Tuwe wakweli hali ya wakulima wa korosho ni mbaya sana kuliko awamu nyingine yoyote.

Nascoba

JF-Expert Member
Mar 16, 2012
310
160
Wadau hali ya wakulima wa korosho ni mbaya sana tofauti kabisa na inavyoripotiwa ktk vyombo vya Habari...
Katika Kijiji chenye watu mia sita wanalipwa watu nane au watu kumi na tatu kisha inatangazwa watu wengi wanalipwa huu uongo unaotangazwa mchana kweupe ni kwa maslahi ya nani.
Wakulima wengi ambao walitarajia kupokea malipo ya korosho ili waandae mashamba ya mpunga Au Mahindi wamebaki tu hawana la kufanya.
mfumo huu sio tuu utaathiri uzalishaji wa korosho msimu ujao bali utaathiri hadi mazao mengine ikiwemo Mpunga na Mahindi.
Imefika pahala mtu anachukua risiti zake za korosho anaenda kuziweka bondi kwa mtu kwa makubaliano kwamba akilipwa watagawana nusu kwa nusu.
Watu wamekwama sana.
Kipindi hiki cha mvua ndo watu hupalilia mikorosho hununua mbolea na salfa kwa ajili ya kuandaa uzalishaji.
Kiukweli serikali inaangamiza kilimo na uchumi wa wananchi wake yenyewe ingawa kwa nje inajinadi kutaka kuwasaidia.
Msaada pekee wa kumpa mkulima wa korosho ni kupeleka pesa ktk maghala mapema kwa ajili ya ununuzi kuliko kumkopa mkulima Tangu mwezi wa tisa na hadi inafika mwezi January hajapata senti yake huo ni unyonyaji usio na mfano.
Tunaiomba serikali iwalipe wakulima pesa zao baada ya kuwa imeshachukua korosho zote iache kutengeneza figisu na kutaka kuwadhulumu wakulima kwa kisingizio cha uhakiki wa mashamba hiyo ni dhulma ya serikali dhidi ya wananchi wake yenyewe.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hapo ndipo unapoonekana umuhimu wa upinzani
Moja Ya kazi Ya kambi upinzani ni kuikosoa na kuishauri serikali ambapo kwa mwendo huo serikali hufaidika Sana na ushauri unaotoka kwa wapinzani japo serikali wanaweza wasikiri hadharani Lkn nyuma Ya pazia wanaufanyia kazi ushauri au mawazo Ya upinzani
Lililopo sasa serikali inaamua tu kuchukua maamuzi yake moja kwa moja mwisho wa siku yanatokea kama haya sasa
Cha kufurahisha upande wa wapinzani kuna wabunge wengi vichwa Kweli kweli hili halina ubishi mfano swala la kikokotoo na hoja alioipigania mb Esta bulaya wote tumeona matokeo yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nunua gazeti la Leo la Nipashe
Jana wananchi Masasi wamejazana ofisi ya mkuu wa wilaya kwa masaa Saba kuishinikiza serikali iwalipe pesa zao za korosho

Sent using Jamii Forums mobile app

Wakulima wanachanganyikiwa kwa sasa kesho kutwa shule zinafunguliwa wakishindwa kupeleka watoto shule watapelekwa mahakamani.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Yatakuja mapimbi hapa yatasema unatumwa na mabeberu.........hii nchi bwana dah......jitu limekaa kwenye kiyoyozi huko linakesha kuongea mashudu tu wakati wakulima wanapata tabu huku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
FB_IMG_1544433264731.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umetumwa wewe, hali ni nzuri na asilimia kubwa wameshalipwa...Eeh Mungu wasaidie
 
Hii ni habari ya uchochezi hakuna hata mtu mmoja anaeidai serkal kwenye korosho haoambao hawajalipwa ni watu wanaotumiwa na mabeberu

Sent using Jamii Forums mobile app
Katibu Mkuu wa CCM ameshasema tuongee ukweli,ukweli unasemwa wewe unageuza kwamba wanatumwa na mabeberu watu kama ninyi ndio adui wa taifa badala ya kuangalia kasoro zilizopo ili kumshauri vizuri Rais wewe unasingizia mabeberu na wakati wakulima wanateseka msaidieni Raisi na muwe wazalendo wa kweli acheni mambo ya ndio mzee Kwa kila jambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom