Tupeni uhuru wetu

Tupeni uhuru wetu

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,758
Reaction score
9,591
helooo waungwana wapendwa wangu

Natumaini hamjambo na mnaendelea vyema na shughuli, kazi, biashara, masomo na pia
mambo mbalimbali ya maisha kiujumla na wengine sasa mnajiandaa kwa mitoko ya jioni
muende wapi kumpumzika na uchovu wa kazi za wiki nzima. Wote nawpeni hai na kuwapenda pia.

Kwa kweli leo acha niseme ukweli uliopo ndani ya moyo wangu hususani hawa watu
wanaoitwa WANAUME wamekuwa kero kubwa kwetu wanawake, na wengine wamekuwa watu wa
ajabu sana wao kazi yao kubwa kusema vibaya wanawake, wengine wanafikia hatua ya kuwapiga wanawake utadhani ni kapeti au ngoma vile ambao haiumii kabisa ukipiga. Mtanishangaa marafiki
zangu wapenzi wa humu jf kwanini leo nimetokea kuongea hivi kwani wananikera sana na wengine wanadhubutu kuleta ndoa za mitala bila hata kuwaambia mke mkubwa bila hata woga kabisa,
wengine wanamaswali yasiyo na mkia wala mbuzi,

Ajabu ni kwamba wao wenyewe wanajiona kuwa wako perfect kwa kila kitu na wala hataki kuulizwa chochote kwani wako sawa, hivi kwaniini wanatunyima uhuru wetu hawa, kwanini wanakuwa wagumu kuelewa mambo hata kama unamuaga kuwa nakwenda kwa shangazi kumsalimia basi yeye atajifanya amesahau na kusema ulikuwa wapi mpaka saa hii unaingia home? mara maneno ya ajabu na ohoo
kwanini leo umesuka msuko huo wa ajabu, mara hooo nipe simu yako akiona majina ya upande mwingine ataanza kusema kuwa huyu ni nani au hii namba ya nani? ilimradi tu ni karaha na kutunyimana uhuru
kwani maneno yao ni bora mtu akupige makofi kuliko kukusema hovyo tu kila wakati maana
utaona karaha na utaona kuwa kama ndoa yenyewe ndo hii si bora niondoke. yaani wanauzi sana
tena sana.

Leo nimeona niseme wazi kwani wananiuzi sana tena sana ni bora kuwaambia ukweli ili kama wako wakujirekebisha wajirekebishe na kuwaambia wenzao kuwa wanawake hatupendi kufuatwafuatwa na kunyimwa uhuru kiasi hichi

TUPENI UHURU WETU NASI TUJITAMBE NA KUJIENDELEZA JAMANI

Hayo ndo maneno yangu ya weekend jamani mabest na marafiki zangu naomba msikasirike kwani ukweli nimewapa yabidi mfunguke na kuchukua uamuzi wa busara ni jinsi gani mwaweza kukaa na wake zenu
kwa upendo. Nasema tupeni uhuru wetu nasi ni wanadamu kama ninyi.

Nawatakia weekend njema na Mungu awabariki sana,. Nawapenda nyote marafiki zangu
ila message send

 
Dah nilidhani unadai uhuru wetu toka CCM kumbe toka kwa sisi marijali hahahah, as always being said there is no free lunch! jikomboeni kielimu na kiuchumi safari yenu itafika, otherwise mtaendelea kudai uhuru wenu mpaka sijui lini.
 
Mmmmmmmmmmmh! To write this shit here in JF of all places Girl you got Balls!!!!!!!!! And im right here watchin them Men as They physically CHEW you up bit by bit!

AND THE CYBER BULLYING MAY BEGIN!!!!!!!!!!!!!!!!!!

:coffee::coffee::coffee::coffee::coffee::coffee::coffee:
 
ukitumia hizo nyodo mmeo atakupiga mpaka uje humu tukushauri. Kila sehemu kuna utaratibu huwezi kutoka asubuhi ukarudi saa 6 usiku eti ulikuwa kwa shangazi. Kudai haki yako waweza kuidai hata kwanjia ya kiungwana tu,yapo mambo ambayo sisi wanaume tunakosea na yapo mambo ambayo nyinyi wanawake mnakosea,ila uhuru usio na sheria mimi kwangu hamna,labda useme uko jukwaani,bungeni na kwenye vikao vyenu ukirudi nyumbani fata utaratibu,serikali haita kuoa wala haikunisaidia kulipa mahari
 
Pole sana ladyfurahia, umedundwa na kuletewa mwenza nini? Kwa nini na nyie msiwe wajanja mkaingia huu upande ambao unakuwa peke yako tu? Au usiolewe kabisa.
 
ladyfurahia hata mie nakutakia weekend njema yenye kukupa uhuru ila usiwe uhuru uliopitiliza.

Muda mwingine inakubidi kujishusha ili kuepusha ugomvi usio na sababu kwani kila mmoja akitaka kumuonyesha mwenzake umaridadi wake ndani ya nyumba hakutakalika.

Ndo maana unaambiwa kukaa kimya ni jibu tosha kwa yule akutakae shari.
 
Uhuru mnao sana na mmepewa na mungu; baada ya yesu kufamsalabani hakuna mtumwa wala mfalme, wala mtwana wala ..... Ila sasa na nyie mmezidi na kudai usawa kwa kila kitu.
Kuna kitu kinachoitwa mgawanyo wa majukumu; mungu alivyotuumba sisi wana-adam ni tofauti na nyie mabinti / wanawake. Hivyo uhuru mlio nao naomba uwe na mipaka; daima mjue kuwa mwanaume ni kichwa cha familia. Sisi wanaume ndo tunawatia vichwa nyie wanawake.
Ujumbe wangu kwenu wanawake ndo huo kwa leo. Ebu nani niondoke nikajipumzishe sehemu tulivu kwani hapa rocky city hali ya hewa ni nzuri sana kukaa kona na waungwana na kuanza kubadilishana mawazo huku tukisubiria mnyama aletwe mezani tukamtafune. Karibu ndama hotel - igoma
 
::
Ukitaka kumjua mtu mpe uhuru.
Utajua una mke au jike.
Halafu hizi demokrasia hizi? Hizi? Yangu macho.
::
ladyfurahia yakikushinda na wewe oa tu!
Kwa nini usemwe? Kwa nini uguswe? Si una elimu? Si mzuri? Si una haki? Si una uhuru?
Ishi peke yako,makovu ya nini?
=
 
Last edited by a moderator:
ukitumia hizo nyodo mmeo atakupiga mpaka uje humu tukushauri. Kila sehemu kuna utaratibu huwezi kutoka asubuhi ukarudi saa 6 usiku eti ulikuwa kwa shangazi. Kudai haki yako waweza kuidai hata kwanjia ya kiungwana tu,yapo mambo ambayo sisi wanaume tunakosea na yapo mambo ambayo nyinyi wanawake mnakosea,ila uhuru usio na sheria mimi kwangu hamna,labda useme uko jukwaani,bungeni na kwenye vikao vyenu ukirudi nyumbani fata utaratibu,serikali haita kuoa wala haikunisaidia kulipa mahari
imekaa njema hiyo kiongozi;
 
Uhuru upo tena wa bure, ambao ni mateka ndio wanatakiwa wadai kwa sauti ya juu. Ila uhuru wa mtu na mtu ni maelewano yenu binafsi.
 
Kwa kweli leo acha niseme ukweli uliopo ndani ya moyo wangu hususani hawa watu
wanaoitwa WANAUME wamekuwa kero kubwa kwetu wanawake, na wengine wamekuwa watu wa
ajabu sana wao kazi yao kubwa kusema vibaya wanawake, wengine wanafikia hatua ya kuwapiga wanawake utadhani ni kapeti au ngoma vile ambao haiumii kabisa ukipiga. Mtanishangaa marafiki
zangu wapenzi wa humu jf kwanini leo nimetokea kuongea hivi kwani wananikera sana na wengine wanadhubutu kuleta ndoa za mitala bila hata kuwaambia mke mkubwa bila hata woga kabisa,
wengine wanamaswali yasiyo na mkia wala mbuzi,

Umeolewa ww?
 
Nyerere alishawahi sema kuwa ili uwe huru unahitaji kujitegemea kwa kila kitu... Sasa nyie kwa vile kuna kitu tunacho sisi, hamtakujakiwa huru
 
Aah wapi ikifika jioni wewe mwenyewe unatangulia bandani kama kuku
 
Back
Top Bottom