Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,367
- 3,778
Si kila askari alijiandaa kuwa na kitega uchumi akiwa kazini lahasha, lakini sasa kwanini anapostaafu asipewe nauli ya kumrudisha kwao kwa wakati ili aende apambane na mashamba?
Swala hili viongozi na Waziri wa mambo ya ndani alitolea ufafanuzi lakini hamna utekelezaji sijui ni kumbembeleza mtoto kwa pipi au la.
kwa sasa mtu anastaafu nauli yake haiji baada tu ya kustaafu, fuatilieni ni wangapi wapo makambini wanasubiri nauli na wameisha staafu na nauli hizo hazii, watu wamekaa miezi sisi tukiwemo, pensheni ndio usiseme, mfuko wa pensheni PSSSF wanasema Serikali.
Inachelewesha kulipa Michango ya wanachama wake ndio maana na wao wanachelewa kuwalipa pensheni zao, serikali hiyo hiyo ndio inayotoa maagizo watu walipwe mapema, sasa hawa watu wanatuonaje sisi mfano, sasa hapa tunashindwa kuelewa ni kampeni ili wapate kura za wastaafu au ni nini.
Wastaafu kama askari wamekuwa wakitaabika baada ya kustaafu, si nauli ya kurudi kwao si pensheni hamna kitu, huenda NSSF inayokusanya michango ya private sector wana unafuu sana labda, ila PSSSF imetuchosha mno mno.
Sidhani kama kuna huruma yoyote ile kwa wastaafu wa PSSSF.
Swala hili viongozi na Waziri wa mambo ya ndani alitolea ufafanuzi lakini hamna utekelezaji sijui ni kumbembeleza mtoto kwa pipi au la.
kwa sasa mtu anastaafu nauli yake haiji baada tu ya kustaafu, fuatilieni ni wangapi wapo makambini wanasubiri nauli na wameisha staafu na nauli hizo hazii, watu wamekaa miezi sisi tukiwemo, pensheni ndio usiseme, mfuko wa pensheni PSSSF wanasema Serikali.
Inachelewesha kulipa Michango ya wanachama wake ndio maana na wao wanachelewa kuwalipa pensheni zao, serikali hiyo hiyo ndio inayotoa maagizo watu walipwe mapema, sasa hawa watu wanatuonaje sisi mfano, sasa hapa tunashindwa kuelewa ni kampeni ili wapate kura za wastaafu au ni nini.
Wastaafu kama askari wamekuwa wakitaabika baada ya kustaafu, si nauli ya kurudi kwao si pensheni hamna kitu, huenda NSSF inayokusanya michango ya private sector wana unafuu sana labda, ila PSSSF imetuchosha mno mno.
Sidhani kama kuna huruma yoyote ile kwa wastaafu wa PSSSF.