Smartboy
JF-Expert Member
- Nov 12, 2010
- 1,110
- 128
Mh. Tundu Lissu amemwuliza Ngeleja kuhusu kampuni ya madini ambayo imechukua maeneo ya wakazi wa Singida Mashariki bila fidia na kujenga kiwanja cha ndege kwenye mashamba ya wananchi.
Na akamwuliza kwanini serikali haijachukua hatua ikiwemo kuwafungulia mashtaka hao wawekezaji. Ngeleja amekanusha na kusema kampuni imemilikishwa kisheria.
Lissu ameomba mwongozo na kutaja kifungu kinachohusu kudanganya bungeni na kusema waziri amedanganya. Kama kawaida Anne Makinda amemwambia akafanye uchunguzi alete huo uongo bungeni.
Hapa patamu ngoja tuone au wataizima kama ile ya Lema.
Na akamwuliza kwanini serikali haijachukua hatua ikiwemo kuwafungulia mashtaka hao wawekezaji. Ngeleja amekanusha na kusema kampuni imemilikishwa kisheria.
Lissu ameomba mwongozo na kutaja kifungu kinachohusu kudanganya bungeni na kusema waziri amedanganya. Kama kawaida Anne Makinda amemwambia akafanye uchunguzi alete huo uongo bungeni.
Hapa patamu ngoja tuone au wataizima kama ile ya Lema.