Hapa kuna series of events mpaka tumefika hapa. Iko hivi,
1) Hapo mwanzo ilikua kila sekta imepangiwa mfuko wake. Baadae wakaja wakaona ni ukiritimba sababu watu kama NSSF kwa mfano hawakuhitaji kufanya ubunifu wowote sababu walijua wewe ukiwa private sector basi ni wao tu automatically.
2) Sheria zikabadilishwa ili mfanyakazi awe na uhuru, anachagua kulingana na mfuko anaoona yeye unamfaa. Hapa ndipo kukawa na ushindani wa kibiashara uliopelekea mifuko hii kuanza kuleta ubunifu ili kuvutia members. Yakaibuka mafao mbali mbali ambayo mwanzo hayakuwepo. Hapa ndipo swala la kufuata sekta likafa, ikawa mfuko wowote unaruhusiwa kumsajili mfanyakazi yoyote. Yaani hapa ndio mtu wa Private sector aliruhusiwa hata kujiunga PSPF.
3) Hii mifuko ilipokuja kuungwa mwanzo wakasema wale waliojiunga mifuko ya sekta ingine (#2)waendelee kubaki kule kule, iwe kama walijiunga bahati mbaya tu. Lakini wapya ndo itabidi wafuate mifuko ya sekta waliyoko. Ila tu mifuko yao ndo itakua imeunganishwa. Mfano kama ulikua PSPF, GEPF, LAPF, PPF hapa wote mtaingia PSSSF ambao ndo mfuko uliobeba hiyo mifuko mengine. Na hapa ndio maana June ulijikuta uko PSSSF.
4) Ila sasa umekuja waraka mpya kwamba wale walioingia mifuko isiyo yao (#2) wakati ule wa uhuru wa kuchagua wanatakiwa kurudi mifuko yao wanayotakiwa kua. Ule uhuru umeonekana kua yalikua ni makosa na lazima yasahihishwe. Ile bahati mbaya (#3) ikaonekana sio bahati mbaya tena. Ndio maana wewe sasa uko NSSF, sio PSSSF tena.