Tuwaombee msamaha Kafulila na wajumbe wengine wajiunge CHADEMA

Tuwaombee msamaha Kafulila na wajumbe wengine wajiunge CHADEMA

Kwani aombe msamaha alifanyaje? Mbowe ndio anatakiwa kumuomba msamaha Kafulila kwa kumuita sisimizi

Wewe mbona hujamuomba msamaha Lowassa kwa kuzunguka nchi nzima tena kwa kutumia pesa za chama kwa kumnadi ni Fisadi!

 
Yeye mwenywe KAFULILA aje aombe msamaha na siyo sisi tumuombee kwa niaba yake maana baadae anaweza akatugeuka akasema sisi ndio tulimfuata na kumuombea msamaha! Hao wajumbe wengine ni ruksa kujiunga nasi kwani hawana historia ya kuwa ndani ya Chama chetu na baadae wakaanza kutuponda.
Hapo umeongea lazima ajutie mwenyewe aliyofanya ndio arudi la sivyo atajiona bab kubwa na kwamba CDM walikuwa wanamtegemea yeye!!
 
Wanajamvi JF
Tumuombee msaha kafulila ili arudi CHADEMA kuendeleza harakati za kuijenga TZ kwa sababu

  • Alikuwa mwanachama wa CDM
  • Aliungana na wabunge wa CDM bungeni kususia hoja ya katiba
  • Anaonyesha kweli yeye ni mpinzani wa CCM si kibaraka
  • CDM ni chama tawala cha upinzani nchini Tz kama CCM wanavyofanya wapokea walio hama na kurejea upya
  • etc
Wajumbe wengine pia wahamie CDM kwani wamekuwa ni wachapa wazuri ndani ya chama chao wakijiunga na CDM wataku mtaji wa faida kubwa

Nawasilisha
Namsikitikia kafulila, amepoteza ubunge mapema mno na yote ni sababu ya kukosa hekima, swala la kupewa msamaha na Chadema, kafulila hakufukuzwa Chadema, mwenyewe aliondoka tena kwa mbwe mbwe nyingi tu! akakimbilia NCCR - Mageuzi, kafika kule akaendeleza mbwe mbwe, akafikia hatua ya kubishana na uongozi alioukuta, akataka ligi akijua watanifanya nini mimi nimekipa chama heshima mimi ni mbunge,

Ni mambo ya kitoto, na yatazidi kumgharimu katika harakati zake za siasa, arudi Chadema ila Chadema wapo smart zaidi ya hao NCCR - Mageuzi, huko wakimsimamisha akashinda ubunge, akileta dharau watamvua uanachama na ubunge ataukosa sasa kama hatafikiria hilo aende TADEA, NRA, UPDP, CHAUSTA nk hivi vyama havina uwakilishi Bungeni kama wanampenda jimboni kwake aende huko akishinda tu! ataheshimiwa sana na viongozi wa vyama hivi hatafukuzwa ila CHADEMA hakumfai.
 
Kwani aombe msamaha alifanyaje? Mbowe ndio anatakiwa kumuomba msamaha Kafulila kwa kumuita sisimizi
we chuku niaje? Mbona unadandia vitu ambavyo havikuhusu,unatafuta mtu wa kukameruni au? Peleka masaburi huko kwa magamba...
 
Yaleyale ya Shibuda yatajirudia kwa Kafulila. Siungi hoja. Anapaswa kujutia ujinga alioufanya,

Tangu lini wewe ukaitakia mema CDM!!
Chochote usichokiunga mkono about CDM means kina maslahi kwa CDM!!
Naunga mkono hoja, arudi CDM but kwa masharti makali!!
Kama aliweza kumuomba msamaha Mbatia akijua ni Kibaraka wa CCM basi hatashindwa kuiomba msamaha CDM akijua ni wapinzani wa kweli!!
Nafikiri kupitia Mh. Zitto, hili suala linajadilika
 
CDM msameheni.....mkichelewa mkilijadili hili atarudi kwa kina ritz..Zitto msaidie. Kafulila is daring, young and potential!
 
Wawasikilize akina Petro na Yohana, mambo yataenda vizuri
 
Namsikitikia kafulila, amepoteza ubunge mapema mno na yote ni sababu ya kukosa hekima, swala la kupewa msamaha na Chadema, kafulila hakufukuzwa Chadema, mwenyewe aliondoka tena kwa mbwe mbwe nyingi tu! akakimbilia NCCR - Mageuzi, kafika kule akaendeleza mbwe mbwe, akafikia hatua ya kubishana na uongozi alioukuta, akataka ligi akijua watanifanya nini mimi nimekipa chama heshima mimi ni mbunge,

Ni mambo ya kitoto, na yatazidi kumgharimu katika harakati zake za siasa, arudi Chadema ila Chadema wapo smart zaidi ya hao NCCR - Mageuzi, huko wakimsimamisha akashinda ubunge, akileta dharau watamvua uanachama na ubunge ataukosa sasa kama hatafikiria hilo aende TADEA, NRA, UPDP, CHAUSTA nk hivi vyama havina uwakilishi Bungeni kama wanampenda jimboni kwake aende huko akishinda tu! ataheshimiwa sana na viongozi wa vyama hivi hatafukuzwa ila CHADEMA hakumfai.

CHADEMA ni chama makini, ni mzazi mwenye hekima, ni mvumilivu lakini mwenye ujasiri. Ukiona kiongozi ameshindikana ndani ya CHADEMA, kamwe hawezi kudumu katika chama kingine chochote cha upinzani, labda huko CCM ambacho ni kokoro la kila takataka.

Kafulila anatakiwa kurudi nyuma, kujutia yale aliyoyafanya akiwa CHADEMA. Kwa mbwembwe zile zile alizoondoka nazo kuelekea NCCR, arudi CHADEMA, na kuwatangazia watanzania wote kuwa alipotoka sana kwa yale aliyoyasema wakati akihama chama. Akiri pia kuwa yale aliyokuwa akiyasema hayakuwa na ukweli ndani yake. Atamke wazi kuwa atakuwa mwanachama mwaminifu wakati wote, mwenye kuangalia maslahi ya Taifa na chama, na kuyaweka nyuma maslahi yake binafsi. Aseme kuwa yuko tayari kuendelea kuwa mwanachama wa kawaida hata kama chama hakitampendekeza yeye kuwa mgombea wake katika jimbo alilokuwa akishikilia. Kama hayawezi haya, CHADEMA isimpokee - matatizo ya Shibuda yanatosha, hakuna haja ya kuongeza mengine.
 
CDM msithubutu kumpokea Kafulila. Atawafanya mje kujuta kama mnavyojuta sasa kwa kumpokea Shibuda.
 
Pole zake huyu jamaa namuona kama kichwa chake hakipo sawa sawa, anahitaji maombi na ushauri aende ccm hapo patamfaa.
 
kijana rudi nymbani cdm, kasi yako ya kuwaumbua magamba haikuwapendeza co-magambas. Najua ulikuwa unasema sana khs cdm na hii ni kutokana na mapenzi makubwa uliyonayo kwa cdm lkn ulishindwa kujitambua na hata siku za mwisho ulikuwa ukiicheza ngoma ya cdm sasa rudi ujifunge kibwebwe uicheze vizuri.
 
Nashukuru kwa kunisahihisha basi Slaa amuombe msamaha Kafulila

nawe una akili ya chekechea wakibadili kuwa aliitwa ivo na Lissu utabadili. si bora utulie uandike ukiwa na akili timamu?
 
kafulila ametambua kuwa yeye si zaidi ya chama,anapaswa awe na political tolerance wala si kufanya atakavo,aidha aendelee ivo ivo ili kuonesha kuwa cdm kumtupa walikuwa sahihi,na cdm wakimsamehe basi akae benchi kwanza ili ajifunze siasa.
 
Unajifunza kutokana na makosa cdm watoe nafasi ya msamaha
 
nasapoti ila kwa tabia ya huyu jamaa itabd wamwekee masharti mazito.

Hewala, na ajue CDM siyo ccm, hatupendi wenye chokochoko, wasaliti, wanafki wala wanaotaka kuwa maarufu kuliko Chama. Simwamini huyu mtu pamoja na Zitto
 
CHADEMA ni chama makini, ni mzazi mwenye hekima, ni mvumilivu lakini mwenye ujasiri. Ukiona kiongozi ameshindikana ndani ya CHADEMA, kamwe hawezi kudumu katika chama kingine chochote cha upinzani, labda huko CCM ambacho ni kokoro la kila takataka.

Kafulila anatakiwa kurudi nyuma, kujutia yale aliyoyafanya akiwa CHADEMA. Kwa mbwembwe zile zile alizoondoka nazo kuelekea NCCR, arudi CHADEMA, na kuwatangazia watanzania wote kuwa alipotoka sana kwa yale aliyoyasema wakati akihama chama. Akiri pia kuwa yale aliyokuwa akiyasema hayakuwa na ukweli ndani yake. Atamke wazi kuwa atakuwa mwanachama mwaminifu wakati wote, mwenye kuangalia maslahi ya Taifa na chama, na kuyaweka nyuma maslahi yake binafsi. Aseme kuwa yuko tayari kuendelea kuwa mwanachama wa kawaida hata kama chama hakitampendekeza yeye kuwa mgombea wake katika jimbo alilokuwa akishikilia. Kama hayawezi haya, CHADEMA isimpokee - matatizo ya Shibuda yanatosha, hakuna haja ya kuongeza mengine.

Sina la kuongeza.
 
Back
Top Bottom