Tusishangae Virusi vya Corona kuingia nchini

Tusishangae Virusi vya Corona kuingia nchini

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
15,202
Reaction score
25,378
Nchi zilizo karibu na china zingine zimefunga mipaka na hakuna raia yeyote kuingia hata awe raia wa nchi husika labda akae kambini kwa wiki nzima na vipimo juu.

Nchini Nigeria upekuzi wa kiafya/kupima umekuwa mkubwa kutokana na nchi hiyo kuwa na wasafiri wengi kutoka china.

Hapa Tanzania sijapata taarifa zaidi ila nimeona vifaa vilivyopo pale JNIA na wanaingia wakipimwa ila nimepata shock kwa mtindo wa upimaji, ikiwa na maana kile kimashine (kwa jamaa mmoja anayepima) anapima alafu hafuatilii matokeo/majibu akaniita mwingine apime bila kuangalia au kusikia alarm.

Hali kama hiyo ni hatari na udhaifu kama huo ndiyo unaweza kupenyeza mwathirika atakayekuja kuleta madhara makubwa kwa taifa.

Tukumbuke nchi kama Korea ya kaskazini taifa lenye uwezo, wao wametoa hadhari ya kumuua yeyote atakayepenya na ugonjwa, marekani wao tayari wameshasema dawa wanayo, sisi tumejipanga vipi kama taifa pindi likitokea?

Baadhi wanajipa moyo eti joto litasaidia, hapana, joto ni Dar tu vipi Arusha, Iringa, Mbeya, Njombe nk kuna joto?
Serikali ijipe tafakuri kuangazia lolote linaloweza kutokea soon kuhusu corona.


NB.
Wazee wa fulsa kwa nia njema, anzeni kuagiza mask za kuuza maana kila janga linakuja na fulsa.

UPDATE:
Hii ni baada ya majuma kadhaa na hali imejidhihirisha tayari, kwa wenye macho wanaona, masikio wanasikia.
 
Nimeona sehem sina uhakika endapo ni habari za kweli, jamaa mwafrika amepona baada ya kuathiriwa na hao virus.

Kuna dhana imeanza kujengeka kwamba huo ugonjwa unaweza usiwe tishio sana kwa waafrika hasa wa ukanda wa kusini mwa Sahara.
 
Huyu ndiye corona mwenyewe.
1581797768598.png
 
Balozi wetu huko China mtanzania pekee mwenye kifua huu ndio wakati wa kulipiza kisasi harudi nao nchini amkabidhi Meko mama Samia ale shavu kwa mujibu wa katiba
 
Museven ameshagundua hiyo corona ni sanaa, yeye anakabiliana na nzige na ukimwi...
 
Back
Top Bottom