chimwemwe67
Member
- Mar 11, 2015
- 69
- 44
Katiba ya Chama chochote cha Siasa au kinginecho au sheria yoyote inayomzuia mtu yeyote kwenda Mahakamani kudai haki yake kwa kuona kama imekiukwa au inaelekea kukiukwa, katiba au Sheria hiyo ni batili tangu mwanzo wake (Null and void ab initio).
Ieleweke kuwa sheria yoyote inayotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au katiba ya Chama chochote kiwe cha Siasa au kijamii au kikundi chochote cha watu haipaswi kuwa juu ya/ au kukiuka matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ibara husika ya Katiba ya CHADEMA ni kandamizi na imekiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho ya mara kwa mara. Hata hivyo nawashangaa sana wananchi katika suala hili maana Mahakama haijatoa uamuzi juu ya uanachama wa Zitto Kabwe ndani ya CHADEMA bali imetupilia mbali kesi yake kwa kuunga mkono pingamizi la awali (P.O) la mawakili wa CHADEMA kwamba kulikuwa na makosa ya kisheria kufungua kesi hiyo kwenye Mahakama kuu ya Tanzania tena kwenye masjala kuu ya Mahakama kuu ya Tanzania (Main Registry of the High Court of Tanzania) badala ya Masjala ya Wilaya ya Mahakama hiyo (District Registry of the High Court of Tanzania)
Na kwamba kesi hiyo ingefunguliwa kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi.
Mimi sipendi kuzungumzia uamuzi wa Mahakama kwenye forum hii maana maadili ya kazi zangu na taaluma yangu hayaniruhusu ila ninachotaka kufanya ni kumkosoa kaka yangu, msomi mwenzangu Tundu Lissu kwamba si kweli kwamba tangu Zitto alipofungua kesi yake mahakamani dhidi ya CHADEMA basi alikuwa si mwanachama tena wa CHADEMA kutokana na ibara ya katiba ya CHADEMA inavyosema, maana kama ingekuwa hivyo basi Zitto asingehudhuria Bungeni tangu tarehe 2/1/2014 lakini mbona ameendelea kuwa Mbunge hadi leo na hata siku zijazo mpaka utaratibu wa kisheria utakapofuatwa?
Yeye Tundu ni nani hadi kutamka kwamba Zitto si mbunge tena wa Kigoma Kaskazini kama alivyotamka jana mbele ya waandishi wa habari? Why souldn't he leave this matter to the proper authorities?
Hata kama Zitto akikoma kuwa Mbunge ni kwa mujibu wa katiba na Sheria za nchi na si kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA hasa kwa Ibara hiyo inayozuia mwanachama wa CHADEMA kwenda Mahakamani maana Ibara hiyo ni batili na kinyume cha Katiba ya nchi.
Zitto bado ana fursa kubwa ya kwenda mahakama ya Rufaa kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi huo wa mahakama kuu na ni haki yake kuendelea na ubunge wake wakati akisubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambacho ni chombo cha juu kabisa cha maamuzi juu ya haki za watu hapa Tanzania.
Kwa msomi wa sheria na wakili mkongwe kama Tundu Lissu kukurupuka kwa hisia za kisiasa na kuropoka juu ya hatima ya Zitto ndani ya CHADEMA mimi naona kama ni tukano kwa taaluma hii ya kifalme (It is an abuse to this noble profession).
Taaluma hii sasa imeingiliwa na wanasiasa uchwara ambao wanaweza kusimama na kutamka lolote ili mradi tu wakidhi hoja zao za kisiasa badala ya kwenda kwenye uhalisia wa kisheria. Ndiyo maana hata Ngeleja ambaye kitaaluma ni mwanasheria alipohojiwa na baraza la tume ya maadili ya viongozi katika kutoa utetezi wake anajitetea kuwa eti siyo yeye tu aliyepokea hela za escrow bali pia hata Zitto Kabwe naye alipokea kutoka sehemu kadha wa kadha.
Uliona wapi mwanasheria wa kweli anatoa utetezi wa aina hiyo? Can somebody justfy wrongs because the same have been commited/done by somebody else? Unaua mtu kwa sababu fulani naye kaua? Hao ndo wanasheria dizaini ya Tundu Lissu, wanajua lakini wanajifanya hawajui ili kujustify position na kiu zao za kisiasa.
Mwisho Zitto nakupa nguvu uamue mambo haya kwa utashi wako mwenyewe. Ikiwa unaona unahitaji kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi wa mahakama kuu kutoka katika mahakama ya rufaa Tanzania sisi tupo tayari kukusaidia hata bure kabisa tukiungana na Wakili Msomi Alberto Msando ili tafsri hiyo isiwe kwa manufaa yako tu bali kwa kizazi chote cha Tanzania.
Ni katika Mahakama ya rufaa tunaweza kupata maelekezo juu ya katiba mbovu za vyama kama CHADEMA zinazofifisha haki za watu/ wanachama wake kukishitaki chama wakati hilo ni takwa na haki ya kikatiba. Kuwa mwanamapinduzi kunahitaji moyo na muda.
Usikate tamaa, kama ni chama chao waachie kidizaini lakini twende Mahakama ya Rufaa tupate tafsri sahihi, na je Mahakama kuu kuendelea na kesi yako bila kutoa notisi kwako au kwa wakili wako kama tarehe ya kusikiliza ilibadilishwa kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari ilikuwa sahihi(kama ni kweli)?
Hayo ndo mambo ya muhimu watanzania wangependa kujua na si longolongo za kisiasa kama za Tundu Lissu na wenzake wenye mtazamo kama huo.
Aluta Continua Comrade Zitto Zuberi Kabwe. Demokrasia ya kweli lazima izingatie sheria na Katiba za Nchi zilizo nzuri zisizokiuka haki za watu. Si sheria zote ni Sheria!
Ieleweke kuwa sheria yoyote inayotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au katiba ya Chama chochote kiwe cha Siasa au kijamii au kikundi chochote cha watu haipaswi kuwa juu ya/ au kukiuka matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ibara husika ya Katiba ya CHADEMA ni kandamizi na imekiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho ya mara kwa mara. Hata hivyo nawashangaa sana wananchi katika suala hili maana Mahakama haijatoa uamuzi juu ya uanachama wa Zitto Kabwe ndani ya CHADEMA bali imetupilia mbali kesi yake kwa kuunga mkono pingamizi la awali (P.O) la mawakili wa CHADEMA kwamba kulikuwa na makosa ya kisheria kufungua kesi hiyo kwenye Mahakama kuu ya Tanzania tena kwenye masjala kuu ya Mahakama kuu ya Tanzania (Main Registry of the High Court of Tanzania) badala ya Masjala ya Wilaya ya Mahakama hiyo (District Registry of the High Court of Tanzania)
Na kwamba kesi hiyo ingefunguliwa kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi.
Mimi sipendi kuzungumzia uamuzi wa Mahakama kwenye forum hii maana maadili ya kazi zangu na taaluma yangu hayaniruhusu ila ninachotaka kufanya ni kumkosoa kaka yangu, msomi mwenzangu Tundu Lissu kwamba si kweli kwamba tangu Zitto alipofungua kesi yake mahakamani dhidi ya CHADEMA basi alikuwa si mwanachama tena wa CHADEMA kutokana na ibara ya katiba ya CHADEMA inavyosema, maana kama ingekuwa hivyo basi Zitto asingehudhuria Bungeni tangu tarehe 2/1/2014 lakini mbona ameendelea kuwa Mbunge hadi leo na hata siku zijazo mpaka utaratibu wa kisheria utakapofuatwa?
Yeye Tundu ni nani hadi kutamka kwamba Zitto si mbunge tena wa Kigoma Kaskazini kama alivyotamka jana mbele ya waandishi wa habari? Why souldn't he leave this matter to the proper authorities?
Hata kama Zitto akikoma kuwa Mbunge ni kwa mujibu wa katiba na Sheria za nchi na si kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA hasa kwa Ibara hiyo inayozuia mwanachama wa CHADEMA kwenda Mahakamani maana Ibara hiyo ni batili na kinyume cha Katiba ya nchi.
Zitto bado ana fursa kubwa ya kwenda mahakama ya Rufaa kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi huo wa mahakama kuu na ni haki yake kuendelea na ubunge wake wakati akisubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambacho ni chombo cha juu kabisa cha maamuzi juu ya haki za watu hapa Tanzania.
Kwa msomi wa sheria na wakili mkongwe kama Tundu Lissu kukurupuka kwa hisia za kisiasa na kuropoka juu ya hatima ya Zitto ndani ya CHADEMA mimi naona kama ni tukano kwa taaluma hii ya kifalme (It is an abuse to this noble profession).
Taaluma hii sasa imeingiliwa na wanasiasa uchwara ambao wanaweza kusimama na kutamka lolote ili mradi tu wakidhi hoja zao za kisiasa badala ya kwenda kwenye uhalisia wa kisheria. Ndiyo maana hata Ngeleja ambaye kitaaluma ni mwanasheria alipohojiwa na baraza la tume ya maadili ya viongozi katika kutoa utetezi wake anajitetea kuwa eti siyo yeye tu aliyepokea hela za escrow bali pia hata Zitto Kabwe naye alipokea kutoka sehemu kadha wa kadha.
Uliona wapi mwanasheria wa kweli anatoa utetezi wa aina hiyo? Can somebody justfy wrongs because the same have been commited/done by somebody else? Unaua mtu kwa sababu fulani naye kaua? Hao ndo wanasheria dizaini ya Tundu Lissu, wanajua lakini wanajifanya hawajui ili kujustify position na kiu zao za kisiasa.
Mwisho Zitto nakupa nguvu uamue mambo haya kwa utashi wako mwenyewe. Ikiwa unaona unahitaji kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi wa mahakama kuu kutoka katika mahakama ya rufaa Tanzania sisi tupo tayari kukusaidia hata bure kabisa tukiungana na Wakili Msomi Alberto Msando ili tafsri hiyo isiwe kwa manufaa yako tu bali kwa kizazi chote cha Tanzania.
Ni katika Mahakama ya rufaa tunaweza kupata maelekezo juu ya katiba mbovu za vyama kama CHADEMA zinazofifisha haki za watu/ wanachama wake kukishitaki chama wakati hilo ni takwa na haki ya kikatiba. Kuwa mwanamapinduzi kunahitaji moyo na muda.
Usikate tamaa, kama ni chama chao waachie kidizaini lakini twende Mahakama ya Rufaa tupate tafsri sahihi, na je Mahakama kuu kuendelea na kesi yako bila kutoa notisi kwako au kwa wakili wako kama tarehe ya kusikiliza ilibadilishwa kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari ilikuwa sahihi(kama ni kweli)?
Hayo ndo mambo ya muhimu watanzania wangependa kujua na si longolongo za kisiasa kama za Tundu Lissu na wenzake wenye mtazamo kama huo.
Aluta Continua Comrade Zitto Zuberi Kabwe. Demokrasia ya kweli lazima izingatie sheria na Katiba za Nchi zilizo nzuri zisizokiuka haki za watu. Si sheria zote ni Sheria!