Tundu Lissu: Viatu vya Dk. Slaa vikubwa

Tundu Lissu: Viatu vya Dk. Slaa vikubwa

Bora kaona hilo
Pengo la dk slaa ni kubwa sana.

Endeleeni kujifariji lakin uhalisia ni huo

Sumaye hawezi mchakamchaka kama ule aliokua akifanya babu.
Litazibwa tu tupo wengi kwenye chama wenye uwezo kumzidi huyo msaliti. Halafu CCM mnapolivalia njuga ndipo tunakaza misuri maana bei mliyofika kwa slaa inawauma chama kinapodunda bado.
 
Ila nyie bei mliofika kwa El na baado kasema atagombea tena
 
Litazibwa tu tupo wengi kwenye chama wenye uwezo kumzidi huyo msaliti. Halafu CCM mnapolivalia njuga ndipo tunakaza misuri maana bei mliyofika kwa slaa inawauma chama kinapodunda bado.
Hata haujulikani kwanza

Kwenye mgao wa kiingilio cha lowasa ulipata.
 
Ndo sababu wengi humu ni wajinga ingawa wanajiita Ma GT. Ukisoma maelezo ya Lissu ukalinganisha na michango ya wengi utagundua hoja za kijinga zilizojaa ushabiki badala ya mantiki.
Hakuna popote aliposema Lissu kwamba hakuna mwenye uwezo wa kujaza nafasi ya Katibu Mkuu ndani ya CHADEMA! Anachokisema Lissu ni sifa za mtu anaetakiwa kuwa Katibu wa Chama.
Dr. Slaa kuwa na uwezo haina maana alikuwa malaika asie na mapungufu, alikuwa nayo, tena mengi na ya hatari, kuna wakati tena sio mara moja mapungufu yake yalimezwa na uimara wa CHADEMA.
Ikumbukwe kwamba huyu hakuanzisha CHADEMA, alikuta chama kikiwa imara na ndio sababu kati ya vyama vyote alichagua kukimbilia CHADEMA baada ya kuchoshwa na ubabaishaji ndani ya CCM.
Ni sahihi kusema alikuja na ameacha mchango mkubwa ndani ya CHADEMA. Ni sahihi pia kusema CHADEMA kilimjenga na kumtangaza pia Dr. Slaa. Lkn mwisho wa siku hakuna aliye juu kuzidi chama.
Chama chochote hakiwezi kuwa chini mwanachama wake akawa juu, hili ni kwa vyama vyote.
Kumfanya mwanachama kuwa ni bora kuliko chama ndiko kulikoifikisha CCM hapa ilipo leo. Mfano mzuri tumeuona wakati wa uchaguzi, kwamba ilifikia mahali Mgombea Urais wa CCM kujitenga na chama, na kuwaomba wapiga kura wamchague yeye na sio chama chake!
Kwa umakini walionao CHADEMA, naamini atapatikana Katibu Mkuu makini kama ilivyokuwa kwa Slaa.
Muhimu watu wafahamu kwamba ni Mwenyekiti wa CHADEMA ndiye anapaswa kuwa makini kabla hajatamka jina la Katibu anayefaa. Sote tunaufahamu uwezo wa Mbowe, bila shaka atafanya hivyo kama alivyofanya kwa Dr. Slaa! Tusubiri!
'' Mfano mzuri tumeuona wakati wa uchaguzi, kwamba ilifikia mahali Mgombea Urais wa CCM kujitenga na chama, na kuwaomba wapiga kura wamchague yeye na sio chama chake!''
Aliacha kuimba CCM mbele kwa mbele ?Alivaa shati lenye rangi tofauti na chama chake ? Tuwe wakweli.hili misikuliona. ni propaganda zisizo na kichwa wala miguu.
 
8485_1023665931031198_6203437645497960529_n.jpg
kama viatu ni vikubwa dawa ni kumshawishi arudi avivae mwenyewe na kuna namna moja tu ya kumshawishi ili arudi nayo si nyingine bali kukiondoa mara moja kile kilichosababisha kuondoka kwake.
 
Dr slaa hakufukuzwa CHADEMA. ...Alijitoa kwa ridhaa yake mwenyewe.CHADEMA Inaheshimu mchango wake uliotukuka ila inasikitishwa na kufikia kwake BEI
 
Colours za lissu ni opportunistic asie na msimamo
 
Si muisoma habari nzima ndio mtoa mate hapa!

Wasomi wazuri wanapopewa majukum makubwa, mara nyingi huwapamba watangulizi wao katika nafasi zao mpya. Sio kweli kuwa Lissu anaona nafasi ya ukatibu mkuu ni kubwa na haiwezi kuifanya kama.alivyoifanya Dr. Slaa, bali ni lugha ya kuheshimu mchango wa mtangulizi wake. (kama akipewa/kama kunafununu za kupewa jukumu hilo)
 
Aliyoyasema Lissu ni kweli!
Nimefurahi kuona kwa mbali watu wanaanza kuheshimu michango ya wenzao hata kama walifarakana!
Chadema,cuf na ccm wamekuwa na kasumba za kudharau juhudi za watu waliowafanyia kazi na kuwekeza muda, mali na utu wao ili kuendeleza vyama!
James Mapalala, Lowasa, Slaa, Zitto, kingunge etc ni baadhi ya watu walioonja shubiri za siasa uchwara za watanzania!
Kama Lissu ameanza kuheshimu, ni vema nasi sote tujaribu kuiga utamaduni huu mpya wa CDM na Lissu in particular!
 
Ni rahisi sana kubomoa.Slaa alejenga msingi,mafisadi walikiogopa chadema,sasa hivi mafisadi wanaiogopa ccm,chadema ndio kimbilio la mafisadi na watu wajanja wajanja.
Enzi za Slaa,Lema asingeruhusiwa kuropoka hovyo,na angefanya hivyo chama kisingethubutu,kuteketeza ruzuku yake kumtetea Lema na mkewe kwa matamshi yao ambayo hawakutumwa na chama
 
Back
Top Bottom