Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,978
- 5,025
Suala la afya liwe ni haki ya msingi kwa kila mtanzania. Serikali iwe responsible na aina ya huduma za afya wanazopewa wananchi wake. Hii ina maana kwamba huduma zitakazotolewa na kituo/hospitali yoyote ziwe under regulations zinazoruhusu wananchi kuwashitaki wenye hospitali/kituo cha afya kama huduma walizopewa haziendani na gharama au ni tofauti na alizohitaji mgonjwa. Nimepitia kwenye katiba hii sijaona sehemu hili lilipoongelewa. Hii itasaidia pia kupunguza uharamia wanaofanyiwa wagonjwa na madaktari wasiokuwa na ethics zilizowakaa,wakazielewa vizuri. Asanteni kwa wale mtakaosaidia kulisemea hili, maana maoni mengi nimeona yanaelekea kwenye siasa tu.