Tuwaombee msamaha Kafulila na wajumbe wengine wajiunge CHADEMA

Tuwaombee msamaha Kafulila na wajumbe wengine wajiunge CHADEMA

Duble Chris

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2011
Posts
3,481
Reaction score
564
Wanajamvi JF
Tumuombee msaha kafulila ili arudi CHADEMA kuendeleza harakati za kuijenga TZ kwa sababu

  • Alikuwa mwanachama wa CDM
  • Aliungana na wabunge wa CDM bungeni kususia hoja ya katiba
  • Anaonyesha kweli yeye ni mpinzani wa CCM si kibaraka
  • CDM ni chama tawala cha upinzani nchini Tz kama CCM wanavyofanya wapokea walio hama na kurejea upya
  • etc
Wajumbe wengine pia wahamie CDM kwani wamekuwa ni wachapa wazuri ndani ya chama chao wakijiunga na CDM wataku mtaji wa faida kubwa

Nawasilisha
 
nasapoti ila kwa tabia ya huyu jamaa itabd wamwekee masharti mazito.
 
Yaleyale ya Shibuda yatajirudia kwa Kafulila. Siungi hoja. Anapaswa kujutia ujinga alioufanya,
 
Yeye mwenywe KAFULILA aje aombe msamaha na siyo sisi tumuombee kwa niaba yake maana baadae anaweza akatugeuka akasema sisi ndio tulimfuata na kumuombea msamaha! Hao wajumbe wengine ni ruksa kujiunga nasi kwani hawana historia ya kuwa ndani ya Chama chetu na baadae wakaanza kutuponda.
 
ana mtaji yule. aje tu hamna noumer lakini asigombee ubunge tena kwa tiketi ya CHADEMA. Jimboni kwake atasimama aliyesimama katka uchaguzi wa 2010 kwa tiketi ya chadema. yeye inabidi amsaidie kupiga kampeni. chadema wasirudie kufanya kosa kama la segerea la kumuacha yule mama waliokwisha kumuandaa wakampa nafasi mtu ambaye hajaandaliwa na hajui katiba ya chadema ikoje. ova
 
hakuna asiyesamehewa! kama atakiri na kuamua basi arudi tu na nadhani chadema kunamfaa kuliko huko alikokuwa
 
Kwani aombe msamaha alifanyaje? Mbowe ndio anatakiwa kumuomba msamaha Kafulila kwa kumuita sisimizi
 
Tatizo la huyu kijana anapenda madaraka mno......anaweza kutuharibia sana,la sivyo inatakiwa apewe onyo ili aendane na mienendo ya CDM
 
Kwani aombe msamaha alifanyaje? Mbowe ndio anatakiwa kumuomba msamaha Kafulila kwa kumuita sisimizi


Huwezi kujua wewe maana wewe ni ccm! Akili zimeshaharibika umebaki na masaburi tu!
 
Yani yeye isimuume aliyefanya kosa aombe msamaha tujekufanya sisi yasiyotuhusu
 
Kwani aombe msamaha alifanyaje? Mbowe ndio anatakiwa kumuomba msamaha Kafulila kwa kumuita sisimizi
na wewe unakurupuka tu aliyesema kafulila ni sisimizi ni dr slaa...unakurupuka tu utadhani unaoga nje
 
Yani yeye isimuume aliyefanya kosa aombe msamaha tujekufanya sisi yasiyotuhusu. Crap
 
siasa za africa bana!wanafanya mambo bila kuzingatia matokeo
 
Tatizo kijana anatukana mamba kabla hajavuka mto. nakumbuka wakati bunge la kumi linaanza, aliwaponda sana wabunge wa CDM waliposusa hotuba ya rais, akasema yeye anajua dawa ya CDM na wamuachie apambane nao, leo yapo wapi? Kufukuzwa vyama viwili ndani ya muda mfupi si jambo dogo, imeharibu sana CV yake ya kisiasa.

Lakini bado ni kijana, akae chini atafakari, ama aache siasa, au ajifunze kuwa na uvumilivu na uungwana katika siasa.
 
na wewe unakurupuka tu aliyesema kafulila ni sisimizi ni dr slaa...unakurupuka tu utadhani unaoga nje

Nashukuru kwa kunisahihisha basi Slaa amuombe msamaha Kafulila
 
Wanajamvi JF
Tumuombee msaha kafulila ili arudi CHADEMA kuendeleza harakati za kuijenga TZ kwa sababu

  • Alikuwa mwanachama wa CDM
  • Aliungana na wabunge wa CDM bungeni kususia hoja ya katiba
  • Anaonyesha kweli yeye ni mpinzani wa CCM si kibaraka
  • CDM ni chama tawala cha upinzani nchini Tz kama CCM wanavyofanya wapokea walio hama na kurejea upya
  • etc
Wajumbe wengine pia wahamie CDM kwani wamekuwa ni wachapa wazuri ndani ya chama chao wakijiunga na CDM wataku mtaji wa faida kubwa

Nawasilisha
Mkuu DC, yote uliyonena ni mema, lakini kumbuka pia kuwa sikio la kufa haliskii dawa
 
Back
Top Bottom