Tundu Lissu: Siwafahamu walionipiga risasi

Tundu Lissu: Siwafahamu walionipiga risasi

Mh Lisu katumia busara, kusema hawa fahamu hao watu na hiyo yote kupunguza maswali na shauku ya watu kutaka kujua. Mh Lisu anajua ataanzisha kitu kipya akisema anawafahamu. Ngoja arudi tutajua mbivu na mbichi
 
Tundu Lissu katika hilo la kuwataja waliomshambulia kazingatia ushauri aliopewa na "wadau" wake.Hakika ilikuwa ni kujiweka mahali pa hatari sana kusema kuwa waliomshambulia anawajua wakati bado yupo juu ya kitanda hospitalini,ilikuwa ni hatari kwake na kwa dereva wake.

Tunashukuru kuwa sasa kwa kinywa chake,ametujengea picha kujua "ushahidi wa kimazingira" wa wahusika.Nyumba ni za serikali,majirani zake ni viongozi wa bunge na serikali,huku Naibu Waziri na kule Naibu Spika.Tena katika eneo lenye CCTV masaa 24.

Ni ajabu kuwa mpaka sasa,hata jirani yake Naibu Spika hajafika kumjulia hali mbunge,kiongozi mwenzake wa bunge na jirani yake nje ya bunge.Tulisema hapa,matibabu sio hisani bali ni haki yake,lakini sababu kuna muhimili mmoja umejichimbia chini zaidi,muhimili mwingine unaongozwa tu kwa "remote control".Aibu sana

Ni bahati mbaya kuwa hata wale walio na propaganda,wametoa video ya Makamu wa Rais na Lissu katika lile eneo ambalo Lissu anamwambia VP mwambie Rais nashukuru sana,lakini wakaacha pale alipomuuliza "Ni kweli Rais kakutuma au umepitia tu baada ya kuja kwenye sherehe za kuapishwa?".Kama kakutuma,basi mwambie Mh.Rais nashukuru sana.

Lakini hawajaeleza Pindi Chana aliulizwaje?Kwamba toka September 07 mpaka leo ndio unakuja??Lissu amekuwa very technical kwenye haya mahojiano.Jambo jema...

Ahadi ya kijasiri ni ile ya kusema atarudi na kuongeza nguvu zaidi,maana upendo wa Watanzania kwake imekuwa ni deni kubwa.Lissu na kauli zake,amenirudisha tena JF

Na wewe umeamini hilo?
 
Mbowe ndio ameshushuka sio au?
Halafu ndie anayejua wenzake waliohusika.

Kwahiyo mboye ndiyo aliye mshambulia? vip wale polisi wanaolinda masaa24?
Lissu alisema katika mlango wa Waziri Kalemani, kuangalia block ya Naibu Spika Dk Tulia, kuna camera za CCTV zinazofanya kazi Saa 24 hivyo kwa mtu yeyote ambaye yupo eneo hilo anaonekana, lakini akasema kuna vitu vinaashiria kuwa kunahitajika jicho la pili kuangalia hili.

Alisema polisi imewazuia watu wasisali, wasimwombee Mungu apone, watu wasimchangie damu, kusiwe na dalili zozote za wazi za kumuunga mkono na huyu ambaye ameshambuliwa na watu wanasemekana hawajulikani.
KAMA NI MBOYE BASI ANATISHA.
 
Dakika ya 11:44'' ya video clip hii inatakiwa itolewe taarifa maalum na vyombo vya usalama kuwa ktk CCTV kamera ndani ya makazi ya viongozi mjini Dodoma wameona nini, hawajaona nini na sababu ya kutoona chochote maana bila hivyo kuna maswali mengine yanaulizwa juu ya ukimya wa vyombo vya usalama.
 
Hili swala ni zito sana. Familia ndio inajua machungu yake na yeye mwenyewe. Wengine ni porojo tu
 
Mara paap Lisu katimkia CCM...900 itapendeza bavicha wote wataharisha siku hyo 😀😀😀😀😀

Tusitegee hilo, hivi sasa ama chance kubwa ya kutwaa madaraka yaa juu ya chadema bila ya kupinga NA Mzee Mtei, Lowasa NA Mbowe hawawezi kumzuia.

Leo Lissu ama support kubwa sana ndani ya chadema, akija ccm atambulia uwaziri NA umaarufu wake utakwisha
 
Maswa 1 , Siyabonga101 , dudus,

Lissu alisema wiki tatu kabla ya shambulio hilo alilalamika hadharani kwamba anafuatiliwa kila anapokwenda na siku moja aliwasimamisha watu hao katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro na kuwauliza sababu za kufanya hivyo.

“Niliwauliza kwa nini wananifuata na kama kuna mtu kawatuma, mwambieni mimi si mhalifu. Lakini sikupewa ulinzi wowote,” alisema.
Taarifa hutolewa kwa utaratibu upi?
 
Hili swala la kutumia polisi kila kitu lingekoma, tufike mahali watu tubishane kwa hoja kama hatuelewani basi yaishie hapo au kura zipigwe kuamua jambo, tabia hii ya kila kitu polisi imejengeka sana katika nchi yetu, watawala wamekuwa hawana uwezo wa kudebate hata kwa kitu kidogo, hoja ijibiwe kwa hoja, polisi haiwezi wasaidia kujibu hoja, hii ni nchi yetu sote hakuna haja ya kupigana mabovu kwa sababu ya madaraka.

Uchaguzi polisi wanaingia wanapiga watu,wanarusha mabomu kama kuna vita kuna shida gani ? tume inawalinda, mahakama, wakurugenzi, wakuu wa mikoa bado tena mnatumia polisi kupiga au kutawanya watu?, itafika kipindi watu wataona wakoloni walikuwa nafuu kuliko tawala za sasa hivi.
 
Taarifa hutolewa kwa utaratibu upi?

..hakuna utaratibu maalum au rasmi wa kutoa taarifa kwa Polisi.

..kwa mfano, TL hajawahi kutoa taarifa "rasmi" kuwa amepigwa risasi.

..sasa mbona IGP alijitokeza kwenye vyombo vya habari na kudai anachunguza?
 
Mh Lisu katumia busara, kusema hawa fahamu hao watu na hiyo yote kupunguza maswali na shauku ya watu kutaka kujua. Mh Lisu anajua ataanzisha kitu kipya akisema anawafahamu. Ngoja arudi tutajua mbivu na mbichi
We unamsemea?
 
Mnataka aseme anawafahamu ili wamrudie

Huwezi kusema unawajua bila ya kutoa ushahidi unaothibitisha unachokidai.

Mimi naamini kweli hawajui hao watu.

Ila pia naamini kuna anaowahisi kuwa ndo wahusika, kwa namna moja ama nyingine.

Suala la kujua linahusiana na ushahidi na uthibitishaji. Sasa anaweza kweli kuthibitisha endapo atasema huyu na yule ndo wahusika? Ngumu sana!
 
Huwezi kusema unawajua bila ya kutoa ushahidi unaothibitisha unachokidai.

Mimi naamini kweli hawajui hao watu.

Ila pia naamini kuna anaowahisi kuwa ndo wahusika, kwa namna moja ama nyingine.

Suala la kujua linahusiana na ushahidi na uthibitishaji. Sasa anaweza kweli kuthibitisha endapo atasema huyu na yule ndo wahusika? Ngumu sana!
Sasa anko ake sabrina
 
Anaeleza, Tundu Lissu maneno yanayo fikirisha.

"Kimawazo nadhani sijabadilika sana, Lissu wa kabla ya September 7 na Lissu wa Leo kimsimamo wa kisiasa hajabadilika kabisa. Lazima tupiganie demokrasia, hiyo ndiyo salama yetu . Tuwe na utawala wa kidemokrasia unao jali haki za binadamu, tuwe na utawala wa sheria, tuwe na mfumo wa uongozi unaojali maisha ya wananchi, unao wajibika kwa wananchi au kwa wawakilishi wake na huu ndio msimamo wangu unajulikana na bado upo vile vile"

Ujumbe kutoka kwa mkewe, Alice Lissu.

"Ujumbe wangu, Tundu siku zote aendelee kuwa Tundu tu. Tundu wa kabla ya tukio na baada ya tukio awe ni Tundu niliyemjua siku zote.

Nini Maoni Yako?

Ndimi, Noel Shao
[HASHTAG]#mjenziWaTanzaniaMpya[/HASHTAG]

Maoni yangu ni kwamba anamwunga Rais Magufuli 100% kwa utawala wake wa kidemokrasia unao jali haki za binadamu, utawala wa sheria, uongozi unaojali maisha ya wananchi, unao wajibika kwa wananchi au kwa wawakilishi wake na huu ndio msimamo wake Lissu unaojulikana na bado upo vile vile, kwa maneno yake mwenyewe.

Ninavyomwelewa Lissu anafanya kazi sahihi ya upinzani kuikosoa Serikali kuelekea utawala bora, tofauti na viongozi wenzake wa upinzani ambao agenda yao kubwa ni matukio. Hata shambulizi lake limekuwa mtaji wa kisiasa. Kwamba msimamo wake umemjengea maadui ndani na nje ya chama chake. Laiti Serikali ingeliliona hilo, na kumwekea ulinzi, huenda asingeshambuliwa
 
Lissu amekuwa chanzo cha hela za magazet now days every day ni new story about him sasa huyu jamaa apone tuuuuuuuuuuuu propaganda zimezidi
 
bora ata ungekaa kimya ingeleta busara katika jambo ambalo lilihitaji muhusika na shambulizi kukaa kimya lakini nashangaa umekurupuka na kushangilia duuh aisee kweli akili ni nywele
 
Back
Top Bottom