Ujumbe mzito sana huu. Hapa wanafiki kama kina Pasco na Manyerere Jackton hutawaona wakiweka mguuCCM ijielekeze kule ambapo tunaweza kupita bila kupingwa.Kule ambapo wananchi bado wanakitambua na kukipenda 'chama cha Nyerere' pasipo kufuatilia hasa kinachofanya na jinsi kinavyowahudumia. Kule ambapo CCM huchaguliwa kwa rangi yake;takrima yake;'mbinu zake' na 'mizengwe yake'. Lakini si Sombetini.
Twende kule ambapo idadi ya wapigakura yaweza kubadilishwa bila ya vikwazo vyovyote. Kule ambapo majina ya waliojiandikisha yaweza kuwa yoyote yale na hatuhojiwi.Twende kule ambapo mgombea wetu aweza kutangazwa mshindi 'kwa dharura na chini ya ulinzi mkali'.Kwakuwa watu wanakipenda chama chetu.Kwakuwa watu wanapenda CCM na viongozi wake.Kwakuwa daftari la kupigia kura laweza kutupa ushindi.Kwakuwa wananchi wanaweza 'kuzuiwa' kwenda kupiga kura zao. Lakini si Sombetini.
Sombetini tusiende. Hakuna haja. Twendeni kwingineko katika Kata 28. Hima chama changu,tusonge mbele!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Last edited by a moderator: