Benki ya Amana inahujumiwa

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,200
10,948
Hii ni benki ya mwanzo nchini kuendesha huduma zake kwa misingi ya sharia za kiislamu. Pia ni muendelezo wa mfumo bora wa kibenki unaofanya kazi nchi nyingi duniani.

Benki hii ilipoanza kazi nchini kulikuwa na maneno kutoka kwa baadhi ya watu lakini hatimae ikaanza shughuli zake na kuonekana kukua kwa kasi. Hata hivyo katika siku za karibu kwa mtazamo wa kimteja nimeona kuna shida zisizotatulika.

Katika pita pita yangu nimekutana na jamaa mwenye taarifa za ndani ambaye amethibitisha kuna hujuma za ndani kwa ndani zinazoendeshwa na wafanyakazi ambao kama wametumwa wafanye kazi hiyo.Kwa upande mwengine kuna benki nyengine ambazo zinakiuka sheria za BOT na kuacha ushirikiano na benki hii tena bila kukemewa.

inajulikana benki yoyote ya kiislamu duniani haiwezi kufilisika kwa njia za kawaida.Hata hivyo panapokuwa na hujuma zinazoendelea ndani kwa ndani hilo si ajabu kutokea.

Kuna tetesi kuwa wale waliopigania uanzishwaji wake na kupelekea furaha kwa jamii ya kiislamu na faida kubwa kwa wananchi kwa jumla walipoona wimbi la ufisadi na mbinu zao kuzidiwa na watu hao waliamua kukaa pembeni kuliko kuangalia kinachotokea.

Moja ya matawi muhimu ya benki ya Amana ni pale Tandamti ambapo awali wafanyabiashara wakubwa wa kiislamu walijazana kuweka fedha zao. Mara kadhaa nimekwenda nikakutana na wenzangu na mie wanaokwenda kutoa sh.10,000 za kununulia fungu la muhogo na dagaa. Inasemekana wengi wamekerwa na uzembe unaondelea wanapohitaji huduma kwenye benki hiyo.

Ushauri kama wapo wakereketwa wa benki ya Amana waliobaki katika uongozi wa juu basi wafukuze wapuuzi wote wanaotaka kutukanisha benki hiyo hasa kwenye vitengo ya teknohama na kila inapowezekana waanze kuajiri waislamu wenyewe kwanza wenye taaluma ya vitengo husika mbali mbali vya benki hiyo.
Salamu hizi zimfikie raisi Samia ili apeleke watu wake wakafuatilie mhimili huu wa uchumi iii mwaka wowote atakaondoka asije akaondoka na benki imekufa. Atabezwa kama alivyofanyiwa Kikwete aliyeondoka madarakani akiwawaacha masheikh wamerundikwa kwa makosa yasiyo na mbele wala nyuma.
 
Inayoitwa hujuma ni ya watu wa ndani wala sio ya washindani wa nje, na unaweza kuta ni gross incompetency sio kwamba wanaamua tuhujumu.

Ingekuwa ni benki ya wazee wa waraka wa bandari usingesikia haya mambo ya sijui hujuma sijui wafanyakazi wanafanya makusudi. Hakuna marupurupu makubwa kwa wafanyakazi, wanajilinganisha na wenzao wa benki nyingine hivyo mwenye uwezo mkubwa hawezi kaa hapo mnabaki na wanyonge wasiokuwa motivated.

Benki ina shareholders wa aina gani na management gani, kama wamekaa kiimani sana badala ya kibiashara lazima tatizo liwepo kwenye uendeshaji, hiyo siyo charity.

Uongozi mbovu unaharibu sana benki hasa hapo Kenya bora hata sisi Tanzania ushindani sio mkubwa sana.

Alafu bila riba hakuna banking system, Saudi Arabia wana mapato ya mabilioni ya dola kutokana na mafuta kwa mwaka ila wana riba ambayo sababu ni haramu wanaiita 'tozo'.

Anayetozwa tozo na anayelipa riba wote wanatoa in monetary terms, ila tozo ni halali. Waitaliano walipoanzisha banking system baadae ikavamiwa na Wayahudi hawakuipa sura ya kutoa hela bure na ukarudishiwa, na mifumo iko hivyo hivyo ni vigumu kubadilisha. Hiyo ni biashara.
 
Inayoitwa hujuma ni ya watu wa ndani wala sio ya washindani wa nje, na unaweza kuta ni gloss incompetency sio kwamba wanaamua tuhujumu.

Ingekuwa ni benki ya wazee wa waraka wa bandari usingesikia haya mambo ya sijui hujuma sijui wafanyakazi wanafanya makusudi. Hakuna marupurupu makubwa kwa wafanyakazi, wanajilinganisha na wenzao wa benki nyingine hivyo mwenye uwezo mkubwa hawezi kaa hapo mnabaki na wanyonge wasiokuwa motivated.

Benki ina shareholders wa aina gani na management gani, kama wamekaa kiimani sana badala ya kibiashara lazima tatizo liwepo kwenye uendeshaji, hiyo siyo charity.

Uongozi mbovu unaharibu sana benki hasa hapo Kenya bora hata sisi Tanzania ushindani sio mkubwa sana.

Alafu bila riba hakuna banking system, Saudi Arabia wana mapato ya mabilioni ya dola kutokana na mafuta kwa mwaka ila wana riba ambayo sababu ni haramu wanaiita 'tozo'.

Anayetozwa tozo na anayelipa riba wote wanatoa in monetary terms, ila tozo ni halali. Waitaliano walipoanzisha banking system baadae ikavamiwa na Wayahudi hawakuipa sura ya kutoa hela bure na ukarudishiwa, na mifumo iko hivyo hivyo ni vigumu kubadilisha. Hiyo ni biashara.
Ninge kushauri to take your time ujifunze jinsi Islamic banking system inavo operate, pesa ya kuhudumia wafanya kazi inapatikana vizuri, haitowi huduma bure inacho tafoutisha na banki zingine ni mambo kama matatu au mawili hususani pale katika kukopa kerejesha na kushindwa kulipa, ukisoma islamised economics hizo oparation are very alaborated. Tatizo letu wabongo hatupendi kusoma vitabu.
 
Bado sijaelewa benki isiyotoza riba kabisa inawezaje kumudu gharama za uendeshaji. Kwa ufupi, kinachotokea ndicho hasa kinachotarajiwa kuwapo, vinginevyo ingekuwa ni mshangao
hiyo kutotoza riba ndio nguzo kubwa inayozishikilia benki za kiislamu zisianguke.Na jiulize kwa nini benki nyengine zimeamua kufuata mfumo huo.Tatizo linaloinyemelea Amana bank ni kama ilivyoelezwa hapo juu.Kuna mapandikizi wengi.
 
hiyo kutotoza riba ndio nguzo kubwa inayozishikilia benki za kiislamu zisianguke.Na jiulize kwa nini benki nyengine zimeamua kufuata mfumo huo.Tatizo linaloinyemelea Amana bank ni kama ilivyoelezwa hapo juu.Kuna mapandikizi wengi.

Zinataka ku capture mateka wa kidini dats all,ila acheni kulialia sana mmezidi,banking ni bishara ya faida sio kurubuni watu eti hakuna riba,riba ipo sana ila mnaibadili jina huo ndio unafiki mlio nao mkawadanganye hao hao mliowashika akili kupitia dini.
 
Bado sijaelewa benki isiyotoza riba kabisa inawezaje kumudu gharama za uendeshaji. Kwa ufupi, kinachotokea ndicho hasa kinachotarajiwa kuwapo, vinginevyo ingekuwa ni mshangao

Riba wameibadili jina tu,ila huwezi kopa let say 500k ukarudisha 500k,wanawadanganya wajinga wenzao ila riba ipo wameibadili jina eti wanaita kugwana faida
 
Alshababu means youths au vijana sijui unamanisha kwamba benki lazima ziendeshwe na wa zee tu vijana hawawezi au una meaning nyingine sijui?
Una sema ?
872477241.jpg
 
Hii ni benki ya mwanzo nchini kuendesha huduma zake kwa misingi ya sharia za kiislamu. Pia ni muendelezo wa mfumo bora wa kibenki unaofanya kazi nchi nyingi duniani.

Benki hii ilipoanza kazi nchini kulikuwa na maneno kutoka kwa baadhi ya watu lakini hatimae ikaanza shughuli zake na kuonekana kukua kwa kasi. Hata hivyo katika siku za karibu kwa mtazamo wa kimteja nimeona kuna shida zisizotatulika.

Katika pita pita yangu nimekutana na jamaa mwenye taarifa za ndani ambaye amethibitisha kuna hujuma za ndani kwa ndani zinazoendeshwa na wafanyakazi ambao kama wametumwa wafanye kazi hiyo.Kwa upande mwengine kuna benki nyengine ambazo zinakiuka sheria za BOT na kuacha ushirikiano na benki hii tena bila kukemewa.

inajulikana benki yoyote ya kiislamu duniani haiwezi kufilisika kwa njia za kawaida.Hata hivyo panapokuwa na hujuma zinazoendelea ndani kwa ndani hilo si ajabu kutokea.

Kuna tetesi kuwa wale waliopigania uanzishwaji wake na kupelekea furaha kwa jamii ya kiislamu na faida kubwa kwa wananchi kwa jumla walipoona wimbi la ufisadi na mbinu zao kuzidiwa na watu hao waliamua kukaa pembeni kuliko kuangalia kinachotokea.

Moja ya matawi muhimu ya benki ya Amana ni pale Mchikichini ambapo awali wafanyabiashara wakubwa wa kiislamu walijazana kuweka fedha zao. Mara kadhaa nimekwenda nikakutana na wenzangu na mie wanaokwenda kutoa sh.10000 za kununulia fungu la muhogo. Inasemekana wengi wamekerwa na uzembe unaondelea wanapohitaji huduma kwenye benki hiyo.

Ushauri kama wapo wakereketwa wa benki ya Amana waliobaki katika uongozi wa juu basi wafukuze wapuuzi wote wanaotaka kutukanisha benki hiyo hasa kwenye vitengo ya teknohama na kila inapowezekana waanze kuajiri waislamu wenyewe kwanza wenye taaluma ya vitengo husika mbali mbali vya benki hiyo.

Kwahiyo nyinyi kila kitu mnahujumiwa?
 
Mkuu mbona unachanganya vitu tuko Tz, hizo picha za Pakistani sijui wapi uko, kama ni umasikini wa kuva yeboyebo Tanzania sisi ni masikini mara mbili kuliko hao watu wengi hata hivyo viatu hawawezi kuvaa wanava matairi ya magari. Kwahiyo jikite kwenye mada ya banking don't expose your hatred and ignorance.
 
Hii ni benki ya mwanzo nchini kuendesha huduma zake kwa misingi ya sharia za kiislamu. Pia ni muendelezo wa mfumo bora wa kibenki unaofanya kazi nchi nyingi duniani.

Benki hii ilipoanza kazi nchini kulikuwa na maneno kutoka kwa baadhi ya watu lakini hatimae ikaanza shughuli zake na kuonekana kukua kwa kasi. Hata hivyo katika siku za karibu kwa mtazamo wa kimteja nimeona kuna shida zisizotatulika.

Katika pita pita yangu nimekutana na jamaa mwenye taarifa za ndani ambaye amethibitisha kuna hujuma za ndani kwa ndani zinazoendeshwa na wafanyakazi ambao kama wametumwa wafanye kazi hiyo.Kwa upande mwengine kuna benki nyengine ambazo zinakiuka sheria za BOT na kuacha ushirikiano na benki hii tena bila kukemewa.

inajulikana benki yoyote ya kiislamu duniani haiwezi kufilisika kwa njia za kawaida.Hata hivyo panapokuwa na hujuma zinazoendelea ndani kwa ndani hilo si ajabu kutokea.

Kuna tetesi kuwa wale waliopigania uanzishwaji wake na kupelekea furaha kwa jamii ya kiislamu na faida kubwa kwa wananchi kwa jumla walipoona wimbi la ufisadi na mbinu zao kuzidiwa na watu hao waliamua kukaa pembeni kuliko kuangalia kinachotokea.

Moja ya matawi muhimu ya benki ya Amana ni pale Mchikichini ambapo awali wafanyabiashara wakubwa wa kiislamu walijazana kuweka fedha zao. Mara kadhaa nimekwenda nikakutana na wenzangu na mie wanaokwenda kutoa sh.10000 za kununulia fungu la muhogo. Inasemekana wengi wamekerwa na uzembe unaondelea wanapohitaji huduma kwenye benki hiyo.

Ushauri kama wapo wakereketwa wa benki ya Amana waliobaki katika uongozi wa juu basi wafukuze wapuuzi wote wanaotaka kutukanisha benki hiyo hasa kwenye vitengo ya teknohama na kila inapowezekana waanze kuajiri waislamu wenyewe kwanza wenye taaluma ya vitengo husika mbali mbali vya benki hiyo.
Hii ndio shida ya kuchanganya biashara na dini
 
Back
Top Bottom