masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Masikini Tundu Lissu, amerudi toka ughaibuni sasa.
Lakini si kishujaa!
Lalamiko lake la kwanza alipoonana na Mama Samia huko Ubelgiji, ilikuwa pesayake, mafao.
Ni kweli mlo hata kwa mwanasiasa ni muhimu, ataishije?
Mambo ya siasa yakawa secondary, hayakuwa na umuhimu sana kwake.
Mama Samia kaondoa fitna za kisiasa zilizoachwa na mtangulizi wake, Magufuli.
Sasa Mbowe yuko huru, Lissu karudi Bongo.
Lakini mapokezi ya Lissu yamekuwa ile wazungu wanasema , lukewarm, vuguvugu, na si motomoto.
Hilo Lissu hajui, nimatokeo ya mama Samia kukubalika kwa wananchi walio wengi, ukilinganisha na mwendazake.
Hivyo hata sababu za kumpinga mama wazi wazi hzionekani kuwa na maana sana.
Lissu( na CHADEMA) akubali asikubali, playing field imebadilika sana.
Sasa Lissu anazunguka mikoani akilia kama Yohana Mbatizaji.
Lakini yeye hana njia yoyote ya kuonyesha, njia nzuri kuliko ya CCM na mama Samia.
Na hilo ndo paradox.
Lissu kadoda, hana jipya.
Ile confrontational style yake haina tija kwake wala kwa siasa za Tanzania.
Namshauri akubali tu kuwa a political backbencher, asuburi aone upepo kwanza.
Kwa sasa hivi Lissu is irrelevant.