Tundu Lissu karibu CCM

Tundu Lissu karibu CCM

mtwa mkulu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2013
Posts
8,585
Reaction score
11,260
images (21).jpeg


Awali ya yote namshukuru Mungu Mwenyezi Mwenye Nguvu zote aliyotenda Muujiza ambao kila mtanzania mwenye macho aliona. Uhai wako ulikuwa kitu Cha thamani sana kwa sababu maalumu.

Kwaniaba ya Chama Changu Cha Kidemokrasia, Chama Cha Mapinduzi niseme maneno machache karibu CCM. Karibu uitumie taaluma yako kuwatumikia watanzania, karibu kwenye Mfumo wa Utawala.

Tunatambua taaluma yako na uwezo mkubwa wa kisiasa ulio nao muheshimiwa. Lakini ukiwa na nia njema ya kuwapigania watanzania na kuwaletea ukombozi dhidi ya CCM ile ya Mafisadi, CCM ya majizi, kwa huzuni kubwa uliangukia mikononi mwa wahuni... Wahuni walio diriki hata kuzurumu Roho yako kwa kutuma migambo wahuni wasiokuwa na mafunzo ya siraha. Wahuni wasiokuwa na democracy ya kweli ndani yao, wasio kuwa na mipango... Wamejawa na ukabila.

Muheshimiwa, umesikia maneno ya Lema... Wewe lema unamjua! Binamu wa ile familia isiyogusika, amekunanga na kukudharau... Hiyo ndiyo CDM iliyopoteza muelekeo, inayoishi kwa kuwadanganya watanzania, wanataka wakutumie kama bigijii..wanahofu majimboni mwao! Lissu wabaya wako umewajua, Mimi na wewe tumesoma Evidence law wabaya wako umewajua!

Lissu usiogope kuyala matapishi yako, wewe uliwahi kutabiri wakati wa awamu ya nne kuwa hii nchi inahitaji rais dikteta. Karibu uungane na rais dikteta upige kazi. Karibu uungane na kamanda Aliyewahi kuwa key figure wa siasa za mapinduzi Dr Slaa, karibu uwatumikie watanzania.Hata yule Tumbili wa Escrow tupo nae huku!

Karibu Chama chenye Democrasia, kinachotoa vyeo kwa watu wenye sifa na sio kwa unyanyasaji wa kingono na uhawala.

Tumesamehe yote, Chama chetu hakina kisasi Wala kinyongo na wewe, sisi sio kama wale, Tutaondoa mazingira magumu mahakamani na kwa thamani yako tutakuandalia mazingira mazuri. Pole sana Lissu.
Naimani utanijibu

KARIBU TANZANIA, KARIBU CCM
 
Bangi mbaya na pesa pia mbaya yaani mtu anaongea pumba hadharan kisa dola
 
Katika nchi maskini kama hii muda wakuandika upuuzi unautoa wapi?
 
Ccm tumeshawachoka ,Tundu lissu hana PhD fake hawezi kujiunga (Mataga=Make-Tanzania-great-again
 
Ni wewe, halafu edit huo uzi wako ujisemee mwenyewe Nani kakuambia Kuna mwana CCM mwingine anamtaka huyo mliberali? Kama unamtaka mkaribishe nyumbani kwako mnywe nae chai.
Kaa pembeni Kwanza kuna battle ya wakubwa hapa hauiwezi
 
Habari njema kabisa hii, karibu sana cde Mh. Tundu Lissu. Tunakukaribisha kwa mikono miwili chamani. Tena itapendeza sana ili kuwakomoa hao mabeberu wanaodhani tunanunulika kwa bei chee.
 
Mmeona tunamkubali Tundu Lissu na hakuna namna Magufuli anaweza kumshinda kwa kura, mmeona bora mumuahidi vyeo ili ahamie ccm! Kwa bahati mbaya tunamkubali maana yuko upinzani, ila ikitokea akahamia ccm hata yeye tutampotezea kama tulivyompotezea Slaa. Kamuiteni Slaa tuliyekuwa tunamkubali huko nyuma, kama sasa hivi anaweza kuwavutia tena wale waliokuwa wanamkubali.

Ni hivi, hatuitaki ccm kwa mazuri na mabaya yake yote. Ifahamike kila kizazi kina chama chake, ccm sio chama cha kizazi hiki, hata muinunue cdm yote iwe ccm, bado hamuwezi kutufanya tuikubali ccm. Najisini box la kura mtakavyo, lakini kizazi hiki hakiko na ccm kwa lolote, sana sana mtutumia shuruti kutawala, lakini sio kwa ridhaa ya wengi hasa vijana.
 
Mmeona tunamkubali Tundu Lissu na hakuna namna Magufuli anaweza kumshinda kwa kura, mmeona bora mumuahidi vyeo ili ahamie ccm! Kwa bahati mbaya tunamkubali maana yuko upinzani, ila ikitokea akahamia ccm hata yeye tutampotezea kama tulivyompotezea Slaa. Kamuiteni Slaa tuliyekuwa tunamkubali huko nyuma, kama sasa hivi anaweza kuwavutia tena wale waliokuwa wanamkubali.

Ni hivi, hatuitaki ccm kwa mazuri na mabaya yake yote. Ifahamike kila kizazi kina chama chake, ccm sio chama cha kizazi hiki, hata muinunue cdm yote iwe ccm, bado hamuwezi kutufanya tuikubali ccm. Najisini box la kura mtakavyo, lakini kizazi hiki hakiko na ccm kwa lolote, sana sana mtutumia shuruti kutawala, lakini sio kwa ridhaa ya wengi hasa vijana.
Nakubaliana na ww Mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom