Tupike maini na matembele

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
33,487
Reaction score
65,822
Hello

Leo nilikuwa na hamu ya izi mboga maini siyapendi sana ila leo nilikuwa na hamu nayo

Nikachukua maini nikayachemsha baada ya kuya katakata na kutoa lile gamba la maini baada ya hapo nikaanda nyanya karoti na hoho

Baada ya maini kuiva nikaweka mafuta baada ya kuiva nikaweka vitunguu na nikachanganya baada ya muda nikaweka maini nika kaanga pamoja na vitunguu kisha nikachukua nyanya iliyo sagwa vizuri nikaweka kisha nikafunika na kuweka pilipili baada ya hapo nika weka na karot pamoja na hoho ziive

Kama unavyoona

Baada ya hapo nikawa naosha matembele niliyo yachambua vzr kisha nikayaweka yachuje maji

Baada ya hapo nikaanza kupika sasa nikaweka mafuta pamoja na vitunguu

Kisha nikaweka nyanya na kufunika nyanya za matembele sipendi kubrendi nakataka kama ivyo
Tu

Baada ya nyanya kuiva nikaweka tembele sasa

Nikafunika kwa muda kisha nikachanganya na baada ya kuiva nikasonga ugali safi maana murumbee ilianza kuuma sana

Karibuni wotee
 
Diko limenyooka unajua
 
Huoi ng'o
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…