Tusiende Sombetini

Tusiende Sombetini

ccm wana KAZI Kubwa sombetii, labda wapeleke baraza lote la mawaziri na rais akiwemo...

Hata wamsimamushe Kikwete kugombea udiwani kwa ticket ya Ccm, na Cdm wamsimamishe mamantilie, Kikwete atapigwa bao.
 
Unamaanisha hicho chama chako mnatumia mizengwe kushinda kwenye chaguzi mbalimbali au unamaanisha nini unaposema CCM waende mahali ambapo wananchi wanaweza kuzuiwa kwenda kwenye uchaguz au mahali ambapo mshind anaweza kutangazwa kwa dharura embu mjipange bana bado mnaweza but mnamizengwe xana
 
Nimekupa like kwa upevu wa mawazo na uchanganuzi mzuri lakini nahisi wewe ni "Deep cover CDM operative"??!! nimekushtukia Bro! you sound too good to be genuine!

We nawe Lol!
 
Hakuna chama kibaya ila ccm wa2 wake wamezidi,hawasaidii wananchi,kaz yao ufisadi tu
 
Wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Kata nne kule mkoani Arusha,nilisema kikaoni na hapa JF kwamba nisingekwenda Arusha. Na ni kweli.Sijaenda. Nilisema kuwa CCM yetu haikuwa na nafasi hata ya kushinda kata moja. Nilibezwa,nilidhihakiwa,nikadharauliwa na kukosolewa. Matokeo yalionekana.Tukapigwa 4-0.

Uchaguzi mdogo mwingine umeshatangazwa na Tume ya Uchaguzi iliyo chini ya Jaji Damian Lubuva. Imesema kuwa Februari kutakuwa na Uchaguzi wa Madiwani wa Kata 29. Kati ya hizo,1 ni ya Arusha:Sombetini. Kule alikotokea Mawazo.Kule alikoacha uongozi Mawazo na kuhamia CHADEMA.Kule ambapo Mawazo na CHADEMA wana nguvu. Kule ambapo,tayari CHADEMA imemsimamisha mtu maarufu pia: Ally Bananga; M-CCM wetu wa zamani.

Kuna Kata 29.Ni heri CCM yetu ijielekeze kata 28. Ijielekeze kule ambapo tunaweza kupita bila kupingwa.Kule ambapo wananchi bado wanakitambua na kukipenda 'chama cha Nyerere' pasipo kufuatilia hasa kinachofanya na jinsi kinavyowahudumia. Kule ambapo CCM huchaguliwa kwa rangi yake;takrima yake;'mbinu zake' na 'mizengwe yake'. Lakini si Sombetini.

Twende kule ambapo idadi ya wapigakura yaweza kubadilishwa bila ya vikwazo vyovyote. Kule ambapo majina ya waliojiandikisha yaweza kuwa yoyote yale na hatuhojiwi.Twende kule ambapo mgombea wetu aweza kutangazwa mshindi 'kwa dharura na chini ya ulinzi mkali'.Kwakuwa watu wanakipenda chama chetu.Kwakuwa watu wanapenda CCM na viongozi wake.Kwakuwa daftari la kupigia kura laweza kutupa ushindi.Kwakuwa wananchi wanaweza 'kuzuiwa' kwenda kupiga kura zao. Lakini si Sombetini.

Sombetini tusiende. Hakuna haja. Twendeni kwingineko katika Kata 28. Hima chama changu,tusonge mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


Mzee Tupatupa umesahau na Bunda, Njombe, Iringa na Songea
 
Hakika umewapa tahadhari ya ukweli.Wasopoufuata ushauri wako, shauri yao kwani aibu itakuwa juu yao.
Wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Kata nne kule mkoani Arusha,nilisema kikaoni na hapa JF kwamba nisingekwenda Arusha. Na ni kweli.Sijaenda. Nilisema kuwa CCM yetu haikuwa na nafasi hata ya kushinda kata moja. Nilibezwa,nilidhihakiwa,nikadharauliwa na kukosolewa. Matokeo yalionekana.Tukapigwa 4-0.

Uchaguzi mdogo mwingine umeshatangazwa na Tume ya Uchaguzi iliyo chini ya Jaji Damian Lubuva. Imesema kuwa Februari kutakuwa na Uchaguzi wa Madiwani wa Kata 29. Kati ya hizo,1 ni ya Arusha:Sombetini. Kule alikotokea Mawazo.Kule alikoacha uongozi Mawazo na kuhamia CHADEMA.Kule ambapo Mawazo na CHADEMA wana nguvu. Kule ambapo,tayari CHADEMA imemsimamisha mtu maarufu pia: Ally Bananga; M-CCM wetu wa zamani.

Kuna Kata 29.Ni heri CCM yetu ijielekeze kata 28. Ijielekeze kule ambapo tunaweza kupita bila kupingwa.Kule ambapo wananchi bado wanakitambua na kukipenda 'chama cha Nyerere' pasipo kufuatilia hasa kinachofanya na jinsi kinavyowahudumia. Kule ambapo CCM huchaguliwa kwa rangi yake;takrima yake;'mbinu zake' na 'mizengwe yake'. Lakini si Sombetini.

Twende kule ambapo idadi ya wapigakura yaweza kubadilishwa bila ya vikwazo vyovyote. Kule ambapo majina ya waliojiandikisha yaweza kuwa yoyote yale na hatuhojiwi.Twende kule ambapo mgombea wetu aweza kutangazwa mshindi 'kwa dharura na chini ya ulinzi mkali'.Kwakuwa watu wanakipenda chama chetu.Kwakuwa watu wanapenda CCM na viongozi wake.Kwakuwa daftari la kupigia kura laweza kutupa ushindi.Kwakuwa wananchi wanaweza 'kuzuiwa' kwenda kupiga kura zao. Lakini si Sombetini.

Sombetini tusiende. Hakuna haja. Twendeni kwingineko katika Kata 28. Hima chama changu,tusonge mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

 
Mi nawashangaa maana walishaanza kupitapita majumbani mwetu usiku kucha, na nasikia tumetengewa fedha 3Bi, nguo, pilau, sukari na miradi kadha inatekelezwa kwa mfumo wa zimamoto ili kututeka tuwapigie.
Tunapokea kila kitu kiroho-safi, lakini tunamjua tutayempa kura zetu.
 
Well said mkuu kule Arusha watapata aibu tu hakuna chao na hata huko kwengine wataambulia patupu nakupeni akiba ya maneno hata kama mtaiba lakini haitawasaidieni kwani wananchi wa sasa sio kama wale wa 2010.Maccm hayana chao kwa sasa ndio maana yanaogopa kurekebisha daftari la wapiga kura.Mie naona katiba ijayo itaamke wazi kwamba kila mwisho wa mwaka ni lazima daftari lihakikiwe i mean wale waliotimiza miaka 18 waingizwe mara moja au kama hiyo na hata kama watu watapata vitambulisho vya Utaifa na kuvitumia iwe hivyo hivyo kila mtu akifikia miaka 18 lazima apate kitambulisho na hicho hicho ndi atapigia kura na pia kupiga kura iwe lazima kwa kuwa pesa ya walipa kodi inatumika kuandaa uchaguzi so wasipojitokeza inakula hasara kwa pesa za walipa kodi na pia tuwe na desturi au serikali iwe kali kwa kumchukulia mtu yeyote aliyefikisha miaka 18 asipopiga kura hii itasaidia sana kupata viongozi bora kwa maendeleo ya nchi kwani nchi lazima ijengengwe na wananchi wenyewe
 
Tupatupa umesahau na ile kata moja kule Bunda mlikokosa mwakilishi je huko mtakwenda tu kwa vile ni kwa bosi wa sera na utawala haramu au??? Tanzania ya leo sio ya Ccm na mabavu tena.RIP Ccm

Nimeipenda sana post hii..................magAmba kazi wanayo!
 
Back
Top Bottom