Uchaguzi 2020 Tundu Lissu umekuwa mtu wa mikwara na kuongea sana, tunaomba matendo. Anza na wabunge walioenguliwa

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,210
42,072
Wanajamvi wasalaam,

Kwanza kabisa ni ukweli ulio wazi hadi sasa CCM wana mtaji wa wabunge 20 na kwa takwimu za jana hadi mwisho wa kutoa majibu ya Rufani nina uhakika CCM itapita bila kupingwa kwenye majimbo sio chini ya 50!

Rais Tundu Lissu amekuwa akipiga mikwara ya kuingiza watu barabarani kila leo lakini hatuoni vitendo na kila leo amekuwa akipiga mikwara kuwa ataingiza watu barabarani lakini hakuna mtu anayeingizwa barabarani bali ni ulaghai tu.

Hivi jamani Devotha Minja na wabunge wa CHADEMA walikosea kujaza fomu kwa sababu hawajui Kiingereza au Kiswahili?

Mh Rais Lissu, tunaomba uingize watu barabarani wabunge wako wengi hadi sasa wameliwa vichwa!

Wasalaam
 
Kama unataka kuingia barabarani si uingie tu? Eti unasubiri Lissu akuingize barabarani.
 
Come on now Ruttashobolwa, we as CHADEMA have survived the past 20+ years under extreme oppression under every single president of this country. We know Voting Meko out will not change our condition.

But again No President from the Green will change our condition to the better, therefore we must change the ruling system or suffer the consequences later.
 
Umoja wa wanawake CCM mna tabu nyie, first time lissu anatamka hayo mkasema jamaa anahatarisha amani ya nchi, ajabu Leo Huyo huyo uliyepiga kelele amani inahatarishwa ndo wa kwanza kumkumbusha lissu aingie road!
 
Sisi ni ndugu na Marafiki,Tunaishi pamoja na Tumeoleana,Familia moja kuna wana ccm na wengine Chadema

Siasa sio mpira wa simba na Yanga wa kufanya mizaha

Mkuu toa ushauri nini kifanyike kuboresha maendeleo ya nchi hii hususani maisha ya watu

Kuleta ngonjera,udaku,mipasho na maneno ya makungwi wakata shombo ni aibu kwa mwana ccm mwezetu

Manatuabisha na mnakiabisha chama cha mapinduzi kuandika mambo ya mipasho na taarabu
 
Kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri ni kawaida, ila kuuficha ujinga ni kipaji ambacho wanacho watu wachache tu! Huelewi unachofanya, na naelewa unafanya dhiaka, lakini kwenye bonge la bichwa ulilo nalo kuna ubongo wa kukutosha, na akili unazo, tatizo ni kiwango unachotumia kwenye akili yote aliyokupa mwenyenzi Mungu!
 
Pumba tupu ,tukiwaabia CCM maji ya shingo mnakataa Dua na uchawi was nini sasa.
IMG_20200908_223449.jpg
 
Maccm hawawezi kutufundisha game plan. Subiri tufike mahali sahihi ujionee. Unataka tukurupuke ili muibe vizuri na kujifanya tulihamia barabarani tukaacha mchakato?

Ngoja arobaini ya mwizi ifike halafu uone kama hata utapata muda wa kuingia kwenye mtandao hapa kuropoka ujinga.
 
Sisi ni ndugu na Marafiki,Tunaishi pamoja na Tumeoleana,Familia moja kuna wana ccm na wengine Chadema

Siasa sio mpira wa simba na Yanga wa kufanya mizaha

Mkuu toa ushauri nini kifanyike kuboresha maendeleo ya nchi hii hususani maisha ya watu

Kuleta ngonjera,udaku,mipasho na maneno ya makungwi wakata shombo ni aibu kwa mwana ccm mwezetu

Manatuabisha na mnakiabisha chama cha mapinduzi kuandika mambo ya mipasho na taarabu
Amani ni zao la haki, kusipokuwa haki usitegemee amani, anza sasa kuzungumzia haki
 
Back
Top Bottom