Tupike wali samaki

Tupike wali samaki

Leejay49

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2023
Posts
19,295
Reaction score
60,915
Hi guys,.hope mko poa

Tunavyoendelea kumwomba Mungu kuelekea kesho D9 basi tusisahau kula..... Haya tuanze

Ukishaweka mchele wako kwenye rice cooker au vyovyote vile utakavyoupika,. Pembeni tutaanza kupika samaki,. Kwenye sufuria yako utaanza kuweka mafuta kidogo,. vitunguu hoho na carrot kama nlivyofanya Mimi hapo

DSC_0290.JPG


Ukishavikaanga vikiiva vizuri utaweka nyanya na chumvi kiasi then utaendelea kukaanga
DSC_0291.JPG

Nyanya zikishaiva utaweka tomato paste kiasi utaendelea kupika dakika chache then utamweka samaki wako ambae ulishamtengeneza vizuri
DSC_0293.JPG

Taratibu utamsambazia viungo,. Akishashikana na viungo vizuri utaongezea nazo yako ambayo ulishaichuja vizuri,.. utakoroga taratibu taratibu ili Nazi isijikate
DSC_0294.JPG

Utaacha Kwa mda kidogo na mchuzi wako utakua tayari kama hivi
DSC_0295.JPG

Hapo sasa unaweza ukaonja kama nilivyofanya Mimi hapo,. Na samaki wangu alikuwa sooooo tasty
DSC_0296.JPG


Unaweza ukaserve na chochote,. Wali ugali au ndizi ila Mimi nilisave na wali wangu ambao mpaka namaliza kupika samaki ulikua umekwisha iva
DSC_0298.JPG


You can try it,. Na uenjoy mwenywe au na familia yako😍
 
Na huyo muhuni ni wewe😆😆

Thanks 😍
Sasa huu msosi utupikie mwingi ili ubakie wa asubuhi tukipige kiporo na mchuzi wa samaki chini kuweka na ukoko tuchangange na ndondo (harage).

Hapo Nina uhakika hatutakuwa na muda wa kurudi home kustua tumbo hiyo kesho. Ni mwendo wa maandamano hadi waseme basi inatosha.
 
Sasa huu msosi utupikie mwingi ili ubakie wa asubuhi tukipige kiporo na mchuzi wa samaki chini kuweka na ukoko tuchangange na ndondo (harage).

Hapo Nina uhakika hatutakuwa na muda wa kurudi home kustua tumbo hiyo kesho. Ni mwendo wa maandamano hadi waseme basi inatosha.
Maagizo yameeleweka mwashimiwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom