Kutofautiana kimawazo katika nchi ni jambo la afya. Haiwezekani sote tukawa na mtizamo mmoja. Hata watoto mapacha hutokea wakati wakatofautiana.
Kwa bahati mbaya kuna zama zimepita kwa kutofautiana tu pana watu wamekufa, wamepotezwa, wamejeruhiwa, wamedhulumiwa, na mengi ya namna hiyo.
Yaliyopita si ndwele bali kiungwana hayawezi kuachwa kuwa ndiyo ilikuwa malipo stahiki kwa wahanga wale.
Mungu bariki tumepata rubani mpya mwenye kuthamimi maridhiano kwa maneno na kwa vitendo. Rubani aliyedhamiria kutuleta pamoja. Makundi yote kwa ujumla yanamkubali na sasa taifa linakuja pamoja.
Hata hivyo kuna wanaoonekana kutopendezwa na hali hii yenye matumaini mapya. Wao wamedhamiria kwa hali na mali kutusambaratisha.
Hawalali. Kila uchao wanakuja na kila aina ya chokochoko, uzandiki, fitna, uongo, uzushi, na vya namna hiyo. Alimradi tu kututatiza sisi kama wananchi na pia kumtatiza mama.
Wanahangaika mno kuzitatiza agenda zake ikiwamo hata kujaribu kumfarakanisha tu kwa lolote na kwa yeyote.
Haieleweki hasa wanataka nini au hawataki nini. Haijulikani pia kuwa, hii ni kwa maslahi gani hasa.
Watu hawa wapo pia humu JF. Mada zao na mabandiko yao mbalimbali yakiwatambulisha hivyo.
Hii nchi ni ya watanzania wote, ambamo kuna wanachama wa vyama vyote wakiwamo pia wasiokuwa na vyama.
"Hivi wandugu, mkiwamo nyie akina Elitewge, kudadavuwa, Nigrastratat, joni, dugunde, Mulokozae na wenzenu wengine ambao kila uchao ni kutafuta fursa za kupalilia utengano tu, mna madhumuni au maslahi gani hasa?"
Hivi wandugu, "Kwa nini mmedhamiria yasiwepo maridhiano kabisa? Kwa nini ni nia yenu kuona watanzania hawa wakiwamo wa CCM na wa CHADEMA haitokei kabisa nafasi ya kukaribiana? Madhumuni yenu ni nini hasa?"
Hatuwezi sote kupigia chapuo kuwa na taifa lenye ustawi, haki na usawa kwa maslahi yetu, wanetu na hata kwa watoto wa watoto wetu?
Tuwakaribishe ndugu hawa kutusaidia kuwaelewa. Labda wakijieleza wenyewe tutawaelewa. Isije kuwa kila mtu labda ana mshangaa mwenziwe.
Kwa bahati mbaya kuna zama zimepita kwa kutofautiana tu pana watu wamekufa, wamepotezwa, wamejeruhiwa, wamedhulumiwa, na mengi ya namna hiyo.
Yaliyopita si ndwele bali kiungwana hayawezi kuachwa kuwa ndiyo ilikuwa malipo stahiki kwa wahanga wale.
Mungu bariki tumepata rubani mpya mwenye kuthamimi maridhiano kwa maneno na kwa vitendo. Rubani aliyedhamiria kutuleta pamoja. Makundi yote kwa ujumla yanamkubali na sasa taifa linakuja pamoja.
Hata hivyo kuna wanaoonekana kutopendezwa na hali hii yenye matumaini mapya. Wao wamedhamiria kwa hali na mali kutusambaratisha.
Hawalali. Kila uchao wanakuja na kila aina ya chokochoko, uzandiki, fitna, uongo, uzushi, na vya namna hiyo. Alimradi tu kututatiza sisi kama wananchi na pia kumtatiza mama.
Wanahangaika mno kuzitatiza agenda zake ikiwamo hata kujaribu kumfarakanisha tu kwa lolote na kwa yeyote.
Haieleweki hasa wanataka nini au hawataki nini. Haijulikani pia kuwa, hii ni kwa maslahi gani hasa.
Watu hawa wapo pia humu JF. Mada zao na mabandiko yao mbalimbali yakiwatambulisha hivyo.
Hii nchi ni ya watanzania wote, ambamo kuna wanachama wa vyama vyote wakiwamo pia wasiokuwa na vyama.
"Hivi wandugu, mkiwamo nyie akina Elitewge, kudadavuwa, Nigrastratat, joni, dugunde, Mulokozae na wenzenu wengine ambao kila uchao ni kutafuta fursa za kupalilia utengano tu, mna madhumuni au maslahi gani hasa?"
Hivi wandugu, "Kwa nini mmedhamiria yasiwepo maridhiano kabisa? Kwa nini ni nia yenu kuona watanzania hawa wakiwamo wa CCM na wa CHADEMA haitokei kabisa nafasi ya kukaribiana? Madhumuni yenu ni nini hasa?"
Hatuwezi sote kupigia chapuo kuwa na taifa lenye ustawi, haki na usawa kwa maslahi yetu, wanetu na hata kwa watoto wa watoto wetu?
Tuwakaribishe ndugu hawa kutusaidia kuwaelewa. Labda wakijieleza wenyewe tutawaelewa. Isije kuwa kila mtu labda ana mshangaa mwenziwe.