Tupeane maujanja ya Excel

VLOOKUP nimeizungumzia Kwa clip fupi kule Telegram Sijajua kama upo kule..

Kiufupi sana.. VLOOKUP Hukuwezesha kutafuta kitu chochote katika Sheet Vertically ndani ya sekunde tu...

=VLOOKUP (D10,A1:F10,4,FALSE)


D10 hii ni CELL ambayo utakuwa ukiandika jina la hiyo item unayoitafuta so inategemea Unataka ionekane wapi katika Sheet yako

A1:F10 ni data zote ambazo Unataka ziwe considered ukiangalia vizuri nimeanza na A1 hadi F10 so lazima I select data zako zote

4 hii ni Column.. Je hiyo value au price ipo katika colum ya ngapi kutoka mwanzo?

FALSE ni kuwa jina utakalo liandika li match sawasawa na unachokitafuta ukiandika TRUE inaamana ikutafutie Value yeyote ambayo inakaribiana

Bonyeza Enter na Anza ku search items katika Cell D10
naomba nami niunge huko
e47b3d1aaf9abb2fdaefe6042acbad44.jpg

Hakikisha umeandika formula pale ambapo Unataka Jumla itokee... Andika kama inavoonekana Kwenye picha halafu bonyeza enter..

Rudia mara mbili Tatu utazoea.. Usisahau kuingia Kwenye Telegram nitakuwa naweka video fupi ili ieleweke vizuri
 
Guys napenda kujua jins excel inavyolink na visual basic then mtu unaweza tengeneza buttons, entry fields. Then unatengeneza button kama clear na forms. Naomba kujua
 
  • Thanks
Reactions: Dyf
Asante Kwa Swali Lako Zuri.. Nimekuandalia Video fupi.. Nimeiweka Kwenye Group kule hakikisha umeingia... Nimejifunza swali lako lote.. Iangalie na fanya mazoezi na kama utakuwa na swali usisite kurudi hapa kuuliza

Ethos ,very good job ua doing here bro.Napata tatizo nikigonga link inaniambia ADDRESS WASNT UNDERSTOOD nashdwa kujoin.HELP PLZ
 
naomba unieleweshe kuhusu hiyo range. sijaelewa kabisa
JINSI YA KUWEKA DROP DOWN LIST

Unaweza ukataka kuweka list ambayo mtumiaji anataka achague kitu fulani na ajaze kadiri ya matumizi yako...

Kitu cha kwanza andika list ya hizo items au majina katika sehemu yeyote katika Sheet yako

Nenda Kwenye Data >>> Data Validation kitatokea kibox kidogo... Bonyeza settings halafu nenda chini Kwenye Allow chagua list kama inavoonekana hapo chini
e134da96c927d1f11e2b78fcf50cc730.jpg


Baada ya hapo Kwenye source andika range ambayo hizo items ulizoziandika zipo.. Kwa Sheet yangu ni =$F$2:$F$6
192c70d861bb3168cd636480b812db35.jpg
f74588778e817d878083006baf256793.jpg

Halafu bonyeza OK


mwisho sheet yako inatakiwa ionekane hivi
View attachment 436363
 
Mkuu Ethos mbona kule telegram kupo hujatupia nondo yeyote kwa muda sasa I think ni tangu feb. Tuwekee clip nyongine tuzid kupata madini zaidi.
 
Nashkuru kwa kushare great info kama hii!ningependa kujua pa kuanzia ile niweze kuitumia excel kwa kujiamini,kiukwel huwa napata ugumu sana!
 
Jaman wataalamu kuna tatizo moja naomba msaada.
Nina mafaili mawili; yote yamekosewa
Faili la kwanza nimechanganya watu waliopo na wasio kuwepo na namba zao za simu.
Faili la pili lina watu waliopo tu ila hakuna namba zao za simu nawezaje kurekebisha kwa haraka badala ya kupitia kila jina?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaman wataalamu kuna tatizo moja naomba msaada.
Nina mafaili mawili; yote yamekosewa
Faili la kwanza nimechanganya watu waliopo na wasio kuwepo na namba zao za simu.
Faili la pili lina watu waliopo tu ila hakuna namba zao za simu nawezaje kurekebisha kwa haraka badala ya kupitia kila jina?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama data umezipanga vizuri tumia Vlookup function

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushawahi kujifunza jinsi ya kutenganisha au kugawanya data katika excel ? yaani zilizopo katika column moja kuwa mbili ? Pata darasa kidogo hapa na nishukuru baadae...

Chagua column ambayo unataka kuigawa,

then nenda kwenye data----->> halafu utaona sehemu kwa juu imeandikwa text to columns click hapo

itatokea hivi

upload_2017-7-21_22-2-26.png



Then chagua delimited, kitakuja kitu kama hiki hapo chini. Fixed width yaani kutenganisha kwa upana fulani tutazungumzia siku ingine. Bonyeza next


upload_2017-7-21_22-6-39.png



Unaweza ukachagua kugawanya kwa kutumia space, semi colon, au alama yoyote ambayo ipo common katika column husika. Mimi hapo nimechagua kutumia dash yaani - utaona neno Jamii forums na number zimetengana. then click next

utapata kitu kama hiki hapa chini baada ya ku click finish


upload_2017-7-21_22-16-42.png



Nakaribisha maswali... Kama upo telegram usisahau kufuata link na kuingia katika group letu.

Link>>>>> Excel/SpreadsheetsTZ



Ethos.
 
Jaman wataalamu kuna tatizo moja naomba msaada.
Nina mafaili mawili; yote yamekosewa
Faili la kwanza nimechanganya watu waliopo na wasio kuwepo na namba zao za simu.
Faili la pili lina watu waliopo tu ila hakuna namba zao za simu nawezaje kurekebisha kwa haraka badala ya kupitia kila jina?

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza ukatuma screen shot nikusaidie? hapa au PM?

Au kutoa mfano zaidi?

Asante.

Ethos

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom