mtwa mkulu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2013
- 8,585
- 11,260
Awali ya yote namshukuru Mungu Mwenyezi Mwenye Nguvu zote aliyotenda Muujiza ambao kila mtanzania mwenye macho aliona. Uhai wako ulikuwa kitu Cha thamani sana kwa sababu maalumu.
Kwaniaba ya Chama Changu Cha Kidemokrasia, Chama Cha Mapinduzi niseme maneno machache karibu CCM. Karibu uitumie taaluma yako kuwatumikia watanzania, karibu kwenye Mfumo wa Utawala.
Tunatambua taaluma yako na uwezo mkubwa wa kisiasa ulio nao muheshimiwa. Lakini ukiwa na nia njema ya kuwapigania watanzania na kuwaletea ukombozi dhidi ya CCM ile ya Mafisadi, CCM ya majizi, kwa huzuni kubwa uliangukia mikononi mwa wahuni... Wahuni walio diriki hata kuzurumu Roho yako kwa kutuma migambo wahuni wasiokuwa na mafunzo ya siraha. Wahuni wasiokuwa na democracy ya kweli ndani yao, wasio kuwa na mipango... Wamejawa na ukabila.
Muheshimiwa, umesikia maneno ya Lema... Wewe lema unamjua! Binamu wa ile familia isiyogusika, amekunanga na kukudharau... Hiyo ndiyo CDM iliyopoteza muelekeo, inayoishi kwa kuwadanganya watanzania, wanataka wakutumie kama bigijii..wanahofu majimboni mwao! Lissu wabaya wako umewajua, Mimi na wewe tumesoma Evidence law wabaya wako umewajua!
Lissu usiogope kuyala matapishi yako, wewe uliwahi kutabiri wakati wa awamu ya nne kuwa hii nchi inahitaji rais dikteta. Karibu uungane na rais dikteta upige kazi. Karibu uungane na kamanda Aliyewahi kuwa key figure wa siasa za mapinduzi Dr Slaa, karibu uwatumikie watanzania.Hata yule Tumbili wa Escrow tupo nae huku!
Karibu Chama chenye Democrasia, kinachotoa vyeo kwa watu wenye sifa na sio kwa unyanyasaji wa kingono na uhawala.
Tumesamehe yote, Chama chetu hakina kisasi Wala kinyongo na wewe, sisi sio kama wale, Tutaondoa mazingira magumu mahakamani na kwa thamani yako tutakuandalia mazingira mazuri. Pole sana Lissu.
Naimani utanijibu
KARIBU TANZANIA, KARIBU CCM