ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,529
- 21,530
My people,
Kwa kila mwanaharakati ambaye anaikosoa Serikali hakika anajua matokeo au madhara ambayo atakutana nayo leo au keshoNdio maana comrade Pole pole alijua na alikuwa tayar kulipia gharama hiyo ,kuonyesha kwamba alikuwa tayari kwa lolote litakalo mkuta akaamua kubakia hapa hapa hali akijua usalama wake hauko asilimia Mia moja,na kweli kilichotokea wote tunakijua
Nini nataka kusema hapa, mwanaharakati yoyote yule awe ndani ya nchi au nje ya nchi basi vita yake na Serikali isimfanye mwananchi wa kawaida akashindwa kuendesha maisha yake ya kila siku,akashindwa kujifanyia shughuli zake za kiuchumi ambazo zinamfanya apate mkate wake wa kila siku na familia yake
Wanaharakati wengi tena hawa waliopata hifadhi nchi jirani au kwengine kokote kule,wao wanafadhiliwa na maisha yao yanaendelea kama kawaida,lakini wanataka sisi tuache shughuli zetu za kutuingizia kipato na kucheza nyimbo zao kuikomboa nchi kwa njia ambayo sio salama na kuyaweka maisha yetu rehani.
Wanatanzania hakuna shujaa kwenye kuhatarisha maisha yako,kudhibitisha hili ndio maana wao wapo huko nyuma ya keyboard kazi yao ni kutuhamasisha kuhatarisha amani ya nchi yetu pendwa Tanzania
Wao wanathamini uhai wao ndio maana wamekimbia nchi hii kulinda uhai wao,lakini wanataka sisi kuweka uhai wetu mashakani,hapana inatosha sasa,tuseme hapana kwa hawa Wanaharakati,kama kweli wana mapenzi na sisi waje hapa Tanzania na wawe front line tuandamane pamoja,tupigwe virungu pamoja,tupigwe risasi pamoja na tuwekwe selo pamoja
Gen Z you have got a lot of life a head of you,una ndoto nyingi za kutimiza lakini usikubali kuwaste your life In the name of kuikomboa Tanganyika, hatuna nchi inaitwa Tanganyika bali tuna nchi inaitwa Tanzania,kwahiyo usipiganie kitu ambacho hakipo now, bali pigania Amani ya Tanzania ambayo ndio urithi wetu
Amani ndio tunu au zawadi muhimu ambayo kila mtanzania anatakiwa kuilinda kwa wivu mkubwa sana,yoyote ambaye kwa namna moja au nyingine anataka kuhatarisha Amani yetu huyo ni adui yetu mkubwa ama awe kiongozi wa Serikali,Dini au kikundi chochote cha watu,tuseme hapana kwa watu hawa,hawana nia nzuri na Taifa letu
Ungana na Team Amani kupambana bila kuchoka na waovu na wahuni wote ambao hawana nia njema na TANZANIA YETU
Tutaelewana tu mdogo mdogo
Ni hayo tu!!