Tuongeze thamani ya majina yetu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
39,939
Reaction score
61,733
Unajisikiaje kutumia jina lile lile ulilopewa na wazazi wako toka udogoni mpaka unakufa nalo?

Kama tunaweza kuongeza thamani ya viwanja vyetu, mashamba, majengo n.k, ni muhimu pia kuongeza thamani ya majina yetu.

Kama mpaka umri huu, bado unatumia majina yaleyale uliyopewa na wazazi, na hujayaongezea thamani kwa kuanza na jina Dr au Prof. utaonekana bado ni mtu wa kizamani, wa karne iliyopita.

Kama tunaongezea thamani kwa kitu kilicho chakaa, ni muhimu pia kuongeza thamani ya jina lako lililochakaa.

Ingawa kuna changamoto ya kufikia hiyo thamani ya majina, wengine wanaamua kujiongezea thamani ya majina mfano mwinjilist, mchungaji, CP nini n.k

Lakini, ni muhimu kutambua, thamani ya majina yako duniani, yataongezwa na haya maneno mawili tu, Dr au Prof. Hizo zingine huwa ni mbwembwe tu.

Twendeni darasani​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…