Tupeane Taarifa benki zinazosuasua ili tutoe fedha zetu kabla hazijatangazwa mfilisi

Baada ya kupata taarifa ya haya mabank kufilisiwa niliamua kufatilia.
Kiasi kinacho ongelewa kinatolewa na bima ya amana kupitia bodi ya bima ya amana.
Bima ya amana ni kiasi kilichowekwa kisheria kinacholipwa na mabenki yote nchini kuelekea bodi ya bima ya amana ili kuweza kuwafidia wateja banki inapotangazwa kufilisika...
Sasa sheria ya Bima ya amana inaeleza wazi kuwa kiasi kinacho lipwa na Bima ya amana kisizidi million na nusu.
Hivyo basi kama uliweka laki tano basi utalipwa laki tano yote na bima ya amana.
Kama uliweka million 20 utapewa million moja na nusu na kiasi kilicho baki utalipwa na bank husika baada ya kukusanywa kwa mali na madeni yote ya wateja wa bank na orodha ya madai kupitia utaratibu maalum hivyo hakuna pesa ya mtu inayopotea bank inapo filisika.....
Pia bima ya amana hii ni ya serikali hivyo ni bima tofauti na zingine ambazo bank inaweza kuwa nazo.
inachukua mda gani kulipwa pesa iliyobaki?
 
Pale ela yake haiwezi kupotea, ila aachane nayo, kuna benki watu wanapitishia mishahara tu, lakini ukiwa serious na huduma za kibenki ni lazima ujibananishe walipo watu wengimfano hai ni kama Crdb na Nmb kwa sasa hawa ndio wamba wa Tanzania, na Kimei akiondoka Nmb itakuwa ndio nambari one Tanzania.
Statement yo yote juu ya Benki ni ya kutafakari sana. Yule Mkenya aliyekuwa CEO wa Precision alipotangaza anaachia ngazi kilichofuata wote tunakijua na hii statement ya juzi kwamba Kimei anaachia ngazi kwa kweli pressure yangu iko juu sana !
 
Serikali inatakiwa iangalie sana hili vuguvugu la mabank uchumi wa nchi yoyote unaendeshwa na banks sasa naona hapa watu wanataka waaminishwe kuwa tz ni banks mbili tuu ndo Zina faa nyingine hazifai it's not right kabisa serikali isipo angalia vizuri tutapata shida kiuchumi hata hizo banks kubwa kubwa nazo zinaweza zikashindwa pia in one way or another assume depositors wote watake hela zao at per unafikiri na wao wanaweza kuwapa wote? Tuache upendeleo kila bank hapa nchini ina umuhimu wake so long as ina good performance ina assets nzuri haina NPL kubwa ina tija kwa taifa.
 
Kwa hiyo bora lipi watangaze kabisa ili watu wajihami na vinsenti vyao, au watangaze ghafla ili watu wapoteza pesa zao.
Katika hali ya kawaida, sote tungependa itangazwe kabisa ili watu wajihami. Lakini kwa jinsi mabenki yalivyo matangazo hayo hutolewa wakati mambo yamekwisha haribika. Kuna wakati benki zinafikia hatua ya kushindwa kuwalipa wateja wake na Mamlaka husika huchukua hatua za kuitangaza kuwa mufilisi.
 
15697284_772134139608656_3206137239561358624_n.jpg
Aisee nimekupenda ghafla. Nipe number Na unapopatikana. Msambwanda unao rangi unayo pia
 
Serikali inatakiwa iangalie sana hili vuguvugu la mabank uchumi wa nchi yoyote unaendeshwa na banks sasa naona hapa watu wanataka waaminishwe kuwa tz ni banks mbili tuu ndo Zina faa nyingine hazifai it's not right kabisa serikali isipo angalia vizuri tutapata shida kiuchumi hata hizo banks kubwa kubwa nazo zinaweza zikashindwa pia in one way or another assume depositors wote watake hela zao at per unafikiri na wao wanaweza kuwapa wote? Tuache upendeleo kila bank hapa nchini ina umuhimu wake so long as ina good performance ina assets nzuri haina NPL kubwa ina tija kwa taifa.
Watu sasa hivi wanaingia woga kwenye hizi benki ndogo, kwa hali kuna hatari hata zilizokuwa zikijiendesha vizuri zikaanza kupoteza wateja...

Watu wataanza kuchomoka mmoja mmoja.
 
Biggest bank by asset size
1. CRDB
2. NMB
3. Standard Chartered
4. NBC
5 Stanbic
6. Exim
 
Nyie hamjui mchezo unaochezwa...kufilisi benki ndogo ndogo ambazo ndo zina afueni ya moja kwa moja kwa wananchi ni mkakati wa serikali na mabenki makubwa ili ukaweke hela zako NMB au CRDB ili uwape hati wafilisi nyumba....so huja pa kukimbilia.

Kwasasa nimetoa hela zangu zote pale NMB samora, kama milioni 82 hivi cash kwa mpigo hadi Teller akaanza kurembua kumbe mm nahamishia kwangu..nimezitandaza chini ya godoro, nikiamka asubuhi nachomoa elfu 10 yangu ya kutwa naingia mtaani
...mwenye mil 82 hawezi kuwa na matumizi ya elfu 10 kwa siku,
..pimbi wewe!
 
Hii mada watu wasipokuwa makini itaweza kusababisha mtikisiko wa uchumi.
Watu wanaweza pata hofu na kukimbilia kutoa pesa zao kwenye mabenki na kufanya "hoarding" ambayo italeta tatizo kubwa sana kwenye mfumo wa kifedha
Hii thread ingefungwa tu kwa kweli, maana paka hapa ilipofikia inaweza kuleta mtikisiko na mdororo mkubwa sana wa kiuchumi, hofu ni kitu kibaya, mi mwenyewe roho inanidunda sana ninapoona mtu anaisema vibaya CRDB, maana anaweza akaleta panic unnecessarily
 
Statement yo yote juu ya Benki ni ya kutafakari sana. Yule Mkenya aliyekuwa CEO wa Precision alipotangaza anaachia ngazi kilichofuata wote tunakijua na hii statement ya juzi kwamba Kimei anaachia ngazi kwa kweli pressure yangu iko juu sana !
Yaani kitu kinachotokea pale Crdb Bank inawezekana ikawa kama Precision Company. Maana wateja wanaangalia Business Partners wao katika biashara. Sasa pale Kimei anaondoka na wateja wake ingawa Crdb Bank kufa itachukua muda lakini ndio ivyo
 
Serikali inatakiwa iangalie sana hili vuguvugu la mabank uchumi wa nchi yoyote unaendeshwa na banks sasa naona hapa watu wanataka waaminishwe kuwa tz ni banks mbili tuu ndo Zina faa nyingine hazifai it's not right kabisa serikali isipo angalia vizuri tutapata shida kiuchumi hata hizo banks kubwa kubwa nazo zinaweza zikashindwa pia in one way or another assume depositors wote watake hela zao at per unafikiri na wao wanaweza kuwapa wote? Tuache upendeleo kila bank hapa nchini ina umuhimu wake so long as ina good performance ina assets nzuri haina NPL kubwa ina tija kwa taifa.
Kwa kifupi Sector ya fedha ishapata tatizo na itapelekea Bank nyingi kufaa. Maana kuna watu wazima ambao ni wastaafu wanapatwa na pressure ya hali ya juu kuhusu fedha zao. Wafanyabiashara wengi wataamisha mitaji yao bank nyingine
 
Back
Top Bottom