziri hamna haya nyie ni mangapi JK ameifanyia hii kweli fadhila ya Punda mateke.

Mambo aliyofanya JK hayajapata kufanywa na Rais yeyote tangu tupate uhuru kama kuna mtu anapinga basi atakuwa anasumbuliwa na mambo mawili udini au ukabila.

Huyu hapa mjadala mzima hajauelewa.

Sijaona mtu anayesema JK afanye kazi za mawaziri.

Lolote zuri JK atakaloifanyia nchi hii, ni wajibu wake, na kaomba mwenyewe the highest office in the land. Na si kweli kwamba hatumtetei JK. Juzi watu wamemlaumu JK kwa teuzi za maafisa wa ngazi za juu wa polisi, kwamba kavunja katiba, mimi nilisema kwamba rais hajavunja katiba, katiba inamruhusu kuunda vyeo.

Kwa hiyo si kweli kwamba tunamlaumu tu. Wengine hatuangalii mtu, tunaangalia hoja. Sasa kama anaboronga nine times out of ten na tuna m blast nine times out of ten, na kumtetea that one time, si kosa letu.

Mambo gani hayo aliyoyafanya JK ambayo hayajapata kufanywa na rais mwingine? Na kwa nini utegemee mambo anayoyafanya rais wa 2014 yawe yamepatwa kufanywa na rais wa 1995, 1985 au 1965?

Let's say JK kafanya mengi mazuri for the sake of argument for a moment.

Kusema "mambo yaliyofanywa na JK hayajapata kufanywa na rais yeyote" ni kurudi kule kule kwenye kulinganisha marais tofautii, waliotawala katika mida tofauti, chini ya zeitgeists tofauti, upuuzi.

JK kasomeshwa bure na serikali ya Nyerere, kwa maana hiyo, hata akifanya mazuri leo, ni matunda ya serikali ya Nyerere, wanaomtetea Nyerere wakisema Nyerere alishindwa kufanya mazuri mengine unayoyaona kama JK anayafanya leo kwa sababu alikuwa anamsomesha JK ili kujenga msingi wa JK kufanya mazuri haya utasemaje?

JK angeishia darasa la tatu angeweza kusimama na kuongea na watu wa dunia nzima? Hapo ana degree ya uchumi tu sijawahi hata siku moja kumsikia anaongelea uchumi kama mchumi!

Acha masikhara wewe.
 
Tatizo ni ninyi wanafiki wakubwa mlitarajia rais afanye nini akafanye na kazi za uwaziri hamna haya nyie ni mangapi JK ameifanyia hii kweli fadhila ya Punda mateke.

Mambo aliyofanya JK hayajapata kufanywa na Rais yeyote tangu tupate uhuru kama kuna mtu anapinga basi atakuwa anasumbuliwa na mambo mawili udini au ukabila.
Na tangu uhuru hatujawahi kuwa na awamu yenye mambo ya ajabu ajabu kama hii.Mfano udini,watu kung'olewa kucha na meno,kusamehe wezi wa EPA,tukikamata mafisadi nchi itayumba,nawajua wauza unga,kusafirisha twiga na wanyama wengine nje ya nchi,watu kumwagiwa tindikali,mabomu katika mikutano ya kisiasa n.k.Yaani ni kichefuchefu kitupu!
 
Back
Top Bottom