Tuwafokee wahenga wetu na kauli/misemo potofu na kengefu

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Mar 1, 2016
12,695
31,487
Ashakuum si matusi, maskini akipata matako ulia mbwata, hizi ni moja ya kauli za wahenga wetu. Hakika nyingi ya kauli hizi zina mafunzo makuu lakini zipo kauli potofu na kengefu.

Aliye juu mngoje chini, hakika hii ni kauli kengefu, inayochochea uvivu, kwanini usichukue ngazi umfuate?

Aidha, mgaa gaa na upwa hali wali mkavu, hii hakika ni kauli potofu, inachochea uzururaji na kuzalisha ma-beach boys wanao zurura kwenye pwani zetu

Pamoja na hizo hapo juu, ipo hii matata sana, mficha uchi hazai, hii inachochea ukahaba, yaani mwanamke au mwanaume anashauriwa auanike uchi wake hadharani, seriously?

Nyingine ni ndondondo si chururu, hapa wahenga wanatuzingua, vitu visivyo fanana siku zote haviwezi kuwa sawa, ni kichagizo tu

Nyingine mbaya kabisa, inayotumiwa na wenzetu makolo, eti wamekufa kiume, kweli? kufa ni kufa tu, hakuna kufa ki-kike au ki-ume

Bila ya kupoteza muda, endelea kuchakata kauli/misemo kengefu na potofu ili tuwafokee wahenga wetu
 
Aidha, mgaa gaa na upwa hali wali mkavu, hii hakika ni kauli potofu, inachochea uzururaji na kuzalisha ma-beach boys wanao zurura kwenye pwani zetu
Hii umeielewa vibaya. Maana ya kugaa gaa na upwa ni kutoka kwenda kutafuta.
Na atafutae hupata ndio maana wakasema mgaa gaa na upwa hali wali mkavu maana huenda akapata samaki(mboga) katika mihangaiko yake
 
Pamoja na hizo hapo juu, ipo hii matata sana, mficha uchi hazai, hii inachochea ukahaba, yaani mwanamke au mwanaume anashauriwe auanike uchi wake hadharani, seriously?
Naona unalazimisha kukosoa maneno ya wahenga wakati we mwenyewe hujayaelewa.
Hapo mwanamke/mwanaume hajashauriwa kuweka uchi hadharani lakini ukificha uchi wako kama ma-sister basi hutozaa.
Ila akiuona mumeo/mkeo basi utazaa
 
Naona unalazimisha kukosoa maneno ya wahenga wakati we mwenyewe hujayaelewa.
Hapo mwanamke/mwanaume hajashauriwa kuweka uchi hadharani lakini ukificha uchi wako kama ma-sister basi hutozaa.
Ila akiuona mumeo/mkeo basi utazaa
vipi wale wanao fichua nyuchi zao na hawazai?
 
Hii umeielewa vibaya. Maana ya kugaa gaa na upwa ni kutoka kwenda kutafuta.
Na atafutae hupata ndio maana wakasema mgaa gaa na upwa hali wali mkavu maana huenda akapata samaki(mboga) katika mihangaiko yake
Hakuna maana yoyote, kugaa gaa ni kuzurura tu bila mpango
 
1) Mficha uchi hazai = Mmficha maradhi hapati tiba.

2) Alie juu mngoje chini = Leo hana shida siku akiwa na shida atakutafuta.

3) Amekufa kiume = Hajakubali kuwa msaliti mfano kama Magufuli vile.

4) Mgaa gaa na upwa hali wali mkavu =

Namba 4 namuachia mwalimu wa Kiswahili Mpwayungu Village aje amalizie 😂🤣🤣
 
Kaaaazi kwel kwel!

Tuseme hujaelewa maana ya hyo misemo au basi tu na ww uonekane kwenye server za jf kuna jambo umeweka
 
Ashakuum si matusi, maskini akipata matako ulia mbwata, hizi ni moja ya kauli za wahenga wetu. Hakika nyingi ya kauli hizi zina mafunzo makuu lakini zipo kauli potofu na kengefu.

Aliye juu mngoje chini, hakika hii ni kauli kengefu, inayochochea uvivu, kwanini usichukue ngazi umfuate?

Aidha, mgaa gaa na upwa hali wali mkavu, hii hakika ni kauli potofu, inachochea uzururaji na kuzalisha ma-beach boys wanao zurura kwenye pwani zetu

Pamoja na hizo hapo juu, ipo hii matata sana, mficha uchi hazai, hii inachochea ukahaba, yaani mwanamke au mwanaume anashauriwa auanike uchi wake hadharani, seriously?

Nyingine ni ndondondo si chururu, hapa wahenga wanatuzingua, vitu visivyo fanana siku zote haviwezi kuwa sawa, ni kichagizo tu

Nyingine mbaya kabisa, inayotumiwa na wenzetu makolo, eti wamekufa kiume, kweli? kufa ni kufa tu, hakuna kufa ki-kike au ki-ume

Bila ya kupoteza muda, endelea kuchakata kauli/misemo kengefu na potofu ili tuwafokee wahenga wetu
Mgaa gas na upwa hali wali mkavu maana yake sio potofu au kuzalisha bich boy kama unavyodai maana yake Haina tofauti na mtembea bure si sawa na mkaa bure.. Atafutae hakosi japo kidogo...

Mficha uchi hazai..,.maana yake ni sawa na kusema mficha maradhi kifo kitamuumbua ...Hawakumaanisha uchi uujuao wewe ila walitumia neno uchi kama siri..Waalisisitiza sana kutokuficha siri zinazoweza kuwa na manufaa kwa upande wako au kwa jamii..

Acha upotoshaji wa misemo ya wahenga ila kama hujui maana ni vyema ukauliza maana ili upewe maana na uweze kujua maana..
 
Back
Top Bottom