Tundu Lissu: Mahakama Zetu Haziaminiki kimataifa

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,321
24,228


Atoa mfano wa ndege ya airbus kukamatwa Uholanzi baada ya baraza la usuluhishi la kimataifa kuona mwekezaji alipwe fidia kwa mkataba uliovunjwa na serikali.

Jopo la waamuzi huwa na watu watatu, mmoja huteuliwa na serikali/mdaiwa yaani Tanzania, mjumbe wa pili huteuliwa na mwekezaji na wa tatu huteuliwa kwa makubaliano baina ya serikali na mwekezaji na huyu huwa ndiyo mwenyekiti wa tribunal anabainisha Tundu Lissu.

Tundu Lissu anazidi kutuelimisha kuwa wawekezaji huweka sharti kuwa kukitokea mgogoro basi waende kwenye hii tribunal / baraza la kimataifa kupata suluhisho. Maana wawekezaji wanafahamu kuwa mahakama zetu na majaji wake hawapo huru.

Tanzania imesaini mikataba na nchi nyingi ambazo ni wadau wa maendeleo kuwa kukitokea kutoelewana baina ya wawekezaji toka Mataifa hayo na Tanzania basi utatuzi utatafutwa katika Baraza hilo la kimataifa la biashara / uwekezaji kupata suluhu au kulipwa fidia.

Hivyo kelele kuwa inakuwaje ndege zetu zinakamatwa kiholela siyo za kweli. Maana wakati wa kuingia mkataba na wawekezaji mambo yote huwekwa hadharani na pia Tanzania imesaini mikataba ya maridhiano ya kimataifa kuwa mchakato gani ufuatwe kukitokea kadhia kama hii ya mwekezaji wa shamba la miwa Bagamoyo kugeukwa dakika ya mwisho baada ya mkataba kuwekwa.

Tundu Lissu anaongeza kuwa maamuzi ya Tribunal hii ya usuluhishi yanatambulika kama maamuzi ya mahakama yoyote ulimwengu na Tanzania ikiridhia hivyo ili kukazia hukumu ya baraza hilo, basi Mali za mdaiwa zinaweza kukamatwa kokote kule kulipo nchi zilizoafikia mikataba hii ya kimataifa.

Tundu Lissu baada ya kuweka sawa nini kimepelekea ndege za serikali yaani airbus a220-300 kukamatwa anasema kuwa ....


1670170633989.png
icsid.worldbank.org
https://icsid.worldbank.org › about
About ICSID - World Bank

ICSID is the world's leading institution devoted to international investment dispute settlement. It has extensive experience in this field
 
Wakili Harold Sungusa : Serikali imetunga sheria nyingi za kujilinda badala ya zile za kutoa haki ndiyo maana tuna Mawakili goigoi wa serikali, ambao hawawezi kushinda kesi kimataifa. Mfumo mzima wa haki na ule wa jinai haki hauwafanyi Mawakili/ wanasheria na waendesha mashtaka kuwa na umahiri, weledi katika kazi


 
BIT ni mikataba ya hadharani kwani ni moja na nchi nyingine Tafadhali Watanzania tumieni mtandao kujielimishi
 
Ukitaja kujua BIT ya nchi kama Switzerland na Tanzania iko wazi mtandaoni just google it please Tanzanian use the internet efficiently
 
Jopo la maamuzi huwa na watu watatu, mmoja huteuliwa na serikali/mdaiwa yaani Tanzania, mjumbe wa pili huteuliwa na mwekezaji na wa tatu huteuliwa kwa makubaliano baina ya serikali na mwekezaji na huyu huwa ndiyo mwenyekiti wa tribunal anabainisha Tundu Lissu.
Na hisi serikali yetu ilipeleka mwakilishi Adv Kidando nguli wa ushahidi wa kupika mahakamani
 
Duuh.....sa itakuwaje

Kila siku tunaambiwa tuwe na mahakama huru, waendesha mashtaka huru, wanasheria wa serikali huru, bunge huru la kupitisha sheria za haki, mihimili ya dola huru yaani Bunge, Mahakama na dola / Executive rais asiwe mithili ya mfalme bali afuate sheria za haki asiwe mtu wa matamko, mtoa pesa zote, mjenga barabara ya kitongoji n..k CCM hawatuelewi wanataka kusifu, kuabudu na kutukuza uvunjajwi wa sheria, katiba, mikataba kisa amri toka juu.

Sasa mihimili yote ya dola la Tanzania yaani Bunge, Mahakama na taasisi ya urais haviaminiki ndani ya nchi na kimataifa .

Bunge la wabunge ambao hawajachaguliwa na wananchi 2020, majaji wanaoonekana ni makada wa CCM, serikali inayofuata sera za kibaguzi kubagua vyama vingine vilivyosajiliwa kwa mujibu wa sheria na kutambulika kikatiba vinazuiliwa kufanya shughuli za siasa ....... wananchi kubomolewa nyumba Kimara DSM bila fidia, Rugemalila Singh plea & bargaining , shamba la miwa Bagamoyo, Stein mkulima wa Afrika ya Kusini, uchafuzi wa uchaguzi 2020, ... listi ni ndefu

Victory Attorneys & Consultants
https://victoryattorneys.co.tz › plea-...
Plea Bargaining Arrangement: The Inevitable Law In Tanzania

Plea bargaining refers to the process whereby an accused and public prosecutor reach a mutual agreement without going through long court


UHAMIAJI - TUNACHUNGUZA URAIA WA ERICK KABENDERA

 
Back
Top Bottom