Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,291
Hii obsession ya kumtukana Rais katika kila thread ndiyo inayowafanya nyie wenyewe mnaochangia kuishia kutukanana na hata kuharibu hadhi ya JF. Mtoa mada wa awali aliuliza kwa nini Tundu Lissu yuko kimya muda mrefu then nyie mnamrukia JK kwa lipi? Ifike mahali watu waipe heshima JF kama jukwaa la watu kujadili hoja objectively na kuzitolea hitimisho litakaloonyesha kwamba wacahngiaji wake wana akili timamu na pengine ni watu wenye familia zinazowaheshimu.
Hii hali ya kumimina matusi ama kwa watawala au kwa wachangiaji wenye mtizamo tofauti ni dalili tosha kwamba kuna watu humu hawastahili kutoa michango yao na si vibaya wakakaa kimya kuliko kugeuza hapa kuwa kituo cha kupambanisha uendawazimu. Leo hii Mwanakijiji anasifiwa kwa umahiri wa hoja zake siyo kwa jinsi anavyogundua matusi mapya kila siku. Tuache hali hii otherwise no body will take us seriously any more na hata sisi chipukizi tutajutia kujiunga.
Umenena vyema chukua takwimu za thread uone zinaanza hupindia wapi. Nimefanya zoezi hilo; kuna kundi ambalo ni mahili kuwaondoa watu kwenye hoja za msingi kwa kuwakasirisha kwa kuwazodoa hasa cdm na kuwapamba ccm. Ukweli utabaki kuwa hao ndio wenye kutumwa kwa kuhofia ya majadiliano mazuri ya JF. Kwa sababu ni ukumbi huru si vyema kuwazuia kwa hiyo kwa upande wangu naunga mkono hata wakitukanana kwa sababu watatafuta njia mbadala wa kureconcile kama ni ethical members wa JF.
Uangalizi tu. Mimi naona wengi humu hawana stadi za uandishi kwa hiyo ni lazima kuwavumilia. Lakini wengine hawana progressive objective ya hii forum wamegeuza ni uwanja wa mipasho. Yote kwa yote mimi sina matatizo nayo kwa kuwa msafara wa mamba kenge hawakosekani.
Mimi na wewe tuko nje ya mada kwa sababu ya wapuuzi. Mada ni Tundu Lisu wapuuzi wanaingiza mifarakano ndani ya CDM lazima wajibiwe period. This is a home of GREAT THINKERS not lazy thinkers who do not read between the lines.