Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,638
- 697,929
Naiandika tungo hii nikijua ya kuwa
Ni kwa wale wana kaya kuu, walio mahiri
Kabisa katika kaya iliyotukuka sana!
Wenye hekima kama wendawazimu na
Wenye busara kama vichaa nikijua fika ya kwamba hawa ndio watakuwa wa kunielewa
Ni tungo ya turufu, turufu ya mustakabali wa kaya yetu! Kaya yetu tuipendayo sana
Naiandika kwa wana kaya wote, watukuka sana! Waheshimiwa sana! Waliojikweza Kabisa! Na hata kwa wale waliolala kuzimu wasubiriao parapanda kuu, nyamafu waonao lakini hawaelewi, wasikiao lakini hawajibu, waliolala daima wakitazama upande!
Nalisema kuwa nani atudanganyae kwamba ustaarabu ni kuwa na miguu minne na kibanda cha ngazi? Kusoma mabuku mengi na kutafakari tusiyoyajua? Hakika siri za kaya hii ni nyingi na zisizoelezeka, na kamwe hatuwezi kuzifahamu zote hata kwa kutumia ujinga wa mwerevu wa bana mtwana kitwana!!!
Twalikumbuka kusahau kuwa ile kweli iitwayo kweli kuu ndio uongo na uoza unukao kuliko manukato ya yule mteule!
Natujiongopee basi ya kuwa hii iitwayo kweli kuu ndio dira yetu ituongozayo kusiko! Kwanini basi tusikae sisi kwa sisi! Sisi na wale na kusemezana wenyewe yale yatuhusuyo kama kaya...vipaumbele vyetu kanuni zetu maono yetu.....
Ni kwa wale wana kaya kuu, walio mahiri
Kabisa katika kaya iliyotukuka sana!
Wenye hekima kama wendawazimu na
Wenye busara kama vichaa nikijua fika ya kwamba hawa ndio watakuwa wa kunielewa
Ni tungo ya turufu, turufu ya mustakabali wa kaya yetu! Kaya yetu tuipendayo sana
Naiandika kwa wana kaya wote, watukuka sana! Waheshimiwa sana! Waliojikweza Kabisa! Na hata kwa wale waliolala kuzimu wasubiriao parapanda kuu, nyamafu waonao lakini hawaelewi, wasikiao lakini hawajibu, waliolala daima wakitazama upande!
Nalisema kuwa nani atudanganyae kwamba ustaarabu ni kuwa na miguu minne na kibanda cha ngazi? Kusoma mabuku mengi na kutafakari tusiyoyajua? Hakika siri za kaya hii ni nyingi na zisizoelezeka, na kamwe hatuwezi kuzifahamu zote hata kwa kutumia ujinga wa mwerevu wa bana mtwana kitwana!!!
Twalikumbuka kusahau kuwa ile kweli iitwayo kweli kuu ndio uongo na uoza unukao kuliko manukato ya yule mteule!
Natujiongopee basi ya kuwa hii iitwayo kweli kuu ndio dira yetu ituongozayo kusiko! Kwanini basi tusikae sisi kwa sisi! Sisi na wale na kusemezana wenyewe yale yatuhusuyo kama kaya...vipaumbele vyetu kanuni zetu maono yetu.....